Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
2 Hawa ndio walikuwa wana wa Israeli:+ Rubeni,+ Simeoni,+ Lawi,+ Yuda,+ Isakari,+ Zabuloni,+ 2 Dani,+ Yosefu,+ Benyamini,+ Naftali,+ Gadi,+ na Asheri.+
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela. Binti ya Shua, mwanamuke Mukanaani,+ ndiye alimuzalia hao watatu (3). Lakini Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, hakumupendeza Yehova, kwa hiyo Yeye akamuua.+ 4 Tamari,+ binti-mukwe wa Yuda, alimuzalia Perezi+ na Zera. Wana wote wenye Yuda alikuwa nao walikuwa tano (5).
5 Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Etani, Hemani, Kalkoli, na Dara. Wote walikuwa tano (5).
7 Mwana* wa Karmi alikuwa Akari,* mwenye aliletea Israeli musiba,*+ mwenye alikosa uaminifu kuhusiana na kitu chenye kilikuwa kimewekwa kwa ajili ya uharibifu.+
8 Mwana* wa Etani alikuwa Azaria.
9 Wana wa Hezroni wenye walizaliwa kwake walikuwa Yerahmeeli,+ Ramu,+ na Kelubai.*
10 Ramu akamuzaa Aminadabu.+ Aminadabu akamuzaa Nashoni+ mukubwa wa wazao wa Yuda. 11 Nashoni akamuzaa Salma.+ Salma akamuzaa Boazi.+ 12 Boazi akazaa Obedi. Obedi akamuzaa Yese.+ 13 Yese akamuzaa muzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu,+ wa tatu (3) Shimea,+ 14 wa ine (4) Netaneli, wa tano (5) Radai, 15 wa sita (6) Ozemu, na wa saba (7) Daudi.+ 16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili.+ Wana wa Seruya walikuwa Abishai,+ Yoabu,+ na Asaheli,+ watatu (3). 17 Abigaili akamuzaa Amasa,+ na baba ya Amasa alikuwa Yeteri Mwishmaeli.
18 Kalebu* mwana wa Hezroni akazaa wana kupitia Azuba bibi yake na kupitia Yerioti; na hawa ndio walikuwa wana wake: Yesheri, Shobabu, na Ardoni. 19 Wakati Azuba alikufa, Kalebu alimuoa Efrati,+ na akamuzalia Huru.+ 20 Huru akamuzaa Uri. Uri akamuzaa Bezaleli.+
21 Kisha Hezroni akalala na binti ya Makiri+ baba ya Gileadi.+ Alimuoa wakati alikuwa na miaka makumi sita (60), na akamuzalia Segubu. 22 Segubu akamuzaa Yairi,+ mwenye alikuwa na miji makumi mbili na tatu (23) katika inchi ya Gileadi.+ 23 Kisha wakati fulani Geshuri+ na Siria+ wakakamata Hawot-yairi+ kutoka kwao, pamoja na Kenati+ na miji yake ya pembeni-pembeni,* miji makumi sita (60). Wote hao walikuwa wazao wa Makiri baba ya Gileadi.
24 Kisha kifo cha Hezroni+ katika Kalebu-efrata, Abiya bibi ya Hezroni akamuzalia Ashuri,+ baba ya Tekoa.+
25 Wana wa Yerahmeeli muzaliwa wa kwanza wa Hezroni walikuwa Ramu muzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya. 26 Yerahmeeli alikuwa na bibi mwingine, mwenye jina lake lilikuwa Atara. Alikuwa mama ya Onamu. 27 Wana wa Ramu muzaliwa wa kwanza wa Yerahmeeli walikuwa Maazi, Yamini, na Ekeri. 28 Wana wa Onamu walikuwa Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri. 29 Jina la bibi ya Abishuri lilikuwa Abihaili, mwenye alimuzalia Abani na Molidi. 30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu. Lakini Seledi alikufa bila kuwa na wana. 31 Mwana* wa Apaimu alikuwa Ishi. Na mwana* wa Ishi alikuwa Sheshani, na mwana* wa Sheshani alikuwa Alai. 32 Wana wa Yada ndugu ya Shamai walikuwa Yeteri na Yonatani. Lakini Yeteri alikufa bila kuwa na wana. 33 Wana wa Yonatani walikuwa Peleti na Zaza. Hao ndio walikuwa wazao wa Yerahmeeli.
34 Sheshani hakukuwa na watoto wanaume, alikuwa na watoto wanamuke tu. Sasa Sheshani alikuwa na mutumishi Mumisri mwenye jina lake lilikuwa Yarha. 35 Sheshani akamutoa binti yake akuwe bibi ya Yarha mutumishi wake, na akamuzalia Atai. 36 Atai akamuzaa Natani. Natani akamuzaa Zabadi. 37 Zabadi akamuzaa Eflali. Eflali akamuzaa Obedi. 38 Obedi akamuzaa Yehu. Yehu akamuzaa Azaria. 39 Azaria akamuzaa Helezi. Helezi akamuzaa Eleasa. 40 Eleasa akamuzaa Sismai. Sismai akamuzaa Shalumu. 41 Shalumu akamuzaa Yekamia. Yekamia akamuzaa Elishama.
42 Wana wa Kalebu*+ ndugu ya Yerahmeeli walikuwa Mesha muzaliwa wake wa kwanza, mwenye alikuwa baba ya Zifu, na wana wa Maresha baba ya Hebroni. 43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema. 44 Shema akamuzaa Rahamu baba ya Yorkeamu. Rekemu akamuzaa Shamai. 45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni. Maoni alikuwa baba ya Bet-suri.+ 46 Efa suria* wa Kalebu alimuzaa Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akamuzaa Gazezi. 47 Wana wa Yahdai walikuwa Regemu, Yotamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafu. 48 Maaka suria* wa Kalebu alizaa Sheberi na Tirhana. 49 Kisha wakati fulani akazaa Shaafu baba ya Madmana+ na Sheva baba ya Makbena na Gibea.+ Binti ya Kalebu+ alikuwa Aksa.+ 50 Hao ndio walikuwa wazao wa Kalebu.
Wana wa Huru+ muzaliwa wa kwanza wa Efrata+ walikuwa Shobali baba ya Kiriat-yearimu,+ 51 Salma baba ya Betlehemu,+ na Harefu baba ya Bet-gaderi. 52 Shobali baba ya Kiriat-yearimu alikuwa na wana: Haroe na nusu ya Wamenuhoti. 53 Familia za Kiriat-yearimu zilikuwa Waitri,+ Waputu, Washumati, na Wamishra. Wasorati+ na Waeshtaoli+ walitoka kwa hao. 54 Wana wa Salma walikuwa Betlehemu,+ Wanetofa, Atrot-bet-yoabu, na nusu ya Wamanahati, na Wazori. 55 Familia za waandishi wenye waliishi Yabesi zilikuwa Watirati, Washimea, na Wasukati. Hao walikuwa Wakeni+ wazao wa Hamati baba wa nyumba ya Rekabu.+