Zaburi
KITABU CHA TANO
(Zaburi 107-150)
2 Acha wale wenye walikombolewa* na Yehova waseme jambo hilo,
Wale wenye alikomboa katika mukono wa* mupinzani,+
3 Wale wenye alikusanya pamoja kutoka katika inchi mbalimbali,+
Kutoka mashariki na kutoka mangaribi,*
Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+
4 Walitanga-tanga katika nyika, katika jangwa;
Hawakupata njia ya kuenda katika muji kwenye wangeweza kuishi.
5 Walikuwa na njaa na kiu;
Walizimia* kwa sababu ya kuchoka sana.
8 Watu wamushukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.+
10 Wamoja kati yao walikuwa wanaishi katika giza nzito sana,
Wafungwa katika mateso na vyuma.
11 Kwa maana walikuwa wameasi neno la Mungu;
Hawakuheshimia shauri la Mwenye Kuwa Juu Zaidi.+
12 Kwa hiyo alinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+
Walijikwaa, na hapakukuwa mutu yeyote wa kuwasaidia.
13 Walimuomba Yehova awasaidie katika taabu yao;
Akawaokoa katika shida yao.
14 Aliwatosha katika giza nzito sana,
Na kukata pingu zao.+
15 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu+
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.
18 Walipoteza hamu ya kula* vyakula vyote;
Walikaribia milango mikubwa ya kifo.
19 Walikuwa wanamuomba Yehova awasaidie katika taabu yao;
Na alikuwa anawaokoa katika shida yao.
20 Alikuwa anatuma neno lake na kuwaponyesha+
Na kuwaokoa katika mashimo yenye walikuwa wamenaswa ndani.
21 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.
22 Acha watoe zabihu za shukrani+
Na kutangaza kazi zake kwa vigelegele vya shangwe.
23 Wale wenye kusafiri kwa mashua* juu ya bahari,
Wenye kufanya biashara yao juu ya maji mengi,+
24 Wameona kazi za Yehova
Na kazi zake za ajabu katika mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana;+
25 Namna zoruba yenye upepo mukali inainuka kwa neno lake,+
Na kuinua mawimbi ya bahari.
26 Wanapanda juu mupaka kwenye anga;
Wanashuka mupaka katika sehemu za chini kabisa.
Uhodari wao unayeyuka* kwa sababu ya musiba wenye kukaribia.
27 Wanayumba-yumba na kuenda huku na huku kama mulevi,
Na ufundi wao wote unakuwa hauna mafaa yoyote.+
28 Kisha wanamulilia Yehova kwa sauti kubwa katika taabu yao,+
Na anawaokoa katika shida yao.
29 Anatuliza zoruba yenye upepo mukali;
Mawimbi ya bahari yananyamaza.+
30 Wanashangilia wakati yanatulia,
Na anawaongoza mupaka kwenye bandari* yenye wanatamani.
31 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.+
33 Anageuza mito kuwa jangwa,
Na chemchemi za maji kuwa udongo wenye kukauka,+
34 Eneo lenye kuzaa kuwa eneo lenye chumvi ambalo limeachwa,+
Kwa sababu ya uovu wa wale wenye kukaa ndani yake.
35 Anageuza jangwa kuwa viziwa vya maji vyenye matete,
Na inchi kavu kuwa chemchemi za maji.+
38 Anawabariki na wanaongezeka sana;
Haache ngombe wao wapunguke.+
39 Lakini tena wanakuwa kidogo na kunyenyekezwa
Kwa sababu ya ukandamizaji, musiba, na huzuni.
40 Anamwanga zarau juu ya watu wenye vyeo
Na kuwafanya watange-tange kwenye hakuna njia katika maeneo yenye yameachwa.+
41 Lakini analinda* maskini ili wasikandamizwe+
Na kufanya familia zao zikuwe nyingi sana kama kundi.