Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
5 Basi Sulemani akamaliza kazi yote yenye alipaswa kufanya kwa ajili ya nyumba ya Yehova.+ Kisha Sulemani akaingiza ndani vitu vyenye Daudi baba yake alikuwa amefanya kuwa vitakatifu,+ na akaweka feza, zahabu, na vyombo vyote katika hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+ 2 Wakati huo Sulemani akakusanya wazee wa Israeli, vichwa vyote vya makabila, wakubwa wa jamaa za upande wa baba za Israeli. Wakakuja Yerusalemu ili kupandisha sanduku la agano la Yehova kutoka katika Muji wa Daudi,+ ni kusema, Sayuni.+ 3 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika mbele ya mufalme kwenye sikukuu* yenye kufanywa katika mwezi wa saba (7).+
4 Basi wazee wote wa Israeli wakakuja, na Walawi wakanyangula Sanduku.+ 5 Wakapandisha Sanduku, hema ya mukutano,+ na vyombo vyote vitakatifu vyenye vilikuwa katika hema hiyo. Makuhani na Walawi* wakavipandisha. 6 Mufalme Sulemani na mukusanyiko wote wa Israeli wenye walikuwa wameitwa ili wakutane naye walikuwa mbele ya Sanduku. Kondoo wengi sana na ngombe wengi sana walikuwa wanatolewa kuwa zabihu+ hivi kwamba hawangeweza kuhesabiwa ao kujulikana hesabu. 7 Kisha makuhani wakaleta sanduku la agano la Yehova mahali pake, katika chumba cha ndani kabisa cha nyumba, Patakatifu Zaidi, chini ya mabawa ya wale makerubi.+ 8 Kwa hiyo mabawa ya makerubi yalikuwa yamenyooshwa juu ya mahali kwenye Sanduku lilikuwa, na hivyo makerubi hao walifunika Sanduku na miti yake+ kutoka juu. 9 Miti hiyo ilikuwa mirefu sana na hivyo sehemu za mwisho za ile miti zilionekana kutoka Patakatifu mbele ya chumba cha ndani kabisa, lakini hazikuonekana kutoka inje. Na iko kule mupaka leo. 10 Hapakukuwa kitu chochote ndani ya Sanduku hilo isipokuwa yale mabamba mbili yenye Musa aliweka ndani kule Horebu,+ wakati Yehova alifanya agano+ pamoja na watu wa Israeli wakati walikuwa wanatoka Misri.+
11 Wakati makuhani walitoka mahali patakatifu (kwa maana makuhani wote wenye walikuwa pale walikuwa wamejitakasa,+ bila kujali vikundi vyao),+ 12 waimbaji wote Walawi+ wenye walikuwa wa Asafu,+ wa Hemani,+ wa Yedutuni,+ na wa wana wao na ndugu zao walikuwa wamevaa nguo za kitambaa kizuri, wakiwa wamebeba matoazi, vyombo vya kamba, na vinubi; walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa mazabahu, na pamoja nao makuhani mia moja makumi mbili (120) walikuwa wanapiga tarumbeta.+ 13 Wakati wapiga-tarumbeta na waimbaji walikuwa wanamusifu na kumushukuru Yehova kwa umoja, na wakati sauti ya tarumbeta, matoazi, na vyombo vingine vya muziki ilipanda wakati walikuwa wanamusifu Yehova, “kwa maana yeye ni mwema; upendo wake mushikamanifu unadumu milele,”+ basi ile nyumba, nyumba ya Yehova, ikajaa wingu.+ 14 Makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya utumishi kwa sababu ya wingu hilo, kwa maana utukufu wa Yehova ulijaza nyumba ya Mungu wa kweli.+