Zaburi
99 Yehova amekuwa Mufalme.+ Acha vikundi vya watu vitetemeke.
Anakaa akiwa mufalme juu ya* makerubi.+ Acha dunia itikisike.
3 Acha wasifu jina lako kubwa,+
Kwa maana ni lenye kuogopesha sana na liko takatifu.
4 Yeye ni mufalme mwenye nguvu ambaye anapenda haki.+
Umefanya mambo manyoofu yakuwe imara kabisa.
Umeleta haki na uadilifu*+ katika Yakobo.
6 Musa na Haruni walikuwa kati ya makuhani wake,+
Na Samweli alikuwa kati ya wale wenye walikuwa wanaitia jina lake.+
Walikuwa wanamuita Yehova,
Na alikuwa anawajibu.+
7 Alikuwa anasema nao kutoka katika nguzo ya wingu.+
Walishika vikumbusho vyake na agizo lenye aliwapatia.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+