Zaburi
3 Mujisifu juu ya jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wenye kumutafuta Yehova ishangilie.+
4 Mumutafute Yehova+ na nguvu zake.
Mutafute uso* wake bila kuacha.
5 Mukumbuke kazi za ajabu zenye amefanya,
Miujiza yake na hukumu zenye ametangaza,+
6 Ninyi uzao wa* Abrahamu mutumishi wake,+
Ninyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko katika dunia yote.+
8 Anakumbuka agano lake milele,+
Ahadi yenye alitoa,* mupaka vizazi elfu,+
9 Agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu,+
Na kiapo chenye alimuapia Isaka,+
10 Chenye aliweka kuwa amri kwa Yakobo
Na kuwa agano la kudumu kwa Israeli,
11 Akisema, “Nitakupatia inchi ya Kanaani+
Kuwa uriti wenu wenye muligawiwa.”+
12 Ilikuwa vile wakati walikuwa hesabu kidogo,+
Ndiyo, kidogo sana, na walikuwa wageni katika inchi.+
13 Walitembea-tembea kutoka taifa moja mupaka taifa lingine,
Kutoka ufalme mumoja mupaka kikundi kingine cha watu.+
14 Hakumuruhusu mutu yeyote awakandamize,+
Lakini kwa sababu yao alikaripia wafalme,+
15 Kwa kusema, “Musiguse watiwa-mafuta wangu,
Na musitendee manabii wangu jambo lolote la mubaya.”+
17 Alituma mutu mumoja awatangulie
Mwenye aliuzishwa ili kuwa mutumwa, Yosefu.+
18 Walifunga* miguu yake kwa pingu,+
Shingo yake ilitiwa katika vyuma;*
19 Mupaka wakati neno lake lilitimia,+
Neno la Yehova ndilo lilimusafisha.
20 Mufalme alituma watu wamufungue,+
Mutawala wa vikundi vya watu alimuweka huru.
21 Akamufanya kuwa bwana wa nyumba yake,
Mutawala juu ya mali zake zote,+
22 Ili akuwe na mamlaka juu ya* wakubwa wake namna alipenda*
Na ili afundishe wazee wake hekima.+
23 Kisha Israeli akaingia Misri,+
Na Yakobo akakaa akiwa mugeni katika inchi ya Hamu.
24 Mungu alifanya watu wake waongezeke sana;+
Aliwafanya wakuwe na nguvu kuliko wapinzani wao,+
25 Aliruhusu mioyo yao ibadilike ili wachukie watu wake,
Ili wafanye mupango mubaya juu ya watumishi wake.+
27 Walifanya alama zake kati yao,
Miujiza yake katika inchi ya Hamu.+
28 Alituma giza na inchi ikakuwa giza;+
Hawakuasi maneno yake.
29 Alibadilisha maji yao kuwa damu
Na kuua samaki wao.+
30 Inchi yao ikajaa vyura,+
Hata katika vyumba vya kifalme.
31 Aliagiza mainzi wavamie
Na imbu katika maeneo yao yote.+
33 Alipiga mizabibu yao na miti yao ya tini
Na kuvunja-vunja miti ya eneo lao.
34 Alisema nzige wavamie,
Nzige wadogo wenye hawakukuwa na hesabu.+
35 Walikula mimea yote katika inchi,
Na walimeza mazao ya udongo.
36 Kisha akapiga na kuua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi yao,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.
37 Alipeleka watu wake inje wakiwa na feza na zahabu;+
Na hakuna mutu yeyote kati ya makabila yake mwenye alijikwaa.
39 Alitandika wingu ili liwafunike+
Na moto ili utoe mwangaza wakati wa usiku.+
42 Kwa maana alikumbuka ahadi takatifu yenye alimupatia Abrahamu mutumishi wake.+
43 Kwa hiyo akatosha watu wake wakishangilia,+
Alitosha wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.
44 Aliwapatia inchi za mataifa;+
Waliriti vitu vyenye vikundi vingine vya watu vilikuwa vimetumika sana ili kuvitengeneza,+
45 Ili watii maagizo yake+
Na kushika sheria zake.
Mumusifu Yah!*