Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
4 Kisha akatengeneza mazabahu ya shaba,+ urefu wa mikono makumi mbili (20), upana wa mikono makumi mbili, na urefu kuenda juu wa mikono kumi (10).
2 Akatengeneza Bahari*+ kwa metali yenye kuyeyushwa. Ilikuwa na umbo ya muviringo, upana wa mikono kumi (10) kutoka sehemu moja ya mudomo mupaka sehemu ingine, na urefu kuenda juu wa mikono tano (5), na iliomba kamba ya urefu wa mikono makumi tatu (30) ili kuizunguka.+ 3 Na kulikuwa mapambo ya vibuyu+ chini yake, yalikuwa yanaizunguka kabisa, vibuyu kumi (10) kwa kila mukono mumoja kuzunguka Bahari hiyo pande zote. Vibuyu hivyo vilikuwa katika mistari mbili na viliyeyushwa kama kitu kimoja pamoja nayo. 4 Ilisimama juu ya ngombe-dume kumi na mbili (12),+ watatu (3) walikuwa wanaangalia kaskazini, watatu walikuwa wanaangalia mangaribi, watatu walikuwa wanaangalia kusini, na watatu walikuwa wanaangalia mashariki; na Bahari hiyo ilikuwa juu yao, na sehemu zao zote za nyuma zilielekea katikati. 5 Na unene wake ulikuwa upana wa kiganja kimoja cha mukono;* na mudomo wake ulitengenezwa kama mudomo wa kikombe, kama ua la yungiyungi. Chombo hicho kingeweza kuingia ndani* vipimo elfu tatu (3 000) vya bati.*
6 Tena, alitengeneza beseni kumi (10) za kusafishia na akaweka tano (5) upande wa kuume na tano upande wa kushoto.+ Walikuwa wanasafishia ndani vitu vyenye vilitumiwa kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.+ Lakini Bahari ilitumiwa na makuhani kwa ajili ya kuoga.+
7 Kisha akatengeneza vinara kumi (10) vya taa vya zahabu,+ kama vile ilionyeshwa,+ na akaviweka katika hekalu, vitano (5) upande wa kuume na vitano upande wa kushoto.+
8 Akatengeneza pia meza kumi (10) na akaziweka katika hekalu, tano (5) upande wa kuume na tano upande wa kushoto;+ na akatengeneza mabakuli mia moja (100) ya zahabu.
9 Kisha akatengeneza kiwanja+ cha makuhani+ na kile kiwanja kikubwa+ na milango ya kiwanja hicho, na akafunika milango yake kwa shaba. 10 Na akaweka ile Bahari upande wa kuume, kuelekea kusini-mashariki.+
11 Hiramu akatengeneza pia makopo, vipao,* na mabakuli.+
Basi Hiramu akamaliza kazi yenye alifanya kwa ajili ya Mufalme Sulemani kwenye nyumba ya Mungu wa kweli:+ 12 zile nguzo mbili+ na vile vifuniko vyenye umbo ya bakuli vyenye vilikuwa kwenye sehemu ya juu ya zile nguzo mbili; zile nyavu mbili+ za* kufunika vile vifuniko mbili vyenye umbo ya bakuli vyenye vilikuwa kwenye sehemu ya juu ya zile nguzo; 13 yale makomamanga mia ine (400)+ kwa ajili ya zile nyavu* mbili, mistari mbili ya makomamanga kwa ajili ya kila wavu, ili kufunika vile vifuniko mbili vyenye umbo ya bakuli vyenye vilikuwa kwenye zile nguzo;+ 14 yale magari* kumi (10) na zile beseni kumi zenye zilikuwa kwenye magari hayo;+ 15 ile Bahari na wale ngombe-dume kumi na mbili (12) wenye walikuwa chini yake;+ 16 na yale makopo, vile vipao,* yale makanya,*+ na vyombo vyake vyote vyenye Hiram-abivu+ alimutengenezea Mufalme Sulemani kwa shaba yenye kungarishwa, kwa ajili ya nyumba ya Yehova. 17 Mufalme akaviyeyusha katika wilaya ya Yordani katika udongo muzito kati ya Sukoti+ na Saretani. 18 Sulemani akatengeneza vyombo hivyo vyote kwa wingi sana; uzito wa shaba haukujulikana.+
19 Sulemani akatengeneza vyombo vyote+ kwa ajili nyumba ya Mungu wa kweli: mazabahu ya zahabu;+ meza+ na mikate ya wonyesho juu ya meza hizo;+ 20 vinara vya taa na taa zake za zahabu safi,+ ili ziwake mbele ya chumba cha ndani zaidi kulingana na vile iliombwa; 21 na maua, taa, na vifaa vya kushikia tambi,* vya zahabu, zahabu safi kabisa; 22 vizimisha-moto, mabakuli, vikombe, na vyetezo, vya zahabu safi; na muingilio wa nyumba, milango yake ya ndani kwa ajili ya Patakatifu Zaidi,+ na milango ya nyumba ya hekalu, vya zahabu.+