Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 42
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Yeremia

      • Watu wanamuomba Yeremia asali ili wapate muongozo (1-6)

      • Yehova anajibu: “Musiende Misri” (7-22)

Yeremia 42:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 40:13, 14

Yeremia 42:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:62

Yeremia 42:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 41:16

Yeremia 42:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nitahuzunika.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 32:36; Yer 18:7, 8; Mik 7:18

Yeremia 42:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 41:17, 18

Yeremia 42:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 34:6

Yeremia 42:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 43:4, 7

Yeremia 42:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kukaa kwa wakati fulani.”

Yeremia 42:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:45; Yer 44:12-14, 27, 28

Yeremia 42:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:8-10; 2Nya 34:24, 25; 36:16, 17; Omb 2:4
  • +Yer 29:18

Yeremia 42:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi zenu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 42:1, 2

Yeremia 42:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 24:19; Ne 9:26; Zek 7:11

Yeremia 42:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 43:10, 11

Maandiko ingine

Yer. 42:1Yer 40:13, 14
Yer. 42:2Kum 28:62
Yer. 42:8Yer 41:16
Yer. 42:10Kum 32:36; Yer 18:7, 8; Mik 7:18
Yer. 42:11Yer 41:17, 18
Yer. 42:12Kut 34:6
Yer. 42:14Yer 43:4, 7
Yer. 42:16Kum 28:45; Yer 44:12-14, 27, 28
Yer. 42:182 Fal. 25:8-10; 2Nya 34:24, 25; 36:16, 17; Omb 2:4
Yer. 42:18Yer 29:18
Yer. 42:20Yer 42:1, 2
Yer. 42:212Nya 24:19; Ne 9:26; Zek 7:11
Yer. 42:22Yer 43:10, 11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia 42:1-22

Yeremia

42 Kisha wakubwa wote wa jeshi, na Yohanani+ mwana wa Karea, Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, wakakaribia 2 na kumuambia Yeremia nabii: “Tafazali, sikia ombi letu la kuomba rehema, na usali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wako, kwa ajili ya mabaki hawa wote, kwa maana kati ya watu wengi ni watu kidogo tu ndio walibakia,+ kama vile unaona. 3 Yehova Mungu wako atuambie njia yenye tunapaswa kutembea ndani na kile tunapaswa kufanya.”

4 Yeremia nabii akawajibu: “Nimewasikia, na ninasali kwa Yehova Mungu wenu kulingana na ombi lenu; na kila neno lenye Yehova anawajibu, nitawaambia. Sitawaficha neno lolote.”

5 Wakamujibu Yeremia: “Yehova akuwe shahidi wa kweli na muaminifu juu yetu ikiwa hatufanye sawasawa kama vile Yehova Mungu wako anatuagiza kupitia wewe. 6 Likuwe jambo la muzuri ao la mubaya, tutatii sauti ya Yehova Mungu wetu, mwenye tunakutuma kwake, ili mambo yakuwe muzuri kwetu kwa sababu tunatii sauti ya Yehova Mungu wetu.”

7 Sasa kisha siku kumi (10) neno la Yehova likakuja kwa Yeremia. 8 Basi akamuita Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye na watu wote, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi.+ 9 Akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli, mwenye mulinituma kwake ili kutoa ombi lenu la kuomba rehema mbele yake, anasema hivi: 10 ‘Kwa kweli kama mutabakia katika inchi hii, basi nitawajenga ninyi na sitawabomoa, na nitawapanda na sitawangoa, kwa maana nitasikitika* juu ya musiba wenye nimewaletea.+ 11 Musiogope kwa sababu ya mufalme wa Babiloni, mwenye munaogopa.’+

“‘Musiogope kwa sababu yake,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana niko pamoja na ninyi, ili kuwaokoa ninyi na kuwakomboa kutoka katika mukono wake. 12 Na nitawaonyesha ninyi rehema,+ na atawaonyesha ninyi rehema na kuwarudisha kwenye inchi yenu wenyewe.

13 “‘Lakini kama munasema, “Hapana, hatutabakia katika inchi hii!” na munakosa kutii sauti ya Yehova Mungu wenu 14 kwa kusema: “Hapana, tofauti na hilo tutaenda katika inchi ya Misri,+ kwenye hatutaona vita wala kusikia sauti ya baragumu wala kuwa na njaa kwa kukosa mukate; ni kule tutaishi,” 15 basi musikie neno la Yehova, Enyi mabaki ya Yuda. Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kama mumeazimia kabisa kuenda Misri na munaenda kukaa* kule, 16 basi upanga uleule wenye munaogopa utawafikia kule katika inchi ya Misri, na njaa ileile yenye munaogopa itawafuata kule Misri, na mutakufia kule.+ 17 Na watu wote wenye wameazimia kuenda Misri ili kukaa kule watakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza. Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye ataokoka wala kuponyoka musiba wenye nitaleta juu yao.”’

18 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kama vile hasira yangu na kasirani yangu kali vilimwangwa juu ya wakaaji wa Yerusalemu,+ ni vile kasirani yangu kali itamwangwa juu yenu kama munaenda Misri, na mutakuwa laana, kitu cha kuogopesha, tukano, na haya,+ na hamutaona mahali hapa tena hata siku moja.’

19 “Yehova amesema juu yenu, Enyi mabaki ya Yuda. Musiende Misri. Munapaswa kujua hakika kwamba nimewaonya leo 20 kwamba kosa lenu litafanya mulipe uzima wenu.* Kwa maana mulinituma kwa Yehova Mungu wenu, mukisema, ‘Sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu, na utuambie kila jambo lenye Yehova Mungu wetu anasema, na sisi tutalifanya.’+ 21 Na nimewaambia ninyi leo, lakini hamutatii sauti ya Yehova Mungu wenu ao kufanya jambo lolote lenye alinituma niwaambie ninyi.+ 22 Kwa hiyo, mujue hakika kwamba mutakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza katika mahali kwenye munatamani kuenda na kukaa.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine