Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
18 Kisha wakati fulani, Daudi alishinda Wafilisti na akawaweka chini ya mamlaka yake na akakamata Gati+ na miji yake ya pembeni-pembeni* kutoka katika mikono ya Wafilisti.+ 2 Kisha akashinda Moabu,+ na Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakaleta ushuru.+
3 Daudi akamushinda Mufalme Hadadezeri+ wa Soba+ karibu na Hamati+ wakati alikuwa anaenda kufanya imara mamlaka yake kwenye Muto Efrati.+ 4 Daudi akakamata magari elfu moja (1 000), wapanda-farasi elfu saba (7 000), na maaskari elfu makumi mbili (20 000) wenye kutembea kwa miguu.+ Kisha Daudi akakata farasi wote wa magari mishipa ya magoti lakini akaacha mia moja (100) kati yao.+ 5 Wakati Wasiria wa Damasko walikuja kumusaidia Mufalme Hadadezeri wa Soba, Daudi alipiga na kuua Wasiria elfu makumi mbili na mbili (22 000).+ 6 Kisha Daudi akaweka kambi za kijeshi katika Siria ya Damasko, na Wasiria wakakuwa watumishi wa Daudi na wakaleta ushuru. Yehova alimupatia Daudi ushindi* kila mahali kwenye alienda.+ 7 Tena, Daudi alikamata ngao za muviringo za zahabu kutoka kwa watumishi wa Hadadezeri na akazileta Yerusalemu. 8 Kutoka Tibhati na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alikamata shaba nyingi sana. Sulemani aliitumia ili kutengenezea ile Bahari ya Shaba,+ nguzo, na vyombo vya shaba.+
9 Wakati Mufalme Tou wa Hamati alisikia kwamba Daudi alikuwa ameshinda jeshi lote la Mufalme Hadadezeri+ wa Soba,+ 10 mara moja akatuma Hadoramu mwana wake kwa Mufalme Daudi ili aulize hali yake na kumupongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumushinda (kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana na Tou mara nyingi), na alimuletea Daudi kila namna ya vyombo vya zahabu, feza, na shaba. 11 Mufalme Daudi akatakasa vitu hivyo kwa ajili ya Yehova,+ pamoja na ile feza na ile zahabu yenye alikuwa amekamata kutoka kwa mataifa yote: kutoka kwa Edomu na Moabu, kutoka kwa Waamoni,+ Wafilisti,+ na Waamaleki.+
12 Abishai+ mwana wa Seruya+ akapiga na kuua Waedomu elfu kumi na munane (18 000) katika Bonde la Chumvi.+ 13 Akaweka kambi za kijeshi katika Edomu, na Waedomu wote wakakuwa watumishi wa Daudi.+ Yehova alimupatia Daudi ushindi* kila mahali kwenye alienda.+ 14 Daudi akaendelea kutawala Israeli yote,+ na alikuwa anatenda haki na uadilifu* kwa ajili ya watu wake wote.+ 15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mukubwa wa jeshi,+ Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alikuwa karani, 16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiatari walikuwa makuhani, na Shavsha alikuwa mwandishi. 17 Benaya mwana wa Yehoyada alisimamia Wakereti+ na Wapeleti.+ Na wana wa Daudi walikuwa na cheo cha kwanza kisha mufalme.