Yeremia
1 Haya ndiyo maneno ya Yeremia* mwana wa Hilkia, mumoja wa makuhani katika Anatoti+ katika inchi ya Benyamini. 2 Neno la Yehova likakuja kwake katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni,+ mufalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu (13) wa utawala wake. 3 Likakuja pia katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, mupaka kumalizika kwa mwaka wa kumi na moja (11) wa Sedekia+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, mupaka wakati Yerusalemu ilienda katika uhamisho katika mwezi wa tano (5).+
4 Neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema:
Nilikufanya kuwa nabii kwa mataifa.”
6 Lakini nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova!
Mimi sijue namna ya kusema,+ kwa maana niko kijana mudogo tu.”+
7 Kisha Yehova akaniambia:
“Usiseme, ‘Niko kijana mudogo tu.’
Kwa maana unapaswa kuenda kwa wote wenye ninakutuma kwao,
Na unapaswa kusema kila jambo lenye ninakuamuru.+
8 Usiogope kwa sababu ya namna wanaonekana,+
Kwa maana ‘mimi niko pamoja na wewe ili kukuokoa,’+ ni vile Yehova anasema.”
9 Kisha Yehova akanyoosha mukono wake na kugusa kinywa changu.+ Na Yehova akaniambia: “Nimetia maneno yangu katika kinywa chako.+ 10 Angalia, nimekupatia daraka leo hii ili ukuwe juu ya mataifa na juu ya falme, ili kungoa na kubomoa, ili kuharibu na kuangusha, ili kujenga na kupanda.”+
11 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Ninaona tawi la muti wa lozi.”*
12 Yehova akaniambia: “Umeona muzuri, kwa maana niko macho kabisa juu ya neno langu ili kulitimiza.”
13 Neno la Yehova likakuja kwangu mara ya pili, likisema: “Unaona nini?” Basi nikasema: “Ninaona chungu* chenye kutokota,* na mudomo wake umeinama kutoka kaskazini.” 14 Kisha Yehova akaniambia:
“Musiba utafunguliwa kutoka kaskazini
Juu ya wakaaji wote wa inchi.+
15 Kwa maana ‘ninaita familia zote za falme za kaskazini,’ ni vile Yehova anasema,+
‘Na watakuja; kila mumoja ataweka kiti chake cha ufalme
Kwenye muingilio wa milango mikubwa ya Yerusalemu,+
Kwenye kuta zake kuzunguka pande zote
Na kwenye miji yote ya Yuda.+
16 Na nitatangaza hukumu zangu juu yao kwa sababu ya uovu wao wote,
Kwa sababu wameniacha,+
Na wanachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya miungu mingine+
Na kuinamia kazi za mikono yao wenyewe.’+
17 Lakini unapaswa kujitayarisha ili kutenda,*
Na unapaswa kusimama na kuwaambia kila jambo lenye ninakuamuru.
Usiwaogope,+
Ili nisikuogopeshe mbele yao.