Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
20 Kwenye mwanzo wa mwaka,* wakati wafalme wanaenda katika mapambano ya kijeshi, Yoabu+ akaongoza wanajeshi katika vita na akaharibu inchi ya Waamoni; akakuja na kuzunguka Raba kwa ajili ya vita,+ wakati Daudi alibakia katika Yerusalemu.+ Yoabu akashambulia Raba na kuibomoa.+ 2 Kisha Daudi akaondoa taji la Malkamu kutoka kwenye kichwa chake, na akapata kwamba lilikuwa na uzito wa talanta moja* ya zahabu, na ndani yake mulikuwa majiwe yenye samani; na taji hilo likawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Akachukua pia vitu vingi sana katika muji huo.+ 3 Na akapeleka inje watu wenye walikuwa ndani yake na akawaweka kwenye kazi+ ya kukata majiwe kwa misumeno na kufanya kazi kwa vyombo vya chuma vyenye makali na kwa mashoka. Ni vile Daudi alifanyia miji yote ya Waamoni. Mwishowe Daudi na maaskari wote wakarudia Yerusalemu.
4 Kisha, vita ikatokea katika Gezeri pamoja na Wafilisti. Wakati huo Sibekai+ Muhusha akamupiga na kumuua Sipai, mwenye alikuwa muzao wa Warefaimu,+ na wakatiishwa.
5 Na kukakuwa tena vita pamoja na Wafilisti, na Elhanani mwana wa Yairi akamupiga na kumuua Lahmi ndugu ya Goliati+ Mugati, mwenye mukuki wake ulikuwa na mupini kama muti wa wasukaji wa nguo.+
6 Vita ikatokea tena katika Gati,+ kwenye kulikuwa mwanaume mumoja mwenye alikuwa na ukubwa wa ajabu;+ alikuwa na vidole sita (6) kwenye kila mukono na vidole sita kwenye kila muguu, vyote pamoja vilikuwa makumi mbili na ine (24); naye pia alikuwa muzao wa Warefaimu.+ 7 Akaendelea kuchokoza+ Israeli. Basi Yonatani mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi, akamupiga na kumuua.
8 Hao walikuwa wazao wa Warefaimu+ katika Gati,+ na walianguka kupitia mukono wa Daudi na kupitia mukono wa watumishi wake.