Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 3
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Mambo ya Nyakati

      • Sulemani anaanza kujenga hekalu (1-7)

      • Patakatifu Zaidi (8-14)

      • Nguzo mbili za shaba (15-17)

2 Mambo ya Nyakati 3:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:1, 37
  • +Mwa 22:2, 14
  • +2 Sa. 24:25; 1Nya 21:18
  • +2 Sa. 24:18; 1Nya 21:22

2 Mambo ya Nyakati 3:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Kipimo cha kawaida cha mukono mumoja kilikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5), lakini watu fulani wanafikiri kwamba “kipimo cha zamani” kinamaanisha kipimo cha mukono murefu chenye kilikuwa sawa na santimetre 51.8 (inchi 20.4). Angalia Nyongeza B14.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:2

2 Mambo ya Nyakati 3:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mikono 20 kueneana na upana wa nyumba.”

  • *

    Maandishi fulani ya zamani inasema “120,” lakini maandishi ingine na tafsiri fulani zinasema “mikono 20.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:3

2 Mambo ya Nyakati 3:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:15, 22
  • +1 Fal. 6:29
  • +1 Fal. 6:21

2 Mambo ya Nyakati 3:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 29:2, 8
  • +1Nya 29:3, 4

2 Mambo ya Nyakati 3:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Hapa kizingiti ni ubao wenye kuwa chini ya mulango.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 26:29
  • +Kut 26:1; 1 Fal. 6:29

2 Mambo ya Nyakati 3:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nyumba ya.”

  • *

    Talanta moja ilikuwa sawa na kilograme 34.2 (aunsi troi 1.101). Angalia Nyongeza B14.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 26:33; 1 Fal. 8:6; Ebr 9:24
  • +1 Fal. 6:20

2 Mambo ya Nyakati 3:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

2 Mambo ya Nyakati 3:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nyumba ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:23-28

2 Mambo ya Nyakati 3:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 8:6; 1Nya 28:18

2 Mambo ya Nyakati 3:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, zikielekea Patakatifu.

2 Mambo ya Nyakati 3:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mt 27:51; Ebr 10:19, 20
  • +Kut 26:31, 33

2 Mambo ya Nyakati 3:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:13
  • +1 Fal. 7:15-22; 2 Fal. 25:17; 2Nya 4:11-13; Yer 52:22, 23

2 Mambo ya Nyakati 3:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kusini.”

  • *

    Ao “kaskazini.”

  • *

    Maana yake “Yeye [ni kusema, Yehova] Afanye Imara Kabisa.”

  • *

    Pengine inamaanisha “Katika Nguvu.”

Maandiko ingine

2 Nya. 3:11 Fal. 6:1, 37
2 Nya. 3:1Mwa 22:2, 14
2 Nya. 3:12 Sa. 24:25; 1Nya 21:18
2 Nya. 3:12 Sa. 24:18; 1Nya 21:22
2 Nya. 3:31 Fal. 6:2
2 Nya. 3:41 Fal. 6:3
2 Nya. 3:51 Fal. 6:15, 22
2 Nya. 3:51 Fal. 6:29
2 Nya. 3:51 Fal. 6:21
2 Nya. 3:61Nya 29:2, 8
2 Nya. 3:61Nya 29:3, 4
2 Nya. 3:7Kut 26:29
2 Nya. 3:7Kut 26:1; 1 Fal. 6:29
2 Nya. 3:8Kut 26:33; 1 Fal. 8:6; Ebr 9:24
2 Nya. 3:81 Fal. 6:20
2 Nya. 3:101 Fal. 6:23-28
2 Nya. 3:111 Fal. 8:6; 1Nya 28:18
2 Nya. 3:14Mt 27:51; Ebr 10:19, 20
2 Nya. 3:14Kut 26:31, 33
2 Nya. 3:152 Fal. 25:13
2 Nya. 3:151 Fal. 7:15-22; 2 Fal. 25:17; 2Nya 4:11-13; Yer 52:22, 23
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Mambo ya Nyakati 3:1-17

Cha Pili cha Mambo ya Nyakati

3 Kisha Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ katika Yerusalemu kwenye Mulima Moria,+ mahali kwenye Yehova alikuwa amemutokea Daudi baba yake,+ mahali kwenye Daudi alikuwa ametayarisha kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Ornani+ Muyebusi. 2 Akaanza kujenga katika siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa ine (4) wa utawala wake. 3 Na musingi wenye Sulemani aliweka kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mungu wa kweli ulikuwa na urefu wa mikono makumi sita (60) na upana wa mikono makumi mbili (20),+ kulingana na kipimo cha zamani.* 4 Baraza la mbele lilikuwa na urefu wa mikono makumi mbili (20), lililingana na upana wa nyumba,* na urefu wake kuenda juu ulikuwa mikono makumi mbili (20);* na akafunika upande wa ndani kwa zahabu safi.+ 5 Alifunika nyumba kubwa kwa mbao za miberoshi, kisha akaifunika kwa zahabu safi,+ na kisha akaipamba kwa michongo ya miti ya mitende+ na minyororo.+ 6 Tena, akafunika nyumba hiyo kwa majiwe ya muzuri yenye samani;+ na zahabu+ yenye alitumia ilikuwa zahabu kutoka Parvaimu. 7 Alifunika nyumba, vipande vikubwa vya miti, vizingiti,* kuta zake, na milango yake kwa zahabu;+ na akachonga makerubi kwenye kuta.+

8 Sasa akajenga chumba cha* Patakatifu Zaidi;+ urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono makumi mbili (20), na upana wake ulikuwa mikono makumi mbili. Akakifunika kwa talanta* mia sita (600) za zahabu safi.+ 9 Uzito wa zahabu kwa ajili ya misumari ulikuwa shekeli makumi tano (50);* na alifunika vyumba vya juu kwa zahabu.

10 Kisha akatengeneza mifano ya makerubi wawili katika chumba cha* Patakatifu Zaidi, na akawafunika kwa zahabu.+ 11 Urefu wote wa mabawa ya makerubi hao+ ulikuwa mikono makumi mbili (20); bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mikono tano (5) na liligusa ukuta wa nyumba, na bawa lake lingine lilikuwa na urefu wa mikono tano na liligusa bawa moja la ule kerubi mwingine. 12 Na bawa moja la ule kerubi mwingine lilikuwa na urefu wa mikono tano (5) na liligusa ukuta mwingine wa nyumba, na bawa lake lingine lilikuwa na urefu wa mikono tano na liligusa bawa moja la ule kerubi wa kwanza. 13 Mabawa ya makerubi hao yalikuwa yamenyooshwa kufikia urefu wa mikono makumi mbili (20); na walikuwa wamesimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ndani.*

14 Akatengeneza pia pazia+ la uzi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, uzi nyekundu, na kitambaa kizuri, na kulipamba kwa mifano ya makerubi.+

15 Kisha akatengeneza nguzo mbili+ mbele ya nyumba hiyo, urefu wa mikono makumi tatu na tano (35), na kifuniko chenye kilikuwa kwenye sehemu ya juu ya kila nguzo kilikuwa cha mikono tano (5).+ 16 Na alitengeneza minyororo, yenye kuwa kama mikufu, na akaiweka kwenye sehemu za juu za nguzo hizo, na akatengeneza makomamanga mia moja (100) na kuyaweka kwenye minyororo hiyo. 17 Akasimamisha nguzo hizo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume* na ingine upande wa kushoto;* akapatia nguzo ya upande wa kuume jina Yakini* na ile ya upande wa kushoto akaipatia jina Boazi.*

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine