Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
3 Kisha Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ katika Yerusalemu kwenye Mulima Moria,+ mahali kwenye Yehova alikuwa amemutokea Daudi baba yake,+ mahali kwenye Daudi alikuwa ametayarisha kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Ornani+ Muyebusi. 2 Akaanza kujenga katika siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa ine (4) wa utawala wake. 3 Na musingi wenye Sulemani aliweka kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mungu wa kweli ulikuwa na urefu wa mikono makumi sita (60) na upana wa mikono makumi mbili (20),+ kulingana na kipimo cha zamani.* 4 Baraza la mbele lilikuwa na urefu wa mikono makumi mbili (20), lililingana na upana wa nyumba,* na urefu wake kuenda juu ulikuwa mikono makumi mbili (20);* na akafunika upande wa ndani kwa zahabu safi.+ 5 Alifunika nyumba kubwa kwa mbao za miberoshi, kisha akaifunika kwa zahabu safi,+ na kisha akaipamba kwa michongo ya miti ya mitende+ na minyororo.+ 6 Tena, akafunika nyumba hiyo kwa majiwe ya muzuri yenye samani;+ na zahabu+ yenye alitumia ilikuwa zahabu kutoka Parvaimu. 7 Alifunika nyumba, vipande vikubwa vya miti, vizingiti,* kuta zake, na milango yake kwa zahabu;+ na akachonga makerubi kwenye kuta.+
8 Sasa akajenga chumba cha* Patakatifu Zaidi;+ urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono makumi mbili (20), na upana wake ulikuwa mikono makumi mbili. Akakifunika kwa talanta* mia sita (600) za zahabu safi.+ 9 Uzito wa zahabu kwa ajili ya misumari ulikuwa shekeli makumi tano (50);* na alifunika vyumba vya juu kwa zahabu.
10 Kisha akatengeneza mifano ya makerubi wawili katika chumba cha* Patakatifu Zaidi, na akawafunika kwa zahabu.+ 11 Urefu wote wa mabawa ya makerubi hao+ ulikuwa mikono makumi mbili (20); bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mikono tano (5) na liligusa ukuta wa nyumba, na bawa lake lingine lilikuwa na urefu wa mikono tano na liligusa bawa moja la ule kerubi mwingine. 12 Na bawa moja la ule kerubi mwingine lilikuwa na urefu wa mikono tano (5) na liligusa ukuta mwingine wa nyumba, na bawa lake lingine lilikuwa na urefu wa mikono tano na liligusa bawa moja la ule kerubi wa kwanza. 13 Mabawa ya makerubi hao yalikuwa yamenyooshwa kufikia urefu wa mikono makumi mbili (20); na walikuwa wamesimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ndani.*
14 Akatengeneza pia pazia+ la uzi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, uzi nyekundu, na kitambaa kizuri, na kulipamba kwa mifano ya makerubi.+
15 Kisha akatengeneza nguzo mbili+ mbele ya nyumba hiyo, urefu wa mikono makumi tatu na tano (35), na kifuniko chenye kilikuwa kwenye sehemu ya juu ya kila nguzo kilikuwa cha mikono tano (5).+ 16 Na alitengeneza minyororo, yenye kuwa kama mikufu, na akaiweka kwenye sehemu za juu za nguzo hizo, na akatengeneza makomamanga mia moja (100) na kuyaweka kwenye minyororo hiyo. 17 Akasimamisha nguzo hizo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume* na ingine upande wa kushoto;* akapatia nguzo ya upande wa kuume jina Yakini* na ile ya upande wa kushoto akaipatia jina Boazi.*