Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
25 Amazia alikuwa na miaka makumi mbili na tano (25) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka makumi mbili na kenda (29) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yehoadani wa Yerusalemu.+ 2 Aliendelea kufanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova, lakini hapana kwa moyo kamili. 3 Wakati tu ufalme ulikuwa imara chini ya uongozi wake, aliua watumishi wake wenye walikuwa wamemuua mufalme, baba yake.+ 4 Lakini hakuua wana wao, kwa maana alitenda kulingana na mambo yenye yameandikwa katika Sheria, katika kitabu cha Musa, ambamo Yehova aliamuru: “Baba hawapaswe kufa kwa sababu ya wana wao, na wana hawapaswe kufa kwa sababu ya baba zao; lakini kila mutu anapaswa kufa kwa sababu ya zambi yake mwenyewe.”+
5 Na Amazia akakusanya Yuda pamoja na kuwaagiza wasimame kulingana na jamaa za upande wa baba, kupitia wakubwa wa maelfu na kupitia wakubwa wa mamia kwa ajili ya Yuda wote na Benyamini.+ Akawaandikisha kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi,+ na akapata kwamba walikuwa wapiganaji-vita elfu mia tatu (300 000) wenye kuzoezwa* ili kutumika katika jeshi, wenye wanaweza kutumia mukuki na ngao kubwa. 6 Tena, alikodi wapiganaji-vita wenye nguvu elfu mia moja (100 000) kutoka Israeli kwa talanta* mia moja (100) za feza. 7 Lakini mutu fulani wa Mungu wa kweli akakuja kwake, na kusema: “Ee mufalme, usiache jeshi la Israeli liende pamoja na wewe, kwa maana Yehova haiko pamoja na Israeli,+ haiko pamoja na mutu yeyote kati ya Waefraimu. 8 Lakini uende peke yako, utende, na ukuwe hodari katika pigano. Tofauti na hilo, Mungu wa kweli anaweza kukufanya ujikwae mbele ya adui, kwa maana Mungu iko* na nguvu za kusaidia+ na za kufanya mutu ajikwae.” 9 Halafu Amazia akamuambia ule mutu wa Mungu wa kweli: “Lakini namna gani kuhusu zile talanta mia moja (100) zenye nimepatia maaskari wa Israeli?” Ule mutu wa Mungu wa kweli akajibu: “Yehova anaweza kukupatia nyingi zaidi kuliko hizo.”+ 10 Basi Amazia akaambia wale maaskari wenye walikuwa wamekuja kwake kutoka Efraimu waende, akawatuma waende kwao. Lakini, wakamukasirikia sana Yuda, basi wakarudia kwao wakiwa na kasirani kali.
11 Kisha Amazia akajipatia uhodari na akaongoza maaskari wake mwenyewe kwenye Bonde la Chumvi,+ na akapiga na kuua wanaume elfu kumi (10 000) wa Seiri.+ 12 Na watu wa Yuda wakakamata watu elfu kumi (10 000) wakiwa wazima. Basi wakawapeleka kwenye sehemu ya juu ya mwamba na kuwatupa chini kutoka kwenye sehemu hiyo ya juu ya mwamba, na wote wakavunjika vipande-vipande. 13 Lakini watu wa jeshi wenye Amazia alikuwa amerudisha wasiende pamoja naye katika vita+ walikuwa wanafanya mashambulizi juu ya miji ya Yuda, kuanzia Samaria+ mupaka Bet-horoni;+ walipiga na kuua watu elfu tatu (3 000) kati yao na kuchukua vitu vingi katika vita.
14 Lakini wakati Amazia alirudia kisha kupiga na kuua Waedomu, alileta miungu ya watu wa Seiri na kujisimamishia hiyo kuwa miungu,+ na akaanza kuinama mbele ya miungu hiyo na kuchoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya miungu hiyo. 15 Basi Yehova akamukasirikia sana Amazia, na akatuma nabii mwenye alimuambia: “Sababu gani unafuata miungu ya watu yenye haikuokoa watu wake kutoka katika mukono wako?”+ 16 Wakati alikuwa anazungumuza naye, mufalme akasema: “Je, tulikuweka kuwa mushauri wa mufalme?+ Acha!+ Sababu gani wakupige na kukuua?” Basi nabii huyo akaacha, lakini akaongezea: “Ninajua kwamba Mungu ameamua kukuharibu, kwa sababu umefanya vile na haukusikiliza shauri langu.”+
17 Kisha kufanya shauri pamoja na washauri wake, Mufalme Amazia wa Yuda akatuma ujumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mufalme wa Israeli, na kusema: “Kuja, tupambane katika pigano.”*+ 18 Mufalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mufalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba katika Lebanoni lilituma ujumbe kwa mwerezi katika Lebanoni, ‘Patia mwana wangu binti yako akuwe bibi yake.’ Hata hivyo, munyama wa pori wa Lebanoni akapita karibu na akakanyanga-kanyanga gugu hilo lenye miiba. 19 Umesema, ‘Angalia! Nimepiga* Edomu.’+ Basi moyo wako umekuwa na majivuno, unataka utukuzwe. Lakini sasa bakia katika nyumba yako mwenyewe.* Sababu gani ulete musiba na uanguke, na kuangusha Yuda pamoja na wewe?”
20 Lakini Amazia hakusikiliza,+ kwa maana jambo hilo lilitoka kwa Mungu wa kweli ili kuwatia katika mukono wa adui,+ kwa sababu walikuwa wamefuata miungu ya Edomu.+ 21 Basi Mufalme Yehoashi wa Israeli akapanda, naye pamoja na Mufalme Amazia wa Yuda wakapambana katika pigano kule Bet-shemeshi,+ yenye ni ya Yuda. 22 Yuda wakashindwa mbele ya Israeli, basi kila mumoja akakimbilia kwenye nyumba* yake. 23 Mufalme Yehoashi wa Israeli akamukamata Mufalme Amazia wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi,* kule Bet-shemeshi. Kisha akamuleta Yerusalemu na akatoboa tundu katika ukuta wa Yerusalemu kuanzia Mulango Mukubwa wa Efraimu+ mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Pembeni,+ urefu wa mikono mia ine (400).* 24 Akakamata zahabu yote na feza na vyombo vyote vyenye vilikuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli pamoja na* Obed-edomu na katika hazina za nyumba ya mufalme,+ na pia watu wenye walikamatwa. Kisha akarudia Samaria.
25 Amazia+ mwana wa Yehoashi mufalme wa Yuda aliishi miaka kumi na tano (15) kisha kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mufalme wa Israeli.+ 26 Na mambo mengine ya historia ya Amazia, kuanzia mwanzo mupaka mwisho, angalia! Je, hayaandikwe katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli? 27 Kuanzia wakati wenye Amazia aligeuka na kuacha kumufuata Yehova, walifanya mupango mubaya+ juu yake katika Yerusalemu, na akakimbilia Lakishi, lakini wakatuma watu wamufuatilie kule Lakishi na wakamuua kule. 28 Basi wakamubeba juu ya farasi na kumurudisha na wakamuzika pamoja na mababu zake katika muji wa Yuda.