Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 23
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Yeremia

      • Wachungaji wazuri na wabaya (1-4)

      • Usalama chini ya “chipukizi la haki” (5-8)

      • Manabii wa uongo wanalaumiwa (9-32)

      • “Muzigo” wa Yehova (33-40)

Yeremia 23:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 10:21; 50:6; Eze 34:2

Yeremia 23:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 34:5

Yeremia 23:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 11:11; 35:10; Yer 29:14; 31:8
  • +Yer 50:19; Eze 34:14; Mik 2:12
  • +Kum 30:3, 5; Amo 9:14; Zek 10:8

Yeremia 23:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 3:15; Yoh 21:15; Mdo 20:28

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Yeremia,

    uku. 129-130

Yeremia 23:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “muriti wa.”

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 11:1; 53:2; Yer 33:15, 16; Zek 3:8; Mt 2:23
  • +Lu 1:32, 33
  • +Isa 9:7; 11:3, 4; 32:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Yeremia, uku. 173

Yeremia 23:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zek 10:6
  • +Kum 33:28; Yer 32:37; Zek 14:11
  • +Isa 54:17

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Yeremia, uku. 173

Yeremia 23:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 16:14, 15

Yeremia 23:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 43:5; Eze 34:13; Sef 3:20

Yeremia 23:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 3:8, 9; 5:7; 13:27; Eze 22:11
  • +Isa 24:4; Yoe 1:10
  • +Yer 12:4

Yeremia 23:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ni waasi-imani.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 28:7; Yer 5:31; 6:13; Eze 22:25; Sef 3:4
  • +2Nya 33:1, 5; 36:14; Yer 7:11; Eze 8:10, 11; 23:39

Yeremia 23:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 13:16

Yeremia 23:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 16:46

Yeremia 23:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Wanatia nguvu mikono ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 29:21, 23
  • +Yer 23:26
  • +Isa 3:9
  • +Mwa 18:20; Kum 32:32; Isa 1:10; Yud 7

Yeremia 23:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 8:14; 9:15

Yeremia 23:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Wanawajaza ninyi na matumaini ya uongo.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 27:9; 29:8
  • +Omb 2:14
  • +Yer 14:14; Eze 13:3; 22:28

Yeremia 23:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 4:10; 6:13, 14; 8:11; Eze 13:10
  • +Mik 3:11

Yeremia 23:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 25:32; 30:23, 24

Yeremia 23:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 14:14; 27:15; 29:8, 9

Yeremia 23:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 25:4, 5

Yeremia 23:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 16:7, 13; Mez. 15:3; Amo 9:2; Ebr 4:13
  • +Zab 139:7

Yeremia 23:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 18:20; Yer 27:9; 29:21, 23

Yeremia 23:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 14:14

Yeremia 23:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 3:7; 2 Fal. 21:1, 3

Yeremia 23:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “hama, marteau.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 5:14
  • +Ebr 4:12

Yeremia 23:30

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 18:20; Yer 14:15; Eze 13:2, 3

Yeremia 23:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 13:7

Yeremia 23:32

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Sef 3:4
  • +Yer 7:8; Omb 2:14

Yeremia 23:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Ujumbe wenye kuchokesha.” Neno hilo la Kiebrania liko na maana mbili: “ujumbe muzito kutoka kwa Mungu” ao “kitu chenye kuchokesha.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 12:7

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/3/2007, uku. 11

Yeremia 23:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

Yeremia 23:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

  • *

    Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

Yeremia 23:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Ujumbe wenye kuchokesha.”

  • *

    Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

  • *

    Ao “Ujumbe wenye kuchokesha.”

