Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
17 Na Yehoshafati+ mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake, na akatia nguvu mamlaka yake juu ya Israeli. 2 Aliweka majeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka kambi za kijeshi katika inchi ya Yuda na katika miji ya Efraimu yenye Asa baba yake alikuwa amekamata.+ 3 Yehova aliendelea kuwa pamoja na Yehoshafati kwa sababu alitembea katika njia za zamani za Daudi babu yake+ na hakutafuta Mabaali. 4 Kwa maana alimutafuta Mungu wa baba yake+ na kufuata* amri yake na hapana mazoea ya Israeli.+ 5 Yehova aliendelea kufanya ufalme ukuwe imara kabisa katika mukono wake;+ na Yuda wote wakaendelea kumupatia Yehoshafati zawadi, na akakuwa na utajiri na utukufu kwa wingi.+ 6 Moyo wake ukakuwa hodari katika njia za Yehova, na hata aliondoa mahali pa juu+ na miti mitakatifu*+ kutoka Yuda.
7 Katika mwaka wa tatu (3) wa utawala wake alituma waite wakubwa wake, Ben-haili, Obadia, Zekaria, Netaneli, na Mikaya, ili kufundisha katika miji ya Yuda. 8 Kulikuwa Walawi pamoja nao: Shemaya, Netania, Zebadia, Asaheli, Shemiramoti, Yehonatani, Adoniya, Tobaya, na Tob-adoniya, na pamoja nao Elishama na Yehoramu makuhani.+ 9 Walianza kufundisha katika Yuda, wakiwa na kitabu cha Sheria ya Yehova,+ na walizunguka katika miji yote ya Yuda wakifundisha kati ya watu.
10 Na woga wa Yehova ukakuja juu ya falme zote za inchi zenye kuzunguka Yuda, na hawakupigana na Yehoshafati. 11 Na Wafilisti wakamuletea Yehoshafati zawadi na feza kama ushuru. Waarabu wakamuletea kondoo-dume elfu saba mia saba (7 700) na mbuzi-dume elfu saba mia saba kutoka katika makundi yao.
12 Yehoshafati akaendelea kuwa mukubwa zaidi na zaidi,+ na akaendelea kujenga ngome+ na miji yenye madepo+ katika Yuda. 13 Alitimiza miradi mikubwa katika miji ya Yuda, na alikuwa na maaskari, wapiganaji-vita wenye nguvu, katika Yerusalemu. 14 Hao walipangwa katika vikundi kulingana na jamaa zao za upande wa baba: wa Yuda wakubwa wa maelfu, Adna mukubwa, na pamoja naye kulikuwa wapiganaji-vita elfu mia tatu (300 000) wenye nguvu.+ 15 Na chini ya uongozi wake kulikuwa Yehohanani mukubwa, na pamoja naye kulikuwa watu elfu mia mbili makumi munane (280 000). 16 Na pia chini ya uongozi wake kulikuwa Amasia mwana wa Zikri, mwenye alijitolea kwa ajili ya utumishi wa Yehova, na pamoja naye kulikuwa wapiganaji-vita elfu mia mbili (200 000) wenye nguvu. 17 Na kutoka kwa Benyamini+ kulikuwa Eliada, mupiganaji-vita mwenye nguvu, na pamoja naye kulikuwa watu elfu mia mbili (200 000) wenye walikuwa na pinde na ngao.+ 18 Na chini ya uongozi wake kulikuwa Yehozabadi, na pamoja naye kulikuwa watu elfu mia moja makumi munane (180 000) wenye walitayarishwa kwa ajili ya jeshi. 19 Hao walikuwa wanafanya utumishi kwa ajili ya mufalme zaidi ya wale wenye mufalme aliweka katika miji yenye ngome katika Yuda yote.+