Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
109 Ee Mungu mwenye ninasifu,+ usibakie kimya.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananifungulia vinywa vyao.
Wanasema kunihusu kwa ndimi za uongo;+
3 Wananizunguka na maneno ya chuki,
Na wananishambulia bila sababu.+
4 Wananipinga hata kama mimi ninawapenda;+
Lakini ninaendelea kusali.
5 Wananilipa ubaya kwa wema.+
Na chuki kwa upendo wangu.+
6 Weka mutu muovu juu yake;
Acha mupinzani* asimame kwenye mukono wake wa kuume.
9 Acha watoto* wake wakuwe bila baba,
Na bibi yake akuwe mujane.
10 Acha watoto* wake wakuwe watu wenye kutanga-tanga wakiomba-omba,
Wakitafuta chakula mbali na nyumba zao zenye kuharibiwa.
12 Mutu yeyote asimutendee kwa fazili,*
Na mutu yeyote asionyeshe wema watoto wake wenye hawana baba.
14 Yehova akumbuke kosa la mababu zake,+
Na zambi ya mama yake isifutwe.
15 Yehova aendelee kukumbuka mambo yenye wamefanya;
Na aondoe kumbukumbu lao lisikuwe tena katika dunia.+
16 Kwa maana hakukumbuka kuonyesha fazili,*+
Lakini aliendelea kumufuatilia mutu mwenye kukandamizwa,+ maskini, na mutu mwenye kuvunjika moyo
Ili amuue.+
17 Alipenda kulaani, kwa hiyo laana hiyo ikamupata;
Hakutaka kubariki, kwa hiyo hakupata baraka yoyote.
18 Alivalishwa laana kama nguo yake.
Na laana hizo zikamwangwa katika mwili wake kama maji,
Katika mifupa yake kama mafuta.
20 Hayo ndiyo malipo kutoka kwa Yehova ya mutu mwenye kunipinga+
Na ya wale wenye kusema mambo maovu juu yangu.*
21 Lakini wewe, Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi,
Tenda kwa faida yangu kwa ajili ya jina lako.+
Uniokoe, kwa sababu upendo wako mushikamanifu ni mwema.+
23 Ninapitilia mbali kama kivuli chenye kufifia;
Nimekungutwa kama nzige.
24 Magoti yangu yanaregea kwa sababu ya kufunga;
Mwili wangu umekonda, na ninaendelea kuwa muzaifu.*
25 Nimekuwa kitu chao cha kuchokoza.+
Wakati wananiona, wanatikisa vichwa vyao.+
26 Unisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;
Uniokoe kupitia upendo wako mushikamanifu.
27 Wajue kwamba mukono wako ndio ulitenda hili;
Kwamba wewe, Ee Yehova, umetenda hili.
28 Watangaze laana, lakini wewe utoe baraka.
Wapatishwe haya wakati wanasimama ili kunishambulia,
Lakini mutumishi wako ashangilie.
30 Kinywa changu kitamusifu Yehova kwa bidii;
Nitamusifu mbele ya watu wengi.+