Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
4 Wana wa Yuda walikuwa Perezi,+ Hezroni,+ Karmi, Huru,+ na Shobali.+ 2 Reaya mwana wa Shobali akamuzaa Yahati; Yahati akazaa Ahumai na Lahadi. Hizo ndizo zilikuwa familia za Wasorati.+ 3 Hawa ndio walikuwa wana wa baba ya Etamu:+ Yezreeli, Ishma, na Idbashi (na jina la dada yao lilikuwa Haselelponi), 4 na Penueli alikuwa baba ya Gedori, na Ezeri alikuwa baba ya Husha. Hao ndio walikuwa wana wa Huru,+ muzaliwa wa kwanza wa Efrata na baba ya Betlehemu.+ 5 Ashuri+ baba ya Tekoa+ alikuwa na bibi wawili, Hela na Naara. 6 Naara akamuzalia Ahuzamu, Heferi, Temeni, na Haahashtari. Hao ndio walikuwa wana wa Naara. 7 Na wana wa Hela walikuwa Sereti, Ishari, na Etnani. 8 Kosi akamuzaa Anubu, Zobeba, na familia za Aharheli mwana wa Harumi.
9 Yabesi aliheshimiwa kuliko ndugu zake; na mama yake alimupatia jina Yabesi,* na kusema: “Nilimuzaa kwa maumivu.” 10 Yabesi akamuitia Mungu wa Israeli, kwa kusema: “Kama tu ungenibariki na kupanua eneo langu na uache mukono wako ukuwe pamoja na mimi na uniokoe kutoka katika musiba, ili musiba huo usiniumize!” Basi Mungu akatimiza ombi lake.
11 Kelubu ndugu ya Shuha akamuzaa Mehiri, mwenye alikuwa baba ya Eshtoni. 12 Eshtoni akamuzaa Bet-rafa, Pasea, na Tehina, baba ya Ir-nahashi. Hao ndio walikuwa wanaume wa Reka. 13 Na wana wa Kenasi walikuwa Otnieli+ na Seraya, na mwana* wa Otnieli alikuwa Hatati. 14 Meonotai akamuzaa Ofra. Seraya akamuzaa Yoabu baba ya Ge-harashimu,* waliitwa vile kwa sababu walikuwa mafundi.
15 Wana wa Kalebu+ mwana wa Yefune walikuwa Iru, Ela, na Naamu; na mwana* wa Ela alikuwa Kenasi. 16 Wana wa Yehaleleli walikuwa Zifu, Zifa, Tiria, na Asareli. 17 Wana wa Ezra walikuwa Yeteri, Meredi, Eferi, na Yaloni; alipata* mimba na akamuzaa Miriamu, Shamai, na Ishba baba ya Eshtemoa. 18 (Na bibi yake Muyahudi alimuzaa Yeredi baba ya Gedori, Heberi baba ya Soko, na Yekutieli baba ya Zanoa.) Hao ndio walikuwa wana wa Bitia, binti ya Farao, mwenye Meredi alioa.
19 Wana wa bibi ya Hodia, dada ya Nahamu, walikuwa baba za Keila Mugarmi na Eshtemoa Mumaakati. 20 Na wana wa Shimoni walikuwa Amnoni, Rina, Ben-hanani, na Tiloni. Na wana wa Ishi walikuwa Zoheti na Ben-zoheti.
21 Wana wa Shela+ mwana wa Yuda walikuwa Eri baba ya Leka, Laada baba ya Maresha, na familia za watu wa nyumba ya Ashbea wenye kufanya kazi za kusuka vitambaa vya muzuri, 22 na Yokimu, wanaume wa Kozeba, Yoashi, na Sarafi, wenye walikuwa bwana za wanamuke Wamoabu, na Yashubi-lehemu. Habari hizi ni za zamani.* 23 Walikuwa wafinyanzi* wenye waliishi katika Netaimu na Gedera. Waliishi kule na walimutumikia mufalme.
24 Wana wa Simeoni+ walikuwa Nemueli, Yamini, Yaribu, Zera, na Shauli.+ 25 Shalumu alikuwa mwana wake, Mibsamu mwana wake, na Mishma mwana wake. 26 Na wana wa Mishma walikuwa Hamueli mwana wake, Zakuri mwana wake, Shimei mwana wake. 27 Na Shimei alikuwa na watoto wanaume kumi na sita (16) na watoto wanamuke sita (6); lakini ndugu zake hawakukuwa na watoto wengi wanaume, na hakuna familia yao yoyote yenye ilikuwa na watoto wengi wanaume kama vile watu wa Yuda.+ 28 Waliishi Beer-sheba,+ Molada,+ Hasar-shuali,+ 29 Bilha, Esemu,+ Toladi, 30 Betueli,+ Horma,+ Siklagi,+ 31 Bet-markaboti, Hasar-susimu,+ Bet-biri, na Shaaraimu. Hiyo ilikuwa miji yao mupaka wakati wa utawala wa Daudi.
32 Makao yao yalikuwa Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni, na Ashani,+ miji tano (5), 33 pamoja na makao yao yenye kuzunguka miji hiyo pande zote mupaka Baali. Hayo ndiyo maandikisho yao kulingana na ukoo wao na mahali kwenye waliishi. 34 Na Meshobabu, Yamleki, Yosha mwana wa Amazia, 35 Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia mwana wa Seraya mwana wa Asieli, 36 na Elioenai, Yaakoba, Yeshohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya, 37 na Ziza mwana wa Shifi mwana wa Aloni mwana wa Yedaya mwana wa Shimri mwana wa Shemaya; 38 watu hao wenye kutajwa kwa majina ndio walikuwa wakubwa katika familia zao, na hesabu ya nyumba ya mababu zao ikaongezeka. 39 Na walienda kwenye muingilio wa Gedori, kwenye upande wa mashariki wa bonde, ili kutafuta malisho kwa ajili ya makundi yao. 40 Mwishowe walipata malisho ya muzuri yenye majani mengi, na inchi ilikuwa kubwa, yenye utulivu, na yenye amani. Watu wenye waliishi pale zamani walikuwa Wahamu.+ 41 Watu hao wenye majina yao yametajwa walikuja katika siku za Mufalme Hezekia+ wa Yuda na wakapiga mahema ya Wahamu na Wameunimu wenye walikuwa kule. Waliwaharibu mupaka leo; na wakakaa mahali pao kwa sababu pale kulikuwa malisho kwa ajili ya makundi yao.
42 Wasimeoni fulani, wanaume mia tano (500), walienda kwenye Mulima Seiri+ wakiwa na Pelatia, Nearia, Refaya, na Uzieli, wana wa Ishi wenye waliwaongoza. 43 Na wakapiga na kuua Waamaleki+ wenye walibakia wenye walikuwa wameponyoka, na wamekuwa wakiishi kule mupaka leo.