Zaburi
95 Mukuje, tumupigie Yehova vigelegele vya shangwe!
Tumupigie vigelegele vya ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mukubwa,
Mufalme mukubwa juu ya miungu mingine yote.+
4 Sehemu za chini kabisa za dunia ziko katika mukono wake;
Vichwa vya milima ni vyake.+
6 Mukuje, tuabudu na kuinama;
Tupige magoti mbele ya Yehova Mutengenezaji wetu.+
Leo kama munasikiliza sauti yake,+
8 Musifanye moyo wenu kuwa mugumu kama vile mulifanya kule Meriba,*+
Kama katika siku ya Masa* katika jangwa,+
9 Wakati mababu zenu walinijaribu;+
Wakanipima, hata kama walikuwa wameona kazi zangu.+
10 Kwa miaka makumi ine (40) nilichukizwa na kizazi hicho, na nikasema:
“Wao ni watu wenye kupotoka sikuzote katika mioyo yao;
Hawajafikia kujua njia zangu.”
11 Kwa hiyo niliapa katika kasirani yangu:
“Hawataingia katika pumuziko langu.”+