Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
5 Hawa ndio wana wa Rubeni,+ muzaliwa wa kwanza wa Israeli. Yeye ndiye alikuwa muzaliwa wa kwanza, lakini kwa sababu alichafua kitanda cha baba yake,+ haki yake ya muzaliwa wa kwanza ilipewa wana wa Yosefu+ mwana wa Israeli, kwa hiyo hakuandikishwa kulingana na ukoo kwa ajili ya haki ya muzaliwa wa kwanza. 2 Hata kama Yuda+ alikuwa na mamlaka kuliko ndugu zake na kiongozi alitoka kwake,+ haki ya muzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu. 3 Wana wa Rubeni muzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ 4 Wana wa Yoeli walikuwa Shemaya mwana wake, Gogu mwana wake, Shimei mwana wake, 5 Mika mwana wake, Reaya mwana wake, Baali mwana wake, 6 na Beera mwana wake, mwenye Mufalme Tilgat-pilneseri+ wa Ashuru alikamata na kupeleka katika uhamisho; alikuwa mukubwa wa Warubeni. 7 Ndugu zake kulingana na familia zao katika maandikisho ya ukoo kulingana na wazao wao walikuwa, Yeieli, akiwa kichwa, Zekaria, 8 na Bela mwana wa Azazi mwana wa Shema mwana wa Yoeli, mwenye aliishi katika Aroeri+ na mupaka Nebo na Baal-meoni.+ 9 Upande wa mashariki alikaa mupaka mahali kwenye jangwa linaanzia kwenye Muto Efrati,+ kwa maana mifugo yao ilikuwa imeongezeka katika inchi ya Gileadi.+ 10 Katika siku za Sauli, walipigana vita na Wahagri, na Wahagri wakashindwa mbele yao, basi wakakaa katika mahema yao katika eneo lote lenye kuwa upande wa mashariki wa Gileadi.
11 Sasa wazao wa Gadi waliishi karibu nao katika inchi ya Bashani mupaka Saleka.+ 12 Yoeli ndiye alikuwa kichwa, Shafamu alikuwa wa pili, na Yanai na Shafati katika Bashani. 13 Na ndugu zao wa jamaa za upande wa baba walikuwa Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia, na Eberi, wote walikuwa saba (7). 14 Hao ndio walikuwa wana wa Abihaili mwana wa Huri mwana wa Yaroa mwana wa Gileadi mwana wa Mikaeli mwana wa Yeshishai mwana wa Yahdo mwana wa Buzi. 15 Ahi mwana wa Abdieli mwana wa Guni alikuwa kichwa cha jamaa yao ya upande wa baba. 16 Waliishi katika Gileadi,+ katika Bashani+ na miji yake ya pembeni-pembeni,* na katika malisho yote ya Sharoni kufikia kwenye miisho yake. 17 Wote waliandikishwa kulingana na ukoo katika siku za Mufalme Yotamu+ wa Yuda na katika siku za Mufalme Yeroboamu*+ wa Israeli.
18 Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase walikuwa na wapiganaji-vita wenye nguvu elfu makumi ine na ine mia saba makumi sita (44 760) katika jeshi lao wenye kubeba ngao na panga na walikuwa na pinde,* na walikuwa wamezoezwa katika vita. 19 Walipigana vita na Wahagri,+ Yeturi, Nafishi,+ na Nodabu. 20 Na walisaidiwa ili kupigana nao, na hivyo Wahagri na wote wenye walikuwa pamoja nao walitiwa katika mukono wao, kwa maana waliita Mungu awasaidie katika vita, na alijibu ombi lao kwa sababu walimutegemea.+ 21 Walikamata mifugo yao—ngamia elfu makumi tano (50 000), kondoo elfu mia mbili makumi tano (250 000), na punda elfu mbili (2 000)—na pia watu* elfu mia moja (100 000). 22 Wengi walianguka wakiwa wameuawa, kwa sababu Mungu wa kweli ndiye alipigana vita hiyo.+ Na walikaa mahali pao mupaka wakati wa uhamisho.+
23 Wazao wa nusu ya kabila la Manase+ waliishi katika inchi kuanzia Bashani mupaka Baal-hermoni na Seniri na Mulima Hermoni.+ Walikuwa wengi. 24 Hawa ndio walikuwa vichwa vya jamaa zao za upande wa baba: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia, na Yahdieli; walikuwa wapiganaji-vita wenye nguvu, wanaume wenye kujulikana sana, na vichwa vya jamaa zao za upande wa baba. 25 Lakini walitenda kwa kukosa uaminifu kumuelekea Mungu wa mababu zao na wakafanya ukahaba na miungu ya vikundi vya watu wa inchi,+ wenye Mungu alikuwa ameharibu kutoka mbele yao. 26 Basi Mungu wa Israeli akachochea roho ya Mufalme Pulu wa Ashuru+ (ni kusema, Mufalme Tilgat-pilneseri+ wa Ashuru) na hivyo akakamata na kupeleka katika uhamisho Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase, na akawapeleka Hala, Habori, Hara, na muto Gozani,+ na wako kule mupaka leo hii.