Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
140 Uniokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;
Unilinde kutoka kwa watu wenye jeuri,+
2 Wale wenye kufanya mipango ya uovu katika mioyo yao+
Na kuchochea ugomvi muchana wote.
4 Unilinde, Ee Yehova, kutokana na mikono ya waovu;+
Unilinde kutokana na watu wenye jeuri,
Wale wenye kufanya mupango wa kunifanya nijikwae.
Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)
6 Ninamuambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.
Sikiliza, Ee Yehova, vilio vyangu vya kuomba musaada.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,
Wewe unalinda kichwa changu katika siku ya vita.+
8 Ee Yehova, usitimize tamaa za waovu.
Usiruhusu mipango yao mibaya ifanikiwe, ili wasijiinue.+ (Sela)
9 Vichwa vya wale wenye kunizunguka
Vifunikwe na uovu wenye kusemwa na midomo yao.+
10 Makaa yenye kuwaka yawanyeshee.+
11 Muchongezi asipate makao juu ya dunia.*+
Uovu ufuatilie watu wenye jeuri na uwapige na kuwaua.
12 Ninajua kwamba Yehova atatetea watu wa hali ya chini
Na kupatia maskini haki.+