Yeremia
42 Kisha wakubwa wote wa jeshi, na Yohanani+ mwana wa Karea, Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, wakakaribia 2 na kumuambia Yeremia nabii: “Tafazali, sikia ombi letu la kuomba rehema, na usali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wako, kwa ajili ya mabaki hawa wote, kwa maana kati ya watu wengi ni watu kidogo tu ndio walibakia,+ kama vile unaona. 3 Yehova Mungu wako atuambie njia yenye tunapaswa kutembea ndani na kile tunapaswa kufanya.”
4 Yeremia nabii akawajibu: “Nimewasikia, na ninasali kwa Yehova Mungu wenu kulingana na ombi lenu; na kila neno lenye Yehova anawajibu, nitawaambia. Sitawaficha neno lolote.”
5 Wakamujibu Yeremia: “Yehova akuwe shahidi wa kweli na muaminifu juu yetu ikiwa hatufanye sawasawa kama vile Yehova Mungu wako anatuagiza kupitia wewe. 6 Likuwe jambo la muzuri ao la mubaya, tutatii sauti ya Yehova Mungu wetu, mwenye tunakutuma kwake, ili mambo yakuwe muzuri kwetu kwa sababu tunatii sauti ya Yehova Mungu wetu.”
7 Sasa kisha siku kumi (10) neno la Yehova likakuja kwa Yeremia. 8 Basi akamuita Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye na watu wote, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi.+ 9 Akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli, mwenye mulinituma kwake ili kutoa ombi lenu la kuomba rehema mbele yake, anasema hivi: 10 ‘Kwa kweli kama mutabakia katika inchi hii, basi nitawajenga ninyi na sitawabomoa, na nitawapanda na sitawangoa, kwa maana nitasikitika* juu ya musiba wenye nimewaletea.+ 11 Musiogope kwa sababu ya mufalme wa Babiloni, mwenye munaogopa.’+
“‘Musiogope kwa sababu yake,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana niko pamoja na ninyi, ili kuwaokoa ninyi na kuwakomboa kutoka katika mukono wake. 12 Na nitawaonyesha ninyi rehema,+ na atawaonyesha ninyi rehema na kuwarudisha kwenye inchi yenu wenyewe.
13 “‘Lakini kama munasema, “Hapana, hatutabakia katika inchi hii!” na munakosa kutii sauti ya Yehova Mungu wenu 14 kwa kusema: “Hapana, tofauti na hilo tutaenda katika inchi ya Misri,+ kwenye hatutaona vita wala kusikia sauti ya baragumu wala kuwa na njaa kwa kukosa mukate; ni kule tutaishi,” 15 basi musikie neno la Yehova, Enyi mabaki ya Yuda. Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kama mumeazimia kabisa kuenda Misri na munaenda kukaa* kule, 16 basi upanga uleule wenye munaogopa utawafikia kule katika inchi ya Misri, na njaa ileile yenye munaogopa itawafuata kule Misri, na mutakufia kule.+ 17 Na watu wote wenye wameazimia kuenda Misri ili kukaa kule watakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza. Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye ataokoka wala kuponyoka musiba wenye nitaleta juu yao.”’
18 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kama vile hasira yangu na kasirani yangu kali vilimwangwa juu ya wakaaji wa Yerusalemu,+ ni vile kasirani yangu kali itamwangwa juu yenu kama munaenda Misri, na mutakuwa laana, kitu cha kuogopesha, tukano, na haya,+ na hamutaona mahali hapa tena hata siku moja.’
19 “Yehova amesema juu yenu, Enyi mabaki ya Yuda. Musiende Misri. Munapaswa kujua hakika kwamba nimewaonya leo 20 kwamba kosa lenu litafanya mulipe uzima wenu.* Kwa maana mulinituma kwa Yehova Mungu wenu, mukisema, ‘Sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu, na utuambie kila jambo lenye Yehova Mungu wetu anasema, na sisi tutalifanya.’+ 21 Na nimewaambia ninyi leo, lakini hamutatii sauti ya Yehova Mungu wenu ao kufanya jambo lolote lenye alinituma niwaambie ninyi.+ 22 Kwa hiyo, mujue hakika kwamba mutakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza katika mahali kwenye munatamani kuenda na kukaa.”+