Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 21
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Mambo ya Nyakati

      • Daudi anahesabia watu bila ruhusa (1-6)

      • Azabu kutoka kwa Yehova (7-17)

      • Daudi anajenga mazabahu (18-30)

1 Mambo ya Nyakati 21:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “mupinzani.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:1-3

1 Mambo ya Nyakati 21:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 8:16
  • +Amu 18:29; 2 Sa. 17:11

1 Mambo ya Nyakati 21:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:4, 8

1 Mambo ya Nyakati 21:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:9

1 Mambo ya Nyakati 21:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 1:47
  • +1Nya 27:23, 24

1 Mambo ya Nyakati 21:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 12:13
  • +Zab 25:11; 51:1
  • +2 Sa. 24:10-14

1 Mambo ya Nyakati 21:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 29:29

1 Mambo ya Nyakati 21:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:26
  • +Law. 26:14, 17
  • +Law. 26:25
  • +2 Fal. 19:35

1 Mambo ya Nyakati 21:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 34:6; Zab 51:1; Isa 55:7; Omb 3:22
  • +2Nya 28:9

1 Mambo ya Nyakati 21:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 16:46
  • +2 Sa. 24:15, 16

1 Mambo ya Nyakati 21:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “akahuzunika.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 32:14; Kum 32:36
  • +Zab 90:13
  • +2Nya 3:1
  • +2 Sa. 5:6

1 Mambo ya Nyakati 21:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 22:31; Yosh. 5:13
  • +2 Fal. 19:1
  • +2 Sa. 24:17

1 Mambo ya Nyakati 21:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 51:4
  • +Kut 32:12; Hes 16:22

1 Mambo ya Nyakati 21:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:11
  • +2 Sa. 24:18-23; 2Nya 3:1

1 Mambo ya Nyakati 21:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Unipatie.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 25:8

1 Mambo ya Nyakati 21:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “jambo lenye kuwa muzuri katika macho yake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 28:27

1 Mambo ya Nyakati 21:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:24, 25

1 Mambo ya Nyakati 21:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

1 Mambo ya Nyakati 21:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:25
  • +Law. 9:23, 24; 1 Fal. 18:38; 2Nya 7:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 77-78

1 Mambo ya Nyakati 21:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:16; Zab 103:20

1 Mambo ya Nyakati 21:29

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 3:4; 1Nya 16:39; 2Nya 1:3

Maandiko ingine

1 Nya. 21:12 Sa. 24:1-3
1 Nya. 21:22 Sa. 8:16
1 Nya. 21:2Amu 18:29; 2 Sa. 17:11
1 Nya. 21:42 Sa. 24:4, 8
1 Nya. 21:52 Sa. 24:9
1 Nya. 21:6Hes 1:47
1 Nya. 21:61Nya 27:23, 24
1 Nya. 21:82 Sa. 12:13
1 Nya. 21:8Zab 25:11; 51:1
1 Nya. 21:82 Sa. 24:10-14
1 Nya. 21:91Nya 29:29
1 Nya. 21:12Law. 26:26
1 Nya. 21:12Law. 26:14, 17
1 Nya. 21:12Law. 26:25
1 Nya. 21:122 Fal. 19:35
1 Nya. 21:13Kut 34:6; Zab 51:1; Isa 55:7; Omb 3:22
1 Nya. 21:132Nya 28:9
1 Nya. 21:14Hes 16:46
1 Nya. 21:142 Sa. 24:15, 16
1 Nya. 21:15Kut 32:14; Kum 32:36
1 Nya. 21:15Zab 90:13
1 Nya. 21:152Nya 3:1
1 Nya. 21:152 Sa. 5:6
1 Nya. 21:16Hes 22:31; Yosh. 5:13
1 Nya. 21:162 Fal. 19:1
1 Nya. 21:162 Sa. 24:17
1 Nya. 21:17Zab 51:4
1 Nya. 21:17Kut 32:12; Hes 16:22
1 Nya. 21:182 Sa. 24:11
1 Nya. 21:182 Sa. 24:18-23; 2Nya 3:1
1 Nya. 21:22Hes 25:8
1 Nya. 21:23Isa 28:27
1 Nya. 21:242 Sa. 24:24, 25
1 Nya. 21:26Kut 20:25
1 Nya. 21:26Law. 9:23, 24; 1 Fal. 18:38; 2Nya 7:1
1 Nya. 21:272 Sa. 24:16; Zab 103:20
1 Nya. 21:291 Fal. 3:4; 1Nya 16:39; 2Nya 1:3
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Mambo ya Nyakati 21:1-30

Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati

21 Kisha Shetani* akasimama ili kupinga Israeli na akamuchochea Daudi ahesabie Israeli.+ 2 Basi Daudi akaambia Yoabu+ na wakubwa wa watu: “Muende, muhesabie Israeli kuanzia Beer-sheba mupaka Dani;+ kisha muniletee habari ili nijue hesabu yao.” 3 Lakini Yoabu akasema: “Yehova azidishe watu wake mara mia moja (100)! Bwana wangu mufalme, je, hao wote tayari hawako watumishi wa bwana wangu? Sababu gani bwana wangu anataka kufanya jambo hilo? Kwa nini akuwe sababu ya hatia kwa Israeli?”

4 Lakini neno la mufalme likakuwa na nguvu kuliko la Yoabu. Basi Yoabu akaondoka na kusafiri katika Israeli yote, kisha akakuja Yerusalemu.+ 5 Sasa Yoabu akamupatia Daudi hesabu ya watu wenye waliandikishwa. Israeli wote walikuwa watu milioni moja na elfu mia moja (1 100 000) wenye kubeba panga, na Yuda, elfu mia ine makumi saba (470 000) wenye kubeba panga.+ 6 Lakini Lawi na Benyamini hawakuandikishwa kati yao,+ kwa sababu neno la mufalme lilimuchukiza Yoabu.+

7 Sasa jambo hilo lilimuchukiza sana Mungu wa kweli, basi akapiga Israeli. 8 Kisha Daudi akamuambia Mungu wa kweli: “Nimetenda zambi+ kubwa kwa kufanya jambo hilo. Na sasa, tafazali, samehe kosa la mutumishi wako,+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+ 9 Kisha Yehova akamuambia Gadi,+ muonaji wa Daudi, kwa kusema: 10 “Uende na umuambie Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakupatia mambo tatu (3) ya kuchagua. Chagua jambo moja lenye nitaleta juu yako.”’” 11 Basi Gadi akaingia kwa Daudi na kumuambia: “Yehova anasema hivi: ‘Chagua 12 kama kukuwe miaka tatu (3) ya njaa,+ ao kama maadui wako wakufagilie mbali kwa miezi tatu wakati upanga wa maadui wako unakufikia,+ ao siku tatu za upanga wa Yehova⁠—ugonjwa wa kuambukiza katika inchi+⁠—​malaika wa Yehova akileta uharibifu+ katika eneo lote la Israeli.’ Sasa fikiria jambo lenye ninapaswa kumujibu Ule mwenye alinituma.” 13 Kwa hiyo Daudi akamuambia Gadi: “Ni jambo lenye kunihangaisha sana. Tafazali, acha nianguke katika mukono wa Yehova, kwa maana rehema yake ni nyingi sana;+ lakini usiniache nianguke katika mukono wa mwanadamu.”+

14 Kisha Yehova akatuma ugonjwa wa kuambukiza+ juu ya Israeli, na hivyo watu elfu makumi saba (70 000) katika Israeli wakaanguka.+ 15 Zaidi ya hayo, Mungu wa kweli alimutuma malaika kule Yerusalemu ili kuiharibu; lakini wakati alikuwa karibu kufanya vile, Yehova akaona jambo hilo na akasikitika* kuhusu musiba huo,+ na akamuambia malaika mwenye alikuwa analeta uharibifu: “Inatosha!+ Sasa shusha mukono wako.” Malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Ornani+ Muyebusi.+

