Yeremia
30 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Andika katika kitabu maneno yote yenye ninakuambia. 3 Kwa maana “angalia! siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati nitakusanya watu wangu wenye walikamatwa mateka, Israeli na Yuda,”+ ni vile Yehova anasema, “na nitawarudisha katika inchi yenye nilipatia mababu zao, na watairiti tena.”’”+
4 Haya ndiyo maneno yenye Yehova aliambia Israeli na Yuda.
5 Yehova anasema hivi:
“Tumesikia sauti za kutetemeka;
Kuko woga, na hakuna amani.
6 Muulize, tafazali, kama mwanaume anaweza kuzaa.
Basi, sababu gani ninaona kila mwanaume mwenye nguvu akishika tumbo lake*
Kama mwanamuke mwenye kuzaa?+
Sababu gani kila uso umegeuka rangi?
7 Ole! Kwa maana siku hiyo ni yenye kuogopesha.*+
Hakuna ingine kama hiyo,
Wakati wa taabu kwa Yakobo.
Lakini ataokolewa kutokana nayo.”
8 “Na katika siku hiyo,” ni vile Yehova wa majeshi anasema, “nitavunja nira kutoka kwenye shingo yako, na vifungio vyako nitavikata* katika sehemu mbili; na wageni* hawatamufanya* tena kuwa mutumwa wao. 9 Watatumikia Yehova Mungu wao na Daudi mufalme wao, mwenye nitawasimamishia.”+
10 “Na wewe, mutumishi wangu Yakobo, usiogope,” ni vile Yehova anasema,
“Na usiingiwe na woga, Ee Israeli.+
Kwa maana nitakuokoa kutoka mbali
Na uzao wako kutoka katika inchi yao ya utekwa.+
Yakobo atarudia na kuwa na utulivu na bila usumbufu,
Bila mutu wa kuwaogopesha.”+
11 “Kwa maana mimi niko pamoja na wewe,” ni vile Yehova anasema, “ili nikuokoe.
Lakini nitafanya uharibifu mukubwa kati ya mataifa yote kwenye nimekutawanya;+
Hata hivyo, wewe sitakuharibu kabisa.+
12 Kwa maana Yehova anasema hivi:
“Hakuna matunzo kwa ajili ya kuvunjika kwako.+
Kidonda chako hakiwezi kupona.
13 Hakuna mutu wa kukutetea,
Hakuna njia ya kuponyesha kidonda chako.
Hakuna matunzo kwa ajili yako.
14 Wote wenye kukupenda kwa tamaa wamekusahau.+
Hawakutafute tena.
Kwa maana nimekupiga kwa pigo la adui,+
Kwa azabu ya mutu mwenye hana huruma,
Kwa sababu ya hatia yako kubwa na zambi zako nyingi.+
15 Sababu gani unalia kwa sauti kubwa kwa sababu ya kuvunjika kwako?
Maumivu yako hayawezi kupona!
Kwa sababu ya hatia yako kubwa na zambi zako nyingi+
Nimekutendea vile.
16 Kwa hiyo wale wote wenye kukumeza watamezwa,+
Na maadui wako wote watakamatwa pia na kuenda katika utekwa.+
Wale wenye kukuiba wataibwa,
Na nitatoa wale wote wenye kunyanganya vitu vyako ili wanyanganywe vitu vyao.”+
17 “Lakini nitakurudishia afya ya muzuri na nitaponyesha vidonda vyako,”+ ni vile Yehova anasema.
“Hata kama walikuita mwenye kutengwa:
‘Sayuni, mwenye hakuna mutu yeyote mwenye anamutafuta.’”+
18 Yehova anasema hivi:
“Angalia, ninakusanya watu wenye walikamatwa mateka wa mahema ya Yakobo,+
Na nitasikilia tabenakulo zake huruma.
Muji utajengwa upya juu ya kilima chake,+
Na munara wenye ngome utasimama mahali pake penye kufaa.
19 Na kutoka kwao kutakuwa shukrani na sauti za kicheko.+
Nitawafanya waongezeke, na hawatakuwa watu kidogo;+
Nitawafanya kuwa wengi,*
Na hawatakuwa watu bure.+
20 Wana wake watakuwa kama zamani,
Na mukusanyiko wake utafanywa kuwa imara kabisa mbele yangu.+
Nitashugulika na wakandamizaji wake wote.+
21 Mutu wake mwenye cheo atakuwa mumoja wa watu wake,
Na mutawala wake atatoka katikati yake.
Nitamufanya akaribie, na atanikaribia.”
“Kwa maana tofauti na hilo, ni nani anaweza kupima kunikaribia?”* ni vile Yehova anasema.
22 “Na mutakuwa watu wangu,+ na mimi nitakuwa Mungu wenu.”+
23 Angalia! Zoruba yenye upepo mukali ya Yehova italipuka kwa kasirani kali,+
Zoruba kali yenye kufagia yenye kuzunguka-zunguka juu ya kichwa cha waovu.
24 Kasirani yenye kuwaka ya Yehova haitarudia nyuma
Mupaka wakati atakuwa ametenda na kutimiza makusudi ya moyo wake.+
Katika kipindi cha mwisho cha zile siku ninyi mutaelewa jambo hilo.+