Zaburi
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Ya Asafu.+
81 Mumupigie Mungu, nguvu zetu, vigelegele vya shangwe.+
Mumupigie Mungu wa Yakobo vigelegele vya ushindi.
2 Muanzishe muziki na kukamata ngoma ya kidogo,*
Kinubi chenye mulio mutamu pamoja na chombo cha kamba.
3 Mupige baragumu wakati wa mwezi mupya,+
Wakati wa mwezi wenye kuenea, kwa ajili ya siku ya sikukuu yetu.+
4 Kwa maana ni agizo kwa ajili ya Israeli,
Sheria ya Mungu wa Yakobo.+
Nilisikia sauti* yenye sikutambua:
6 “Niliinua muzigo kutoka kwenye bega lake;+
Mikono yake iliwekwa huru kutoka kwenye kitunga.
Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba.*+ (Sela)
8 Musikie, watu wangu, na nitatoa ushahidi juu yenu.
Ee Israeli, kama tu utanisikiliza.+
9 Kati yenu, hakutakuwa mungu yeyote wa kigeni;
Na hamutamuinamia mungu wa kigeni.+
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,
Mwenye alikutosha katika inchi ya Misri.+
Fungua wazi kinywa chako, na nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza sauti yangu;
Israeli hakujitiisha kwangu.+
14 Ningetiisha haraka maadui wao;
Ningegeuza mukono wangu ili kushambulia wapinzani wao.+
15 Wale wenye kumuchukia Yehova watajikunja mbele yake,
Na mwisho* wao utakuwa wa milele.