Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
22 Kisha wakaaji wa Yerusalemu wakamufanya Ahazia mwana wake mudogo zaidi kuwa mufalme pa nafasi yake, kwa maana kikundi cha wanyanganyi chenye kilikuja pamoja na Waarabu kwenye kambi kilikuwa kimeua wale wakubwa wote.+ Basi Ahazia mwana wa Yehoramu akaanza kutawala akiwa mufalme wa Yuda.+ 2 Ahazia alikuwa na miaka makumi mbili na mbili (22) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa mwaka mumoja katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Atalia,+ mujukuu wa* Omri.+
3 Yeye pia alitembea katika njia za nyumba ya Ahabu,+ kwa maana mama yake alikuwa mushauri wake katika kutenda kwa uovu. 4 Na aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, kama nyumba ya Ahabu, kwa maana walikuwa washauri wake kisha kifo cha baba yake, kwa uharibifu wake. 5 Alifuata shauri lao na akaenda pamoja na Yehoramu mwana wa Mufalme Ahabu wa Israeli ili kupigana vita na Mufalme Hazaeli+ wa Siria kule Ramoti-gileadi,+ kwenye wapiga-mishale walimuumiza Yehoramu. 6 Akarudia Yezreeli+ ili apone vidonda vyenye walikuwa wamemuumiza kule Rama wakati alipigana na Mufalme Hazaeli wa Siria.+
Ahazia* mwana wa Yehoramu+ mufalme wa Yuda alishuka kuenda Yezreeli ili kumuona Yehoramu+ mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa ameumizwa.*+ 7 Lakini Mungu alitokeza kuanguka kwa Ahazia kupitia safari yake ya kuenda kwa Yehoramu; na wakati alikuja, alienda pamoja na Yehoramu ili kukutana na Yehu+ mujukuu* wa Nimshi, mwenye Yehova alikuwa ametia mafuta ili kuharibu* nyumba ya Ahabu.+ 8 Wakati Yehu alianza kufanya hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, alipata wakubwa wa Yuda na wana wa ndugu za Ahazia, watumishi wa Ahazia, na akawaua.+ 9 Kisha akatafuta Ahazia; wakamukamata mahali kwenye alikuwa anajificha katika Samaria, na wakamuleta kwa Yehu. Halafu wakamuua na kumuzika,+ kwa maana walisema: “Yeye ni mujukuu wa Yehoshafati, mwenye alitafuta Yehova kwa moyo wake wote.”+ Hakuna mutu yeyote wa nyumba ya Ahazia mwenye alikuwa na mamlaka ya kutawala ufalme huo.
10 Wakati Atalia,+ mama ya Ahazia, aliona kwamba mwana wake alikuwa amekufa, akasimama na kuharibu ukoo wote wa kifalme* wa nyumba ya Yuda.+ 11 Lakini, Yehoshabeati binti ya mufalme akamuchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia na akamuiba kutoka kati ya wana wa mufalme wenye walipaswa kuuawa, na akamuweka yeye pamoja na mutu wa kumulea katika chumba kimoja cha ndani cha kulala. Yehoshabeati binti ya Mufalme Yehoramu+ (alikuwa bibi ya Yehoyada+ kuhani na dada ya Ahazia) aliweza kumuficha ili Atalia asimuone, kwa hiyo hakumuua.+ 12 Akakaa pamoja nao kwa miaka sita (6), akiwa amefichwa kwenye nyumba ya Mungu wa kweli, wakati Atalia alikuwa anatawala juu ya inchi.