Danieli
3 Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu yenye urefu wa mikono makumi sita (60)* na upana wa mikono sita (6).* Aliisimamisha kwenye eneo tambarare la Dura katika jimbo la* Babiloni. 2 Kisha Mufalme Nebukadneza akatuma ujumbe ili kukusanya maliwali, wasaidizi wa maliwali, magavana, washauri, waweka-hazina, waamuzi, waamuzi wa raia, na wasimamizi wote wa majimbo* wakuje kwenye muzinduo wa sanamu yenye Mufalme Nebukadneza alikuwa amesimamisha.
3 Basi maliwali, wasaidizi wa maliwali, magavana, washauri, waweka-hazina, waamuzi, waamuzi wa raia, na wakubwa wote wa majimbo* wakakusanyika kwa ajili ya kuzindua sanamu yenye Mufalme Nebukadneza alikuwa amesimamisha. Na wakasimama mbele ya sanamu yenye Nebukadneza alikuwa amesimamisha. 4 Mutangazaji akatangaza hivi kwa sauti kubwa: “Munaamuriwa, Enyi vikundi vya watu, mataifa, na vikundi vya luga, 5 kwamba wakati mutasikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu (3), chombo cha kamba, zumari-tete, na vyombo vingine vyote vya muziki, munapaswa kuanguka chini na kuabudu sanamu ya zahabu yenye Mufalme Nebukadneza amesimamisha. 6 Mutu yeyote mwenye hataanguka chini na kuabudu atatupwa mara moja ndani ya tanuru yenye kuwaka moto.”+ 7 Basi wakati vikundi vyote vya watu vilisikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu (3), chombo cha kamba, na vyombo vingine vyote vya muziki, vikundi vyote vya watu, mataifa, na vikundi vya luga vikaanguka chini na kuabudu sanamu ya zahabu yenye Mufalme Nebukadneza alikuwa amesimamisha.
8 Sasa wakati huo Wakaldayo fulani wakakuja na kushitaki* Wayahudi. 9 Wakamuambia Mufalme Nebukadneza: “Ee mufalme, uishi milele. 10 Wewe, Ee mufalme, ulitoa amri kwamba kila mutu mwenye anasikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu (3), chombo cha kamba, zumari-tete, na vyombo vingine vyote vya muziki, anapaswa kuanguka chini na kuabudu ile sanamu ya zahabu; 11 na kwamba mutu yeyote mwenye hataanguka chini na kuabudu anapaswa kutupwa ndani ya tanuru yenye kuwaka moto.+ 12 Lakini kuko Wayahudi fulani wenye uliweka wasimamie jimbo la* Babiloni: Shadraki, Meshaki, na Abednego.+ Wanaume hawa hawakukuheshimia, Ee mufalme. Hawatumikie miungu yako, na wanakataa kuabudu sanamu ya zahabu yenye ulisimamisha.”
13 Kisha Nebukadneza, akiwa amekasirika sana, akaamuru Shadraki, Meshaki, na Abednego waletwe. Basi wanaume hao wakaletwa mbele ya mufalme. 14 Nebukadneza akawaambia: “Je, ni kweli kabisa, Shadraki, Meshaki, na Abednego, kwamba hamutumikie miungu yangu+ na kwamba munakataa kuabudu sanamu ya zahabu yenye nimesimamisha? 15 Sasa wakati mutasikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu (3), chombo cha kamba, zumari-tete, na vyombo vingine vyote vya muziki, kama muko tayari kuanguka chini na kuabudu sanamu yenye nimetengeneza, ni muzuri. Lakini kama munakataa kuabudu, mutatupwa mara moja ndani ya tanuru yenye kuwaka moto. Na ni mungu gani mwenye anaweza kuwaokoa kutoka katika mikono yangu?”+
16 Shadraki, Meshaki, na Abednego wakamujibu mufalme: “Ee Nebukadneza, hatuna lazima ya kukujibu juu ya jambo hili. 17 Kama inapaswa kuwa vile, Mungu wetu mwenye tunatumikia anaweza kutuokoa kutoka ndani ya tanuru hiyo yenye kuwaka moto, Ee mufalme, na kutuokoa kutoka katika mukono wako.+ 18 Lakini hata kama hafanye vile, ujue, Ee mufalme, kama hatutatumikia miungu yako wala kuabudu sanamu ya zahabu yenye ulisimamisha.”+
19 Kisha Nebukadneza akamukasirikia sana Shadraki, Meshaki, na Abednego, na uso wake ukabadilika,* na akatoa amri kwamba tanuru iwashwe moto mara saba (7) kuliko kawaida yake. 20 Akaamuru wanaume fulani wenye nguvu katika jeshi lake wawafunge Shadraki, Meshaki, na Abednego na kuwatupa katika tanuru yenye kuwaka moto.
21 Basi wanaume hao wakafungwa wakiwa bado wenye kuvaa nguo za inje, nguo, kofia, na nguo zao zingine zote, na wakatupwa ndani ya tanuru yenye kuwaka moto. 22 Kwa sababu amri ya mufalme ilikuwa kali sana na tanuru ilikuwa moto kuliko kawaida, wale wanaume wenye waliwakamata Shadraki, Meshaki, na Abednego ndio wenye waliuawa na miali ya moto. 23 Lakini wanaume hao watatu (3), Shadraki, Meshaki, na Abednego, wakaanguka ndani ya ile tanuru yenye kuwaka moto wakiwa wamefungwa.
24 Kisha Mufalme Nebukadneza akaogopa na akasimama mbio na kuuliza maofisa wake wakubwa: “Je, hatukufunga wanaume watatu (3) na kuwatupa ndani ya moto?” Wakamujibu mufalme: “Ndiyo, Ee mufalme.” 25 Akasema: “Angalia! Ninaona wanaume ine (4) wakitembea-tembea wakiwa huru katikati ya moto, na hawaumie, na ule wa ine anafanana na mwana wa miungu.”
26 Nebukadneza akakaribia mulango wa ile tanuru yenye kuwaka moto na kusema: “Shadraki, Meshaki, na Abednego, ninyi watumishi wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,+ mutoke inje na mukuje hapa!” Shadraki, Meshaki, na Abednego wakatoka katikati ya ule moto. 27 Na maliwali, wasaidizi wa maliwali, magavana, na maofisa wakubwa wa mufalme wenye walikuwa wamekusanyika pale+ wakaona kwamba moto haukufanya kitu* kwenye miili ya wanaume hao;+ hakuna hata unywele mumoja wa vichwa vyao wenye uliungua, nguo zao za inje hazikuonekana tofauti, na hawakukuwa hata na harufu ya moto.
28 Kisha Nebukadneza akasema: “Asifiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki, na Abednego,+ mwenye alituma malaika wake na kuokoa watumishi wake. Walimutegemea na wakatenda kinyume na amri ya mufalme na walikuwa tayari kufa* kuliko kumutumikia na kumuabudu mungu yeyote isipokuwa tu Mungu wao.+ 29 Kwa hiyo ninatoa amri kwamba kikundi chochote cha watu, taifa, ao kikundi cha luga chenye kitasema jambo lolote la mubaya juu ya Mungu wa Shadraki, Meshaki, na Abednego, kinapaswa kukatwa vipande-vipande, na nyumba zao zinapaswa kugeuzwa kuwa vyoo vya watu wote;* kwa maana hakuna mungu mwingine yeyote mwenye anaweza kuokoa kama huyu.”+
30 Kisha mufalme akapandisha cheo Shadraki, Meshaki, na Abednego* katika jimbo la* Babiloni.+