Zaburi
33 Mupige vigelegele vya shangwe, kwa sababu ya Yehova, ninyi wenye haki.+
Ni jambo lenye kufaa kwa wanyoofu kumusifu yeye.
2 Mumushukuru Yehova kwa kinubi;
Mumuimbie sifa* kwa chombo cha kamba kumi (10).
3 Mumuimbie wimbo mupya;+
Mupige kamba kwa ufundi, pamoja na vigelegele vya shangwe.
4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+
Na kila jambo lenye anafanya linategemeka.
5 Anapenda uadilifu* na haki.+
Dunia imejaa upendo mushikamanifu wa Yehova.+
6 Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa,+
Na kwa roho* ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.*
7 Anakusanya maji ya bahari kama vile ukuta wa maji;+
Anatia maji yenye mawimbi makubwa katika madepo.
8 Dunia yote imuogope Yehova.+
Wakaaji wa inchi yenye kuzaa wamuogope sana.
13 Yehova anaangalia chini akiwa mbinguni;
Anaona wana wote wa binadamu.+
14 Akiwa katika makao yake,
Anakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anaumba mioyo ya wote;
Anachunguza kazi zao zote.+
16 Hakuna mufalme mwenye anaokolewa kupitia jeshi kubwa;+
Mutu mwenye nguvu haokolewe kupitia nguvu zake nyingi.+
18 Angalia! Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa,+
Wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu,
Na kulinda uzima wao wakati wa njaa.+
20 Tunamungojea* Yehova.
Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu inashangilia katika yeye,
Kwa maana tunategemea jina lake takatifu.+