Yeremia 23:40

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 24:9; 42:18; Omb 5:20; Da. 9:16

Maandiko ingine

Yer. 23:1Yer 10:21; 50:6; Eze 34:2
Yer. 23:2Eze 34:5
Yer. 23:3Isa 11:11; 35:10; Yer 29:14; 31:8
Yer. 23:3Yer 50:19; Eze 34:14; Mik 2:12
Yer. 23:3Kum 30:3, 5; Amo 9:14; Zek 10:8
Yer. 23:4Yer 3:15; Yoh 21:15; Mdo 20:28
Yer. 23:5Isa 11:1; 53:2; Yer 33:15, 16; Zek 3:8; Mt 2:23
Yer. 23:5Lu 1:32, 33
Yer. 23:5Isa 9:7; 11:3, 4; 32:1
Yer. 23:6Zek 10:6
Yer. 23:6Kum 33:28; Yer 32:37; Zek 14:11
Yer. 23:6Isa 54:17
Yer. 23:7Yer 16:14, 15
Yer. 23:8Isa 43:5; Eze 34:13; Sef 3:20
Yer. 23:10Yer 3:8, 9; 5:7; 13:27; Eze 22:11
Yer. 23:10Isa 24:4; Yoe 1:10
Yer. 23:10Yer 12:4
Yer. 23:11Isa 28:7; Yer 5:31; 6:13; Eze 22:25; Sef 3:4
Yer. 23:112Nya 33:1, 5; 36:14; Yer 7:11; Eze 8:10, 11; 23:39
Yer. 23:12Yer 13:16
Yer. 23:13Eze 16:46
Yer. 23:14Yer 29:21, 23
Yer. 23:14Yer 23:26
Yer. 23:14Isa 3:9
Yer. 23:14Mwa 18:20; Kum 32:32; Isa 1:10; Yud 7
Yer. 23:15Yer 8:14; 9:15
Yer. 23:16Yer 27:9; 29:8
Yer. 23:16Omb 2:14
Yer. 23:16Yer 14:14; Eze 13:3; 22:28
Yer. 23:17Yer 4:10; 6:13, 14; 8:11; Eze 13:10
Yer. 23:17Mik 3:11
Yer. 23:19Yer 25:32; 30:23, 24
Yer. 23:21Yer 14:14; 27:15; 29:8, 9
Yer. 23:22Yer 25:4, 5
Yer. 23:24Mwa 16:7, 13; Mez. 15:3; Amo 9:2; Ebr 4:13
Yer. 23:24Zab 139:7
Yer. 23:25Kum 18:20; Yer 27:9; 29:21, 23
Yer. 23:26Yer 14:14
Yer. 23:27Amu 3:7; 2 Fal. 21:1, 3
Yer. 23:29Yer 5:14
Yer. 23:29Ebr 4:12
Yer. 23:30Kum 18:20; Yer 14:15; Eze 13:2, 3
Yer. 23:31Eze 13:7
Yer. 23:32Sef 3:4
Yer. 23:32Yer 7:8; Omb 2:14
Yer. 23:33Yer 12:7
Yer. 23:40Yer 24:9; 42:18; Omb 5:20; Da. 9:16
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia 23:1-40

Yeremia

23 “Ole wao wachungaji wenye kuharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” ni vile Yehova anasema.+

2 Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya wachungaji wenye wanachunga watu wangu: “Mumetawanya kondoo wangu; muliendelea kuwatawanya, na hamukuwaelekezea uangalifu.”+

“Basi nitawaelekezea ninyi uangalifu wangu kwa sababu ya matendo yenu maovu,” ni vile Yehova anasema.

3 “Kisha nitakusanya pamoja mabaki ya kondoo zangu kutoka katika inchi zote kwenye nilikuwa nimewatawanya,+ na nitawarudisha kwenye malisho yao,+ na watazaa na kuwa wengi.+ 4 Na nitasimamisha juu yao wachungaji wenye kwa kweli watawachunga.+ Hawataogopa tena wala kutetemeshwa, na hakuna mwenye atakosekana,” ni vile Yehova anasema.

