Zaburi
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.*
58 Je, munaweza kuzungumuza kuhusu haki wakati mumenyamaza?+
Je, munaweza kuhukumu kwa unyoofu, ninyi wana wa binadamu?+
2 Kuliko kufanya vile, munapanga ukosefu wa haki katika moyo wenu,+
Na mikono yenu inaeneza jeuri katika inchi.+
5 Hatasikiliza sauti ya watu wenye kuchezesha nyoka,
Hata wafanye uchawi kwa ufundi namna gani.
6 Ee Mungu, vunja meno yao katika vinywa vyao!
Vunja mataya* ya simba hawa,* Ee Yehova!
7 Acha waishe kama maji yenye kukauka.
Acha Yeye akunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.
8 Acha wakuwe kama konokono mwenye anayeyuka wakati anatembea;
Kama mutoto mwenye alikufia katika tumbo la mwanamuke na mwenye haone jua hata kidogo.
9 Mbele vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za muti wa mukwamba,
Ataharibu umajimaji na tawi lenye kuwaka, kama kwa upepo wa zoruba.+
11 Kisha watu watasema: “Hakika kuko zawabu kwa ajili ya mwenye haki.+
Kwa kweli kuko Mungu mwenye anahukumu katika dunia.”+