Cha Pili cha Wafalme
24 Katika siku za Yehoyakimu, Mufalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuja kumushambulia, na Yehoyakimu akakuwa mutumishi wake kwa miaka tatu (3). Hata hivyo, alimugeuka na akaasi. 2 Kisha Yehova akaanza kutuma vikundi vya wanyanganyi Wakaldayo,+ Wasiria, Wamoabu, na Waamoni vikuje kumushambulia. Aliendelea kutuma vikundi hivyo vishambulie Yuda na kuiharibu, kulingana na neno lenye Yehova+ alikuwa amesema kupitia watumishi wake manabii. 3 Hakika ilikuwa kwa agizo la Yehova kwamba mambo hayo yalipata Yuda, ili kuwaondoa mbele ya macho yake+ kwa sababu ya zambi zote zenye Manase alikuwa ametenda,+ 4 na pia damu yenye haina kosa yenye alikuwa amemwanga,+ kwa maana alikuwa amejaza Yerusalemu damu yenye haina kosa na Yehova hakutaka kusamehe.+
5 Na mambo mengine ya historia ya Yehoyakimu, mambo yote yenye alifanya, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda?+ 6 Kisha Yehoyakimu akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake;+ na Yehoyakini mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.
7 Mufalme wa Misri hakutoka tena hata siku moja katika inchi yake, kwa maana mufalme wa Babiloni alikuwa amekamata vitu vyote vyenye vilikuwa vya mufalme wa Misri,+ kuanzia kwenye Bonde* la Muto la Misri+ mupaka kwenye Muto Efrati.+
8 Yehoyakini+ alikuwa na miaka kumi na munane (18) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miezi tatu (3) katika Yerusalemu.+ Jina la mama yake lilikuwa Nehushta binti ya Elnatani wa Yerusalemu. 9 Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, kulingana na mambo yote yenye baba yake alikuwa amefanya. 10 Wakati huo watumishi wa Mufalme Nebukadneza wa Babiloni walipanda kuja kushambulia Yerusalemu, na muji huo ukazungukwa kwa ajili ya vita.+ 11 Mufalme Nebukadneza wa Babiloni alikuja kwenye muji wakati watumishi wake walikuwa wanauzunguka kwa ajili ya vita.
12 Mufalme Yehoyakini wa Yuda akatoka inje kuenda kwa mufalme wa Babiloni,+ pamoja na mama yake, watumishi wake, wakubwa wake, na watu wenye cheo kwenye makao yake;+ na mufalme wa Babiloni akamukamata mateka katika mwaka wa munane (8) wa utawala wake.+ 13 Kisha akakamata kutoka pale hazina zote za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mufalme.+ Akakata vipande-vipande vyombo vyote vya zahabu vyenye Sulemani mufalme wa Israeli alikuwa ametengeneza katika hekalu la Yehova.+ Jambo hilo lilitokea kama vile Yehova alikuwa ametabiri. 14 Akapeleka katika uhamisho Yerusalemu yote, wakubwa wote,+ wapiganaji-vita wote wenye nguvu, na kila fundi na kila mwenye kufua chuma*+—alipeleka katika uhamisho watu elfu kumi (10 000). Hakuna mutu yeyote mwenye alibakia isipokuwa watu maskini sana wa inchi.+ 15 Basi akakamata Yehoyakini+ na kumupeleka katika uhamisho Babiloni;+ akapeleka pia mama ya mufalme, bibi za mufalme, maofisa wa makao ya mufalme, na watu wa kwanza katika inchi, akawakamata kutoka Yerusalemu na kuwapeleka katika uhamisho Babiloni. 16 Mufalme wa Babiloni alikamata pia na kupeleka katika uhamisho Babiloni wapiganaji-vita wote, elfu saba (7 000), na pia mafundi na wenye kufua chuma* elfu moja (1 000), wote walikuwa wanaume wenye nguvu na wenye wamezoezwa kwa ajili ya vita. 17 Mufalme wa Babiloni alimufanya Matania, ndugu ya baba ya Yehoyakini,+ kuwa mufalme pa nafasi yake na akabadilisha jina lake kuwa Sedekia.+
18 Sedekia alikuwa na miaka makumi mbili na moja (21) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na moja (11) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 19 Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, kulingana na mambo yote yenye Yehoyakimu alikuwa amefanya.+ 20 Ni kwa sababu ya kasirani ya Yehova kwamba mambo hayo yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, mupaka wakati aliwatupa kutoka mbele ya macho yake.+ Na Sedekia akamuasi mufalme wa Babiloni.+