Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
2 Sasa Sulemani akatoa agizo kwamba nyumba ijengwe kwa ajili ya jina la Yehova+ na nyumba* kwa ajili ya ufalme wake.+ 2 Sulemani akaandikisha wanaume elfu makumi saba (70 000) kuwa wafanyakazi wa kawaida,* wanaume elfu makumi munane (80 000) kuwa wachongaji wa majiwe katika milima,+ na wanaume elfu tatu mia sita (3 600) kuwa waangalizi juu yao.+ 3 Pia, Sulemani akatuma ujumbe kwa Hiramu+ mufalme wa Tiro: “Unifanyie kama vile ulimufanyia Daudi baba yangu wakati ulimutumia mbao za mierezi ili ajenge nyumba* ya kuishi ndani.+ 4 Sasa ninajenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu, ili kuitakasa kwake, ili kuchoma uvumba wenye marashi mbele yake,+ na pia kwa ajili ya mikate ya kila wakati yenye kupangwa moja juu ya ingine*+ na matoleo ya kuteketezwa, asubui na mangaribi,+ katika siku za Sabato,+ katika miezi mipya,+ na kwenye vipindi vya sikukuu+ za Yehova Mungu wetu. Hili ni jambo lenye Israeli wanapaswa kuendelea kufanya. 5 Nyumba yenye ninajenga itakuwa kubwa, kwa maana Mungu wetu ni mukubwa kuliko miungu mingine yote. 6 Na ni nani mwenye anaweza kumujengea nyumba? Kwa maana mbingu na mbingu za mbingu haziwezi kumuenea,+ basi mimi ni nani ili nimujengee nyumba isipokuwa ikuwe mahali pa kuchoma zabihu ili zitoe moshi mbele yake? 7 Sasa unitumie fundi mwenye kuwa na ujuzi wa kufanya kazi ya zahabu, feza, shaba,+ chuma, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, uzi nyekundu, na uzi ya bluu, na mwenye anajua namna ya kuchonga michongo. Atafanya kazi katika Yuda na katika Yerusalemu pamoja na mafundi wangu wenye ujuzi, wenye Daudi baba yangu ametayarisha.+ 8 Na unitumie mbao za mierezi, miberoshi,+ na misandali+ kutoka Lebanoni, kwa maana ninajua muzuri kwamba watumishi wako ni wenye uzoefu wa kukata miti ya Lebanoni.+ Watumishi wangu watafanya kazi pamoja na watumishi wako+ 9 ili kunitayarishia mbao nyingi sana, kwa maana nyumba yenye nitajenga itakuwa kubwa ajabu. 10 Sasa angalia! Nitatoa chakula kwa ajili ya watumishi wako,+ wakataji wa miti wenye kukata miti: kori* elfu makumi mbili (20 000) za ngano, kori elfu makumi mbili za shayiri, bati* elfu makumi mbili za divai, na bati elfu makumi mbili za mafuta.”
11 Halafu Hiramu mufalme wa Tiro akatuma kwa Sulemani ujumbe huu wenye kuandikwa: “Kwa sababu Yehova anapenda watu wake, amekufanya kuwa mufalme wao.” 12 Kisha Hiramu akasema: “Yehova Mungu wa Israeli asifiwe, mwenye alifanya mbingu na dunia, kwa sababu amemupatia Mufalme Daudi mwana mwenye hekima,+ mwenye kuwa na busara na uelewaji,+ mwenye atajenga nyumba kwa ajili ya Yehova na nyumba kwa ajili ya ufalme wake. 13 Sasa ninamutuma fundi mwenye ujuzi, mwenye kuwa na uelewaji, Hiram-abi,+ 14 mwenye ni mwana wa mwanamuke Mudani lakini mwenye baba yake alikuwa mutu wa Tiro; iko* na uzoefu wa kufanya kazi ya zahabu, feza, shaba, chuma, majiwe, mbao, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, uzi za bluu, kitambaa kizuri, na uzi nyekundu.+ Anaweza kuchonga michongo ya kila aina na kufanya kila muchoro wenye anapewa.+ Atatumika pamoja na mafundi wako mwenyewe wenye ujuzi na mafundi wenye ujuzi wa bwana wangu Daudi baba yako. 15 Sasa bwana wangu atume ngano, shayiri, mafuta, na divai vyenye ameahidi watumishi wake.+ 16 Na sisi tutakata miti kutoka Lebanoni,+ hesabu yoyote yenye uko nayo lazima, na tutaileta kwako mafungu-mafungu juu ya bahari mupaka Yopa;+ na utaipandisha mupaka Yerusalemu.”+
17 Kisha Sulemani akahesabia wanaume wote wenye walikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Israeli,+ kisha ile hesabu ya watu yenye Daudi baba yake alikuwa amefanya,+ na kukapatikana wanaume elfu mia moja makumi tano na tatu na mia sita (153 600). 18 Kwa hiyo akaweka watu elfu makumi saba (70 000) kati yao kuwa wafanyakazi wa kawaida,* wanaume elfu makumi munane (80 000) kuwa wachongaji wa majiwe+ katika milima, na wanaume elfu tatu mia sita (3 600) kuwa waangalizi wa kufanya watu watumike.+