Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
27 Hii ndiyo hesabu ya Waisraeli, vichwa vya jamaa za upande wa baba, wakubwa wa maelfu na wa mamia,+ na maofisa wao wenye walifanya utumishi kwa ajili ya mufalme+ katika kila jambo la vikundi vyenye vilikuwa vinaingia ndani na kutoka inje mwezi kisha mwezi katika miezi yote ya mwaka; kulikuwa watu elfu makumi mbili na ine (24 000) katika kila kikundi.
2 Juu ya kikundi cha kwanza cha mwezi wa kwanza kulikuwa Yashobeamu+ mwana wa Zabdieli, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 3 Kati ya wana wa Perezi,+ yeye ndiye alikuwa kichwa cha wakubwa wote wa vikundi vyenye vilipewa daraka la kutumika katika mwezi wa kwanza. 4 Juu ya kikundi cha mwezi wa pili kulikuwa Dodai+ Mwahohi+ pamoja na kikundi chake, na Mikloti ndiye alikuwa kiongozi, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 5 Mukubwa wa kikundi cha tatu (3) chenye kilipewa daraka la kutumika katika mwezi wa tatu alikuwa Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mukubwa wa makuhani, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 6 Huyo Benaya alikuwa mupiganaji-vita mwenye nguvu kati ya wale makumi tatu (30) na alikuwa anasimamia wale makumi tatu, na juu ya kikundi chake kulikuwa Amizabadi mwana wake. 7 Wa ine (4) kwa ajili ya mwezi wa ine alikuwa Asaheli,+ ndugu ya Yoabu,+ na Zebadia mwana wake kisha yeye, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 8 Mukubwa wa tano (5) kwa ajili ya mwezi wa tano alikuwa Shamhuti Mwizrahia, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 9 Wa sita (6) kwa ajili ya mwezi wa sita alikuwa Ira+ mwana wa Ikeshi Mutekoa,+ na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 10 Wa saba (7) kwa ajili ya mwezi wa saba alikuwa Helezi+ Mupeloni wa Waefraimu, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 11 Wa munane (8) kwa ajili ya mwezi wa munane alikuwa Sibekai+ Muhusha wa Wazera,+ na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 12 Wa kenda (9) kwa ajili ya mwezi wa kenda alikuwa Abiezeri+ Mwanatoti+ wa Wabenyamini, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 13 Wa kumi (10) kwa ajili ya mwezi wa kumi alikuwa Maharai+ Munetofa wa Wazera,+ na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 14 Wa kumi na moja (11) kwa ajili ya mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya+ Mupiratoni wa wana wa Efraimu, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake. 15 Wa kumi na mbili (12) kwa ajili ya mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Munetofa, wa Otnieli, na watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walikuwa katika kikundi chake.
16 Hawa ndio walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kati ya Warubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi; kati ya Wasimeoni, Shefatia mwana wa Maaka; 17 kutoka kwa Lawi, Hashabia mwana wa Kemueli; kutoka kwa Haruni, Sadoki; 18 kutoka kwa Yuda, Elihu,+ mumoja wa ndugu za Daudi; kutoka kwa Isakari, Omri mwana wa Mikaeli; 19 kutoka kwa Zabuloni, Ishmaya mwana wa Obadia; kutoka kwa Naftali, Yerimoti mwana wa Azrieli; 20 kati ya Waefraimu, Hoshea mwana wa Azazia; kutoka katika nusu ya kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaya; 21 kutoka kwa nusu ya kabila la Manase katika Gileadi, Ido mwana wa Zekaria; kutoka kwa Benyamini, Yaasieli mwana wa Abneri;+ 22 kutoka kwa Dani, Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio walikuwa wakubwa wa makabila ya Israeli.
23 Daudi hakuhesabia wale wenye walikuwa na miaka makumi mbili (20) na kushuka chini, kwa sababu Yehova alikuwa ameahidi kwamba angefanya Israeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ 24 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa ameanza kuwahesabia, lakini hakumaliza; na kasirani ya Mungu iliwaka juu ya Israeli* kwa sababu ya jambo hilo,+ na hesabu hiyo haikuwekwa katika habari ya historia ya nyakati za Mufalme Daudi.
25 Azmaveti mwana wa Adieli alisimamia hazina za mufalme.+ Yonatani mwana wa Uzia alisimamia madepo* katika maeneo ya mashamba, katika miji, katika vijiji, na katika minara. 26 Ezri mwana wa Kelubu alisimamia wafanyakazi wa mashamba wenye walilima udongo. 27 Shimei Murama alisimamia mashamba ya mizabibu; Zabdi Mushifi alisimamia mazao ya mashamba ya mizabibu kwa ajili ya madepo ya divai. 28 Baal-hanani Mugederi alisimamia mashamba ya mizeituni na mikuyu+ katika Shefela;+ Yoashi alisimamia madepo ya mafuta. 29 Shitrai Musharoni alisimamia mifugo yenye ilikuwa inakula majani katika Sharoni,+ na Shafati mwana wa Adlai alisimamia mifugo katika mabonde tambarare.* 30 Obili Mwishmaeli alisimamia ngamia; Yehdeya Mumeronoti alisimamia punda.* 31 Yazizi Muhagri alisimamia makundi. Hao wote ndio walikuwa wakubwa wa mali za Mufalme Daudi.
32 Yonatani,+ mupwa wa Daudi, alikuwa mushauri, mwanaume mwenye uelewaji na pia mwandishi, na Yehieli mwana wa Hakmoni alitunza wana wa mufalme.+ 33 Ahitofeli+ alikuwa mushauri wa mufalme, na Hushai+ Mwarki alikuwa rafiki ya* mufalme. 34 Kisha Ahitofeli kulikuwa Yehoyada mwana wa Benaya+ na Abiatari;+ na Yoabu+ alikuwa mukubwa wa jeshi la mufalme.