Muziki wa Asafu.+
82 Mungu anakamata nafasi yake katika mukusanyiko wa kimungu;+
Anahukumu katikati ya miungu:+
2 “Mutaendelea kuhukumu bila haki mupaka wakati gani+
Na kupendelea waovu?+ (Sela)
3 Mutetee mutu wa hali ya chini na mwenye hana baba.+
Mutendee kwa haki mutu mwenye hana uwezo na maskini.+
4 Mumuokoe mutu wa hali ya chini na maskini;
Muwaokoe katika mukono wa muovu.”
5 Hawajue wala hawaelewe;+
Wanatembea huku na huku katika giza;
Misingi yote ya dunia inatikiswa.+
6 “Mimi nimesema, ‘Ninyi ni miungu,+
Ninyi wote muko wana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi.
7 Lakini mutakufa kama vile wanadamu wanakufa;+
Na mutaanguka kama vile mukubwa mwingine yeyote!’”+
8 Simama, Ee Mungu, na uhukumu dunia,+
Kwa maana mataifa yote ni yako.