Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda.
132 Ee Yehova, umukumbuke Daudi
Na mateso yake yote;+
2 Namna alimuapia Yehova,
Namna alimuwekea naziri Mwenye Nguvu wa Yakobo:+
3 “Sitaingia katika hema yangu, katika nyumba yangu.+
Sitalala kwenye kiti changu, kwenye kitanda changu;
4 Sitaruhusu macho yangu yalale usingizi,
Wala kope zangu zisinzie
5 Mupaka wakati nitapata mahali kwa ajili ya Yehova,
9 Makuhani wako wavae haki,
Na washikamanifu wako wapige vigelegele vya shangwe.
11 Yehova amemuapia Daudi;
Hakika hatakosa kutimiza neno lake:
12 Kama wana wako wanashika agano langu
Na vikumbusho vyangu vyenye ninawafundisha,+
Wana wao pia
Watakaa kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+
14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumuzikia milele;
Nitakaa hapa,+ kwa maana hiyo ndiyo tamaa yangu.
15 Nitapabariki sana kwa vyakula;
Nitashibisha maskini wake kwa mikate.+
17 Kule nitafanya nguvu za Daudi zikomae.*
Nimetayarisha taa kwa ajili ya mutiwa-mafuta wangu.+
18 Nitavalisha maadui wake haya,
Lakini taji lenye kuwa kwenye kichwa chake litasitawi.”+