Zaburi
Muziki wa Daudi, wakati alikuwa katika jangwa la Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+
2 Kwa hiyo nimekuangalia katika mahali patakatifu;
Nimeona nguvu zako na utukufu wako.+
4 Basi nitakusifu maisha yangu yote;
Katika jina lako nitainua mikono yangu.
5 Nimetosheka* na fungu bora lenye kuwa la muzuri kabisa,*
Kwa hiyo kinywa changu kitakusifu kwa midomo yenye shangwe.+
6 Ninakukumbuka wewe nikiwa kwenye kitanda changu;
7 Kwa maana wewe ni musaidizi wangu,+
Nami ninapiga vigelegele vya shangwe katika kivuli cha mabawa yako.+
9 Lakini wale wenye kutafuta kuharibu uzima wangu*
Watashuka katika sehemu za chini kabisa za dunia.
10 Watatiwa katika nguvu za upanga;
Watakuwa chakula cha mbweha.
11 Lakini mufalme atashangilia katika Mungu.
Kila mutu mwenye anaapa katika jina Lake atashangilia,*
Kwa maana kinywa cha wenye kusema uongo kitanyamazishwa.