5 “Angalia! Siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati nitasimamishia Daudi chipukizi la* haki.+ Na mufalme atatawala+ na kuonyesha ufahamu na kutenda haki na uadilifu* katika inchi.+ 6 Katika siku zake Yuda ataokolewa,+ na Israeli atakaa kwa usalama.+ Na hili ndilo jina lenye ataitwa: Yehova Ni Haki Yetu.”+

7 “Hata hivyo, siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati hawatasema tena, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha watu wa Israeli katika inchi ya Misri!’+ 8 lakini tofauti na hilo, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha na kurudisha wazao wa nyumba ya Israeli katika inchi ya kaskazini na katika inchi zote kwenye nilikuwa nimewatawanya,’ na watakaa katika inchi yao wenyewe.”+

9 Kuhusu manabii:

Moyo wangu umevunjika ndani yangu.

Mifupa yangu yote inatetemeka.

Mimi ni kama mutu mwenye kulewa

Na kama mutu mwenye amelemewa na divai,

Kwa sababu ya Yehova na kwa sababu ya maneno yake matakatifu.

10 Kwa maana inchi imejaa wazinifu;+

Kwa sababu ya laana inchi inaomboleza+

Na malisho ya jangwa yamekauka.+

Njia yao ni ya uovu, na wanatumia nguvu zao mubaya.

11 “Nabii pamoja na kuhani wamechafuliwa.*+

Hata katika nyumba yangu mwenyewe nimepata uovu wao,”+ ni vile Yehova anasema.

12 “Basi njia yao itakuwa na uterezi na giza;+

Watasukumwa na wataanguka.

Kwa maana nitaleta musiba juu yao

Katika mwaka wa kuomba hesabu,” ni vile Yehova anasema.

13 “Na katika manabii wa Samaria+ nimeona jambo lenye kuchukiza.

Unabii wao unachochewa na Baali,

Na wanapotosha watu wangu Israeli.

14 Na katika manabii wa Yerusalemu nimeona mambo yenye kuchukiza sana.

Wanafanya uzinifu+ na kutembea katika uongo;+

Wanatia moyo* watenda-maovu,

Na hawageuke na kuacha uovu wao.

Kwangu wote ni kama Sodoma,+

Na wakaaji wake ni kama Gomora.”+

15 Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi juu ya manabii:

“Angalia, ninawafanya wakule pakanga

Na kuwapatia maji yenye sumu wakunywe.+

Kwa maana kutoka kwa manabii wa Yerusalemu uasi-imani umeenea katika inchi yote.”

16 Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Musisikilize maneno ya manabii wenye wanawatolea ninyi unabii.+

Wanawadanganya ninyi.*

Maono yenye wanasema yanatoka katika moyo wao wenyewe,+

Hapana katika kinywa cha Yehova.+

17 Wanaambia tena na tena wale wenye hawaniheshimie,

‘Yehova amesema: “Mutakuwa na amani.”’+

Na kila mutu mwenye anafuata moyo wake mwenyewe mugumu wanamuambia,

‘Hakuna musiba wowote wenye utakuja juu yako.’+

18 Kwa maana ni nani mwenye amesimama katika kikundi cha marafiki wa karibu wa Yehova

Ili aone na kusikia neno lake?

Ni nani mwenye amekazia uangalifu neno lake ili alisikie?

19 Angalia! Zoruba yenye upepo mukali ya Yehova italipuka kwa kasirani kali;

Kama zoruba kali yenye kuzunguka-zunguka itazunguka juu ya kichwa cha waovu.+

20 Kasirani ya Yehova haitarudia nyuma

Mupaka wakati atakuwa ametenda na kutimiza makusudi ya moyo wake.

Katika kipindi cha mwisho cha zile siku ninyi mutaelewa jambo hilo waziwazi.

