Yeremia
41 Katika mwezi wa saba (7) Ishmaeli+ mwana wa Netania mwana wa Elishama, mwenye alikuwa wa ukoo wa kifalme* na mumoja kati ya wakubwa wa mufalme, akakuja pamoja na watu wengine kumi (10) kwa Gedalia mwana wa Ahikamu kule Mispa.+ Wakati walikuwa wanakula chakula pamoja katika Mispa, 2 Ishmaeli mwana wa Netania na wale watu kumi (10) wenye walikuwa pamoja naye wakasimama na kumupiga na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga. Kwa hiyo akamuua mutu mwenye mufalme wa Babiloni alikuwa ameweka juu ya inchi. 3 Ishmaeli akapiga na kuua pia Wayahudi wote wenye walikuwa pamoja na Gedalia katika Mispa, na pia maaskari Wakaldayo wenye walikuwa pale.
4 Katika siku ya pili kisha Gedalia kuuawa, mbele mutu yeyote ajue jambo hilo, 5 watu makumi munane (80) wakakuja kutoka Shekemu,+ kutoka Shilo,+ na kutoka Samaria.+ Ndevu zao zilikuwa zimenyolewa, nguo zao zilikuwa zimepasuliwa, walikuwa wamejikata-kata,+ na walikuwa na matoleo ya nafaka na uvumba+ katika mukono wao ili wavilete kwenye nyumba ya Yehova. 6 Basi Ishmaeli mwana wa Netania akatoka Mispa ili kukutana nao, akilia wakati alikuwa anatembea. Wakati alikutana nao, akawaambia: “Mukuje kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.” 7 Lakini wakati waliingia katika muji, Ishmaeli mwana wa Netania na watu wake wakawaua na kuwatupa ndani ya tangi la maji.
8 Lakini kulikuwa watu kumi (10) kati yao wenye walimuambia Ishmaeli: “Usituue, kwa maana tuko na madepo yenye kufichwa ya ngano, shayiri, mafuta, na asali katika eneo la mashamba.” Basi akajizuia kuwaua pamoja na ndugu zao. 9 Sasa Ishmaeli akatupa ndani ya tangi kubwa la maji mizoga yote ya watu wenye alikuwa ameua, tangi lenye Mufalme Asa alikuwa ametengeneza kwa sababu ya Mufalme Baasha wa Israeli.+ Hilo ndilo tangi la maji lenye Ishmaeli mwana wa Netania alijaza watu wenye waliuawa.
10 Watu wote wenye walibakia katika Mispa,+ Ishmaeli akawakamata mateka, kutia ndani mabinti wa mufalme na watu wote wenye walibakia katika Mispa, wenye Nebuzaradani mukubwa wa walinzi alikuwa ameweka chini ya ulinzi wa Gedalia+ mwana wa Ahikamu. Ishmaeli mwana wa Netania akawakamata mateka na kuvuka kuenda kwa Waamoni.+
11 Wakati Yohanani+ mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye walisikia uovu wote wenye Ishmaeli mwana wa Netania alikuwa ametenda, 12 wakakamata watu wote na kuenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Netania, na wakamupata pembeni ya maji makubwa* katika Gibeoni.
13 Watu wote wenye walikuwa pamoja na Ishmaeli wakafurahi wakati waliona Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye. 14 Kisha watu wote wenye Ishmaeli alikuwa amekamata mateka kule Mispa+ wakageuka na kurudia pamoja na Yohanani mwana wa Karea. 15 Lakini Ishmaeli mwana wa Netania pamoja na watu munane (8) kati ya watu wake wakaponyoka kutoka kwa Yohanani na wakaenda kwa Waamoni.
16 Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye wakakamata pamoja nao watu wenye walibakia kutoka Mispa, wale wenye walikuwa wameokoa kutoka kwa Ishmaeli mwana wa Netania kisha yeye kumupiga na kumuua Gedalia+ mwana wa Ahikamu. Wakarudisha wanaume, maaskari, wanamuke, watoto, na maofisa wa makao ya mufalme kutoka Gibeoni. 17 Basi wakaenda na kukaa mahali pa kukaa pa Kimhamu pembeni ya Betlehemu,+ wakikusudia kuendelea na kuingia Misri+ 18 kwa sababu ya Wakaldayo. Kwa maana walikuwa wamewaogopa, kwa kuwa Ishmaeli mwana wa Netania alikuwa amemupiga na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwenye mufalme wa Babiloni alikuwa ameweka juu ya inchi.+