Cha Pili cha Wafalme
7 Sasa Elisha akasema: “Musikilize neno la Yehova. Yehova anasema hivi: ‘Kesho karibu na wakati huu kwenye mulango mukubwa wa* samaria, kipimo kimoja cha sea* cha unga muzuri kitakuwa na bei ya shekeli* moja, na vipimo mbili vya sea vya shayiri vitakuwa na bei ya shekeli moja.’”+ 2 Halafu kamanda musaidizi mwenye mufalme alitegemea akamuambia hivi ule mutu wa Mungu wa kweli: “Hata kama Yehova anafungua milango mikubwa ya maji mengi ya mbinguni, je, kweli jambo* hilo linaweza kutokea?”+ Naye akasema, “Utaona jambo hilo kwa macho yako mwenyewe,+ lakini hautakula vyakula hivyo.”+
3 Kulikuwa watu ine (4) wenye ukoma kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa muji,+ na wakaambiana: “Sababu gani tunakaa hapa mupaka tukufe? 4 Kama tunasema, ‘Tuingie katika muji,’ wakati kuko njaa katika muji,+ tutakufia mule. Na kama tunakaa hapa, tutakufa tu. Basi sasa tuende kwenye kambi ya Wasiria. Kama wanalinda uzima wetu, tutaishi, lakini kama wanatuua, basi tutakufa.” 5 Kwa hiyo wakasimama wakati wa giza la mangaribi na wakaingia katika kambi ya Wasiria. Wakati walifika inje ya kambi ya Wasiria, hapakukuwa mutu yeyote.
6 Kwa maana Yehova alikuwa amefanya kambi ya Wasiria isikie sauti ya magari ya vita na farasi, sauti ya jeshi kubwa.+ Basi wakaambiana: “Angalia! Mufalme wa Israeli amekodi wafalme wa Wahiti na wafalme wa Misri ili wakuje kutushambulia!” 7 Mara moja wakasimama na kukimbia wakati wa giza la mangaribi, wakaacha mahema yao, farasi wao, punda wao, na kambi yote kama vile vilikuwa, na wakakimbia ili kuokoa uzima wao.*
8 Wakati watu hao wenye ukoma walifika inje ya kambi hiyo, wakaingia ndani ya hema moja na wakaanza kula na kunywa. Wakabeba feza, zahabu, na nguo kutoka mule na wakaenda na kuvificha. Kisha wakarudia na kuingia katika hema ingine na wakabeba vitu kutoka mule na wakaenda na kuvificha.
9 Mwishowe wakaambiana: “Jambo lenye tunafanya haliko muzuri. Leo ni siku ya habari njema! Kama tunasita na kungojea mupaka mapambazuko,* tutastahili azabu. Sasa tuende tuambie nyumba ya mufalme habari hii.” 10 Basi wakaenda na kusema kwa sauti kubwa na walinzi wa milango mikubwa ya muji na kuwaambia: “Tulienda katika kambi ya Wasiria, lakini hapakukuwa mutu—hatukusikia sauti ya mutu yeyote. Kulikuwa tu farasi na punda wenye kufungwa na mahema yenye yaliachwa kama vile yalikuwa.” 11 Mara moja wale walinzi wa milango mikubwa wakaita, na habari hiyo ikajulishwa ndani ya nyumba ya mufalme.
12 Mara moja mufalme akaamuka usiku na kuambia watumishi wake: “Tafazali, muache niwaambie mambo yenye Wasiria wametutendea. Wanajua kwamba tuko na njaa,+ kwa hiyo walitoka katika kambi ili kujificha katika eneo la mashamba, wakisema, ‘Watatoka katika muji, na tutawakamata wakiwa wazima na kuingia katika muji.’”+ 13 Kisha mumoja wa watumishi wake akasema: “Tafazali, acha wanaume fulani wakamate farasi tano (5) kati ya wale wenye wanabakia, wenye wako katika muji. Angalia! Wao watakuwa sawa tu na kikundi chote cha watu wa Israeli wenye kubakia hapa. Angalia! Wao watakuwa sawa tu na kikundi chote cha watu wa Israeli wenye waliangamia. Basi tuwatume waende na tuone.” 14 Basi wakakamata magari mbili pamoja na farasi, na mufalme akawatuma kwenye kambi ya Wasiria, na kusema: “Muende na muone.” 15 Wakawafuata mupaka kwenye Yordani, na njia yote ilikuwa inajaa nguo na vyombo vyenye Wasiria walikuwa wametupa wakati walikuwa wanakimbia kwa woga. Wale wajumbe wakarudia na wakamuambia mufalme habari hiyo.
16 Kisha watu wakatoka na kunyanganya vitu katika kambi ya Wasiria, na hivyo kipimo kimoja cha sea cha unga muzuri kikakuwa na bei ya shekeli moja, na vipimo mbili vya sea vya shayiri vikakuwa na bei ya shekeli moja, kulingana na neno la Yehova.+ 17 Mufalme alikuwa ameweka ule kamanda musaidizi mwenye alitegemea, akuwe musimamizi wa mulango mukubwa, lakini watu wakamukanyanga-kanyanga kwenye mulango mukubwa mupaka akakufa, kama vile ule mutu wa Mungu wa kweli alikuwa amemuambia mufalme wakati alishuka kwake. 18 Ilitendeka kama vile ule mutu wa Mungu wa kweli alikuwa amemuambia mufalme: “Vipimo mbili vya sea vya shayiri vitakuwa na bei ya shekeli moja, na kipimo kimoja cha sea cha unga muzuri kitakuwa na bei ya shekeli moja kesho wakati huu kwenye mulango mukubwa wa Samaria.”+ 19 Lakini ule kamanda musaidizi alikuwa amemuambia ule mutu wa Mungu wa kweli: “Hata kama Yehova anafungua milango mikubwa ya maji mengi ya mbinguni, je, jambo hilo* linaweza kutokea?” Na Elisha alikuwa amesema: “Utaona jambo hilo kwa macho yako mwenyewe, lakini hautakula vyakula hivyo.” 20 Ni vile kabisa mambo yalimufikia, kwa maana watu walimukanyanga-kanyanga kwenye mulango mukubwa mupaka akakufa.