21 Sikutuma manabii, lakini walikimbia.

Sikusema nao, lakini walitoa unabii.+

22 Lakini kama wangekuwa wamesimama katika kikundi changu cha marafiki wa karibu,

Wangekuwa wamefanya watu wangu wasikie maneno yangu

Na wangekuwa wamefanya warudie kutoka kwenye njia yao ya mubaya na matendo yao maovu.”+

23 “Je, mimi ni Mungu mwenye kuwa karibu tu,” ni vile Yehova anasema, “na pia siko Mungu kutoka mbali?”

24 “Je, mutu yeyote anaweza kujificha mahali pa siri kwenye siwezi kumuona?”+ ni vile Yehova anasema.

“Je, mimi sijaze mbingu na dunia?”+ ni vile Yehova anasema.

25 “Nimesikia manabii wenye wanatoa unabii wa uongo katika jina langu wakisema, ‘Niliota ndoto! Niliota ndoto!’+ 26 Jambo hili litaendelea mupaka wakati gani katika moyo wa manabii, kutoa unabii wa uongo? Wao ni manabii wa udanganyifu wa moyo wao wenyewe.+ 27 Wanakusudia kufanya watu wangu wasahau jina langu kupitia ndoto zenye wanaelezeana, kama vile baba zao walisahau jina langu kwa sababu ya Baali.+ 28 Acha nabii mwenye kuwa na ndoto aeleze ndoto hiyo, lakini ule mwenye kuwa na neno langu anapaswa kusema neno langu kwa ukweli.”

“Nyasi iko na uhusiano gani na nafaka?” ni vile Yehova anasema.

29 “Je, neno langu haliko kama vile moto,”+ ni vile Yehova anasema, “na kama nyundo* ya chuma yenye inavunja mwamba?”+

30 “Basi angalia, ninapinga manabii,” ni vile Yehova anasema, “wenye wanaiba maneno yangu kila mumoja kutoka kwa mwenzake.”+

31 “Angalia, ninapinga manabii,” ni vile Yehova anasema, “wale wenye wanatumia ulimi wao kusema, ‘Anasema!’”+

32 “Angalia, ninapinga manabii wa ndoto za uongo,” ni vile Yehova anasema, “wenye wanazieleza na kupotosha watu wangu kwa sababu ya uongo wao na kujisifu kwao.”+

“Lakini sikuwatuma wala kuwaamuru. Basi hawataletea watu hawa faida hata kidogo,”+ ni vile Yehova anasema.

33 “Na wakati watu hawa ao nabii ao kuhani wanakuuliza, ‘Muzigo* wa Yehova ni nini?’ unapaswa kuwajibu, ‘“Ninyi watu ndio muzigo! Na mimi nitawatupa ninyi,”+ ni vile Yehova anasema.’ 34 Na kuhusu nabii ao kuhani ao watu wenye wanasema, ‘Huu ndio muzigo* wa Yehova!’ Nitakaza uangalifu wangu juu ya mutu huyo na juu ya nyumba yake. 35 Ni hivi kila mumoja wenu anamuambia mwenzake na pia ndugu yake: ‘Yehova ametoa jibu gani? Na Yehova amesema nini?’ 36 Lakini musitaje tena muzigo* wa Yehova, kwa maana muzigo* ni neno la kila mutu mwenyewe, na mumebadilisha maneno ya Mungu mwenye kuishi, Yehova wa majeshi, Mungu wetu.

37 “Utamuambia nabii huyo hivi: ‘Yehova amekupatia jibu gani? Na Yehova amesema nini? 38 Na kama munaendelea kusema, “Muzigo* wa Yehova!” Yehova anasema hivi: “Kwa sababu munasema, ‘Neno hili ndilo muzigo* wa Yehova,’ kisha mimi kuwaambia ninyi, ‘Hamupaswe kusema: “Muzigo* wa Yehova!”’ 39 muangalie! Nitawanyangula ninyi na kuwatupa mbali kutoka mbele yangu, ninyi pamoja na muji wenye niliwapatia ninyi na mababu zenu. 40 Na nitaleta juu yenu haya ya milele na fezeha ya milele, yenye haitasahauliwa.”’”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine