Danieli
1 Katika mwaka wa tatu (3) wa ufalme wa Mufalme Yehoyakimu+ wa Yuda, Mufalme Nebukadneza wa Babiloni alikuja Yerusalemu na kuizunguka kwa ajili ya vita.+ 2 Kisha wakati fulani Yehova akamutia Yehoyakimu Mufalme wa Yuda katika mukono wa Nebukadneza,+ pamoja na sehemu fulani ya vyombo vya nyumba ya * Mungu wa kweli, na akavileta katika inchi ya Shinari*+ katika nyumba ya * mungu wake. Akaweka vyombo hivyo katika hazina ya mungu wake.+
3 Kisha Mufalme akamuamuru Ashpenazi ofisa wa makao yake ya kifalme alete wamoja kati ya Waisraeli, * kutia ndani wenye kutoka katika uzao wa kifalme na uzao wa watu wenye vyeo.+ 4 Walipaswa kuwa vijana * wenye hawana kasoro yoyote, wenye sura ya muzuri, wenye hekima, ujuzi, na utambuzi,+ na wenye uwezo wa kutumika katika nyumba ya mufalme. Alipaswa kuwafundisha maandishi na luga ya Wakaldayo. 5 Zaidi ya hayo, mufalme aliwawekea posho ya kila siku kutoka kwenye vyakula vitamu vya mufalme na kutoka kwenye divai yenye alikuwa anakunywa. Walipaswa kuzoezwa* kwa miaka tatu (3), na kwenye mwisho wa kipindi hicho wangeanza kumutumikia mufalme.
6 Sasa kati yao kulikuwa wamoja kutoka kabila la Yuda:* Danieli,*+ Hanania,* Mishaeli,* na Azaria.*+ 7 Na ofisa mukubwa wa makao ya mufalme akawapatia majina;* akamupatia Danieli jina Belteshaza,+ akamupatia Hanania jina Shadraki, akamupatia Mishaeli jina Meshaki, na akamupatia Azaria jina Abednego.+
8 Lakini Danieli aliazimia katika moyo wake kwamba hatajichafua na vyakula vitamu vya mufalme ao na divai yenye alikuwa anakunywa. Basi alimuomba ule ofisa mukubwa wa makao ya mufalme amuruhusu asijichafue kwa njia hiyo. 9 Na Mungu wa kweli akafanya ofisa mukubwa wa makao ya mufalme amuonyeshe Danieli wema* na rehema.+ 10 Lakini ule ofisa mukubwa wa makao ya mufalme akamuambia Danieli: “Ninamuogopa bwana wangu mufalme, mwenye ameweka chakula chenu na kinywaji. Itakuwa namna gani kama anaona sura zenu zimeharibika kuliko za vijana* wengine wa miaka yenu? Mutafanya nikuwe na hatia* mbele ya mufalme.” 11 Lakini Danieli akamuambia mulinzi mwenye ofisa mukubwa wa makao ya mufalme aliweka juu ya Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria: 12 “Tafazali, jaribu watumishi wako kwa siku kumi (10), na tupewe mboga za majani tukule na maji ya kunywa; 13 kisha ulinganishe sura zetu na sura za vijana* wenye wanakula vyakula vitamu vya mufalme, na utendee watumishi wako kulingana na vile unaona.”
14 Basi akakubali pendekezo lao na akawajaribu kwa siku kumi (10). 15 Kwenye mwisho wa siku kumi (10), sura zao zilikuwa za muzuri na walionekana wenye afya ya muzuri* zaidi kuliko vijana* wengine wote wenye walikuwa wanakula vyakula vitamu vya mufalme. 16 Kwa hiyo mulinzi alikuwa anatosha vyakula vyao vitamu na divai yao na kuwapatia mboga za majani. 17 Na Mungu wa kweli akapatia wale vijana* ine (4) ujuzi na ufahamu katika kila namna ya maandishi na hekima; na Danieli akapewa uelewaji katika kila namna ya maono na ndoto.+
18 Kwenye mwisho wa wakati wenye mufalme alikuwa amesema ili waletwe ndani,+ ule ofisa mukubwa wa makao ya mufalme akawaleta mbele ya Nebukadneza. 19 Wakati mufalme alisema nao, hakuna hata mumoja katika kikundi chote mwenye alipatikana kuwa kama Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria;+ na wakaendelea kutumika mbele ya mufalme. 20 Katika kila jambo lenye kuomba hekima na uelewaji lenye mufalme aliwauliza, aliwaona kuwa wazuri mara kumi (10) zaidi kuliko makuhani wote wenye kufanya uchawi na watu wote wenye kuitia roho wachafu+ katika ufalme wake wote. 21 Na Danieli akaendelea kukaa kule mupaka mwaka wa kwanza wa Mufalme Koreshi.+