16 Wakati Daudi aliinua macho yake, akamuona malaika wa Yehova akiwa amesimama kati ya dunia na mbingu, na katika mukono wake alikuwa na upanga wenye umechomolewa+ na kuelekezwa Yerusalemu. Daudi na wazee, wakiwa wamevaa nguo za magunia,+ mara moja wakajiangusha uso chini.+ 17 Daudi akamuambia Mungu wa kweli: “Je, haiko mimi ndiye nilisema watu wahesabiwe? Mimi ndiye nilifanya zambi, na mimi ndiye nilifanya kosa;+ lakini kondoo hawa⁠—​wamefanya nini? Ee Yehova Mungu wangu, tafazali, acha mukono wako ukuje juu yangu na juu ya nyumba ya baba yangu; lakini usilete pigo hili juu ya watu wako.”+

18 Kisha malaika wa Yehova akamuambia Gadi+ amuambie Daudi apande na kumujengea Yehova mazabahu kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Ornani Muyebusi.+ 19 Basi Daudi akapanda kulingana na neno la Gadi, lenye alikuwa amesema katika jina la Yehova. 20 Wakati huo, Ornani akageuka na kumuona ule malaika, na wana wake ine (4) wenye walikuwa pamoja naye wakajificha. Sasa Ornani alikuwa anapiga-piga ngano. 21 Wakati Daudi alipanda kwa Ornani, Ornani aliangalia na kumuona Daudi, na mara moja akatoka kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka na kumuinamia Daudi uso chini. 22 Daudi akamuambia Ornani: “Unipatie ninunue* nafasi ya kiwanja cha kupigia-pigia nafaka, ili nimujengee Yehova mazabahu pale. Unipatie ninunue nafasi hiyo kwa bei kamili, ili pigo lenye kuwa juu ya watu lisimamishwe.”+ 23 Lakini Ornani akamuambia Daudi: “Uikamate ikuwe yako, na bwana wangu mufalme afanye jambo lenye kuonekana kuwa muzuri kwake.* Angalia, ninatoa ngombe kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa na kifaa cha kupiga-piga nafaka+ kwa ajili ya kuni na ngano kuwa toleo la nafaka. Ninatoa vile vyote.

24 Hata hivyo, Mufalme Daudi akamuambia Ornani: “Hapana, ninapaswa kuinunua kwa bei kamili, kwa sababu sitakamata kitu chako na kukipatia Yehova ao kutoa zabihu za kuteketezwa zenye hazinigarimu kitu.”+ 25 Basi Daudi akamupatia Ornani zahabu yenye uzito wa shekeli* mia sita (600) kwa ajili ya nafasi hiyo. 26 Na Daudi akamujengea Yehova mazabahu+ pale na kutoa zabihu za kuteketezwa na zabihu za ushirika, na akamuitia Yehova, mwenye sasa alimujibu kwa moto+ kutoka mbinguni juu ya mazabahu hiyo ya toleo la kuteketezwa. 27 Kisha Yehova akamuagiza ule malaika+ arudishe upanga wake katika mufuko wake wa upanga. 28 Wakati huo, wakati Daudi aliona kwamba Yehova alikuwa amemujibu kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Ornani Muyebusi, akaendelea kutoa zabihu pale. 29 Hata hivyo, ile tabenakulo ya Yehova yenye Musa alikuwa ametengeneza katika jangwa na ile mazabahu ya toleo la kuteketezwa vilikuwa mahali pa juu kule Gibeoni wakati huo.+ 30 Lakini Daudi alikuwa hajaweza kuenda mbele ya mazabahu hiyo ili kutafuta shauri kwa Mungu, kwa maana aliogopa sana kwa sababu ya upanga wa malaika wa Yehova.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine