Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Danieli 11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Danieli

      • Wafalme wa Uajemi na Ugiriki (1-4)

      • Wafalme wa kusini na kaskazini (5-45)

        • Kutokea kwa mulipishaji (20)

        • Kiongozi wa agano atavunjwa (22)

        • Kutukuzwa kwa mungu wa ngome (38)

        • Mufalme wa kusini na mufalme wa kaskazini wanasukumana (40)

        • Habari zenye kusumbua kutoka mashariki na kaskazini (44)

Danieli 11:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “na kama ngome kwake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 5:30, 31; 9:1

Danieli 11:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “watainuka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 8:21

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Utumishi na Maisha ya Mukristo—Buku la Mukutano,

    10/2017, uku. 4

Danieli 11:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 8:5, 21

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Utumishi na Maisha ya Mukristo—Buku la Mukutano,

    10/2017, uku. 4

Danieli 11:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 7:6; 8:8, 22

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Utumishi na Maisha ya Mukristo—Buku la Mukutano,

    10/2017, uku. 4

Danieli 11:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “makubaliano yenye.”

Danieli 11:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “sanamu zao za kuyeyushwa.”

  • *

    Ao “vyenye samani.”

Danieli 11:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wana wa wanyanganyi.”

Danieli 11:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “majeshi.”

Danieli 11:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ule Uzuri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 48:2; Da. 8:9; 11:41, 45

Danieli 11:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ataazimia.”

Danieli 11:20

Maelezo ya Chini

  • *

    “Mulipishaji,” pengine wa kodi; Ao “musimamizi wa kazi.”

Danieli 11:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “bila kuonya.”

Danieli 11:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “majeshi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 9:25; Yoh 1:45, 49
  • +Mwa 15:18; Mdo 3:25

Danieli 11:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “Bila kuonya.”

  • *

    Tnn., “unono wa.”

  • *

    Ao “wilaya ya utawala.”

Danieli 11:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “litaharibiwa kupitia mafuriko.”

Danieli 11:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 12:9

Danieli 11:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua za maji; bateaux.”

  • *

    Ao “ataongoza kasirani yake kali.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 10:4; Hes 24:24; Isa 23:1; Yer 2:10; Eze 27:6
  • +Da. 11:28

Danieli 11:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “majeshi yatasimama.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 8:11
  • +Da. 8:12
  • +Da. 12:11; Mt 24:15; Mk 13:14; Lu 21:20

Danieli 11:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ya kusifu-sifu; ya kukosa unyoofu.”

Danieli 11:33

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 12:10

Danieli 11:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ya kusifu-sifu; ya kukosa unyoofu.”

Danieli 11:35

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 12:10

Danieli 11:36

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 10:17; Zab 136:1, 2

Danieli 11:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “pa nafasi yake.”

  • *

    Ao “vyenye samani.”

Danieli 11:39

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “akisaidiwa.”

  • *

    Ao pengine, “yeyote mwenye yeye anamutambua.”

Danieli 11:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “atapigana mapembe naye.”

  • *

    Ao “mashua za maji; bateaux.”

Danieli 11:41

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ule Uzuri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 48:2; Da. 8:9; 11:16, 45

Danieli 11:43

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “vyenye samani.”

  • *

    Ao “watamufuata.”

Danieli 11:44

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mahali jua linatokea.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/5/2015, uku. 29-30

Danieli 11:45

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ule Uzuri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 48:2; Da. 8:9; 11:16, 41

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/5/2015, uku. 29-30

Maandiko ingine

Dan. 11:1Da. 5:30, 31; 9:1
Dan. 11:2Da. 8:21
Dan. 11:3Da. 8:5, 21
Dan. 11:4Da. 7:6; 8:8, 22
Dan. 11:16Zab 48:2; Da. 8:9; 11:41, 45
Dan. 11:22Da. 9:25; Yoh 1:45, 49
Dan. 11:22Mwa 15:18; Mdo 3:25
Dan. 11:27Da. 12:9
Dan. 11:30Mwa 10:4; Hes 24:24; Isa 23:1; Yer 2:10; Eze 27:6
Dan. 11:30Da. 11:28
Dan. 11:31Da. 8:11
Dan. 11:31Da. 8:12
Dan. 11:31Da. 12:11; Mt 24:15; Mk 13:14; Lu 21:20
Dan. 11:33Da. 12:10
Dan. 11:35Da. 12:10
Dan. 11:36Kum 10:17; Zab 136:1, 2
Dan. 11:41Zab 48:2; Da. 8:9; 11:16, 45
Dan. 11:45Zab 48:2; Da. 8:9; 11:16, 41
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • 45
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Danieli 11:1-45

Danieli

11 “Lakini mimi, katika mwaka wa kwanza wa Dario+ Mumedi, nilisimama ili kumutia nguvu na kumuimarisha.* 2 Mambo yenye nitakuambia sasa ni kweli:

“Angalia! Wafalme wengine watatu (3) watasimama* kwa ajili ya Uajemi, na wa ine (4) atajikusanyia utajiri mwingi kuliko wale wengine wote. Na wakati atakuwa na nguvu kupitia utajiri wake, ataamusha kila kitu ili kupinga ufalme wa Ugiriki.+

3 “Na mufalme mwenye nguvu atasimama na atatawala kwa mamlaka makubwa+ na atafanya vile anapenda. 4 Lakini wakati atakuwa amesimama, ufalme wake utavunjwa na kugawanywa kuelekea pepo ine (4) za mbingu,+ lakini hapana kwa wazao wake na hapana kama mamlaka yenye alitawala nayo; kwa maana ufalme wake utangolewa na kuenda kwa watu wengine tofauti na hawa.

5 “Na mufalme wa kusini atakuwa na nguvu, ni kusema, mumoja wa wakubwa wake; lakini kuko mumoja mwenye atamushinda na kutawala akiwa na mamlaka makubwa, makubwa kuliko mamlaka ya kutawala ya ule mwingine.

6 “Kisha miaka fulani watafanya agano, na binti ya mufalme wa kusini atakuja kwa mufalme wa kaskazini ili kufanya mupango wenye* usawa. Lakini binti huyo hatabakia na nguvu za mukono wake; na ule mufalme hatasimama, wala mukono wake; na binti huyo atatolewa, yeye pamoja na wale wenye kumuleta ndani, na ule mwenye alimuzaa, na ule mwenye alikuwa anamutia nguvu katika nyakati hizo. 7 Na mutu fulani kutoka chipukizi la mizizi yake atasimama mahali pa mufalme, na atakuja ili kupigana na jeshi na atakuja ili kushambulia ngome ya mufalme wa kaskazini na atachukua hatua ili kupigana nao na kuwashinda. 8 Tena, pamoja na miungu yao, pamoja na sanamu zao za metali,* pamoja na vyombo vyao vyenye kutamanika* vya feza na vya zahabu, na pamoja na watu wenye walikamatwa mateka, atakuja Misri. Kwa miaka fulani atasimama mbali na mufalme wa kaskazini, 9 mwenye atakuja ili kushambulia ufalme wa mufalme wa kusini, lakini atarudia katika inchi yake mwenyewe.

10 “Lakini wana wake, watajitayarisha kwa ajili ya vita na watakusanya jeshi kubwa sana. Kwa kweli, atakuja na kufagia kama mafuriko. Lakini atarudia, na atapigana vita mupaka kwenye ngome yake.

11 “Na mufalme wa kusini atakuwa na uchungu na atatoka na kupigana naye, ni kusema, na mufalme wa kaskazini; na atakusanya watu wengi sana, lakini watu hao wengi watatiwa katika mukono wa huyo. 12 Na watu hao wengi watachukuliwa. Moyo wake utajitukuza, na atafanya makumi ya maelfu waanguke; lakini hatatumia nafasi yake yenye nguvu.

13 “Na mufalme wa kaskazini atarudia na kukusanya watu wengi sana kuliko wale wa kwanza; na kwenye mwisho wa nyakati, kisha miaka fulani, kwa kweli atakuja akiwa na jeshi kubwa na mali nyingi. 14 Katika nyakati hizo watu wengi watasimama ili kupinga mufalme wa kusini.

“Na watu wenye jeuri* kati ya watu wako watapelekwa ili wajaribu kutimiza maono; lakini watajikwaa.

15 “Na mufalme wa kaskazini atakuja na kujenga boma la kuzunguka kwa ajili ya vita na kukamata muji wenye ngome. Na mikono* ya kusini haitasimama, wala watu wake wenye walichaguliwa; na hawatakuwa na nguvu ya kusimama. 16 Ule mwenye anakuja ili kupingana naye atafanya vile anapenda, na hakuna mwenye atasimama mbele yake. Atasimama katika inchi ya lile Pambo,*+ na uwezo wa kuharibu utakuwa katika mukono wake. 17 Na atakaza uso wake ili* kuja na nguvu zote za ufalme wake, na kutakuwa mapatano pamoja naye; na atatenda kwa njia yenye matokeo. Kuhusu binti ya wanamuke, huyo atapewa uwezo wa kumuharibu. Na binti huyo hatasimama, na hataendelea kuwa wake. 18 Atageuza uso wake nyuma kuelekea kwenye inchi za pembeni ya bahari na atakamata watu wengi mateka. Na kiongozi wa jeshi atafanya lawama kutoka kwake iishe kwa ajili yake mwenyewe, ili lawama yake isikuwe. Atafanya hiyo irudie kwa ule mwingine. 19 Kisha atageuza uso wake nyuma kwenye ngome za inchi yake mwenyewe, na atajikwaa na kuanguka, na hatapatikana.

20 “Na katika cheo chake mutu fulani atasimama mwenye anafanya mulipishaji* apite katika ufalme wenye kupendeza, lakini katika siku kidogo atavunjwa, hata hivyo, hapana katika kasirani wala katika vita.

21 “Na katika cheo chake mutu fulani mwenye kuzarauliwa atasimama, na hawatamupatia heshima ya ufalme; na ataingia wakati wa usalama* na kuchukua ufalme kwa ujanja. 22 Na mikono* ya mafuriko itaharibiwa kwa sababu yake, na itavunjwa; kama vile itakuwa kwa Kiongozi+ wa agano.+ 23 Na kwa sababu ya agano lao pamoja naye, ataendeleza udanganyifu na atasimama na kuwa na nguvu kupitia taifa la kidogo. 24 Wakati wa usalama,* ataingia katika maeneo yenye utajiri zaidi ya* jimbo* na kufanya mambo yenye baba zake na baba za baba zake hawakufanya. Atawagawia vitu vyenye vinanyanganywa katika vita na vitu vyenye vinachukuliwa katika vita, na mali; na atafanya mipango yake ya mubaya ili kupindua mahali kwenye ngome, lakini kwa wakati kidogo tu.

25 “Na atakusanya nguvu zake na moyo wake ili kupingana na mufalme wa kusini akiwa na jeshi kubwa, na mufalme wa kusini atajitayarisha kwa ajili ya vita akiwa na jeshi kubwa sana na lenye nguvu. Na hatasimama, kwa sababu watafanya mipango mibaya juu yake. 26 Na wale wenye wanakula vyakula vyake vitamu watatokeza kuanguka kwake.

“Lakini jeshi lake, litaharibiwa,* na wengi watauawa.

27 “Kuhusu wafalme hao wawili, moyo wao utakuwa na muelekeo wa kufanya mambo ya mubaya, na watakaa kwenye meza moja wakiambiana uongo. Lakini hakuna kitu chenye kitafanikiwa, kwa sababu bado mwisho ni kwa ajili ya wakati wenye uliwekwa.+

28 “Na atarudia katika inchi yake akiwa na mali nyingi, na moyo wake utapinga agano takatifu. Atatenda kwa njia yenye matokeo na kurudia katika inchi yake.

29 “Na kwa wakati wenye uliwekwa atarudia na kuja ili kupigana na kusini. Lakini wakati huo hautakuwa kama vile ilikuwa pale mwanzo, 30 kwa maana mashua* za Kitimu+ zitakuja kumushambulia, na atanyenyekezwa.

“Atarudia na kumwanga lawama* juu ya agano takatifu+ na kutenda kwa njia yenye matokeo; na atarudia na kukaza uangalifu juu ya wale wenye kuacha agano takatifu. 31 Na mikono itasimama,* kutoka kwake; na kuchafua patakatifu,+ ile ngome, na kuondoa zabihu ya kuendelea.+

“Na watasimamisha lile chukizo lenye linaleta uharibifu.+

32 “Na wale wenye wanatenda kwa uovu ili kupinga agano, atawaongoza katika uasi-imani kupitia maneno laini.* Lakini watu wenye wanamujua Mungu wao watashinda na kutenda kwa njia yenye matokeo. 33 Na wale wenye kuwa na ufahamu+ kati ya watu watapatia watu wengi uelewaji. Na watakwazwa kwa upanga na kwa mwali wa moto, kwa kutekwa na kwa kunyanganywa, kwa siku fulani. 34 Lakini wakati watakuwa wamekwazwa, watapewa musaada kidogo; na wengi watajiunga nao kupitia maneno laini.* 35 Na wamoja kati ya wale wenye ufahamu watakwazwa, ili kufanya kazi ya kusafisha kwa sababu yao na kutakasa na kufanya kuwa weupe+ mupaka wakati wa mwisho; kwa sababu bado ni kwa ajili ya wakati wenye uliwekwa.

36 “Mufalme atafanya vile anapenda, na atajiinua na kujitukuza juu ya kila mungu; na atasema mambo ya kushangaza ili kumupinga Mungu wa miungu.+ Na atapata matokeo ya muzuri mupaka wakati kasirani kali itafikia mwisho; kwa sababu kile kilikusudiwa lazima kitokee. 37 Hatamuheshimia Mungu wa baba zake; na hataonyesha heshima kwa tamaa ya wanamuke wala kwa mungu mwingine yeyote, lakini atajitukuza mwenyewe juu ya kila mutu. 38 Lakini tofauti na hilo* atamutukuza mungu wa ngome; atamutukuza mungu mwenye baba zake hawakujua kupitia zahabu na feza na majiwe yenye samani na vitu vyenye kutamanika.* 39 Atatenda kwa njia yenye matokeo juu ya ngome zenye kuwa nguvu, pamoja* na mungu wa kigeni. Atapatia utukufu mukubwa wale wenye wanamutambua,* na atawafanya watawale kati ya watu wengi; na atagawa inchi kwa bei.

40 “Katika wakati wa mwisho mufalme wa kusini atasukumana naye,* na mufalme wa kaskazini atamushambulia akiwa na magari na wapanda-farasi na mashua* nyingi; na ataingia katika inchi hizo na kuzifagia kama mafuriko. 41 Pia ataingia katika inchi ya lile Pambo,*+ na inchi nyingi zitakwazwa. Lakini hizi ndizo zitaponyoka kutoka katika mukono wake: Edomu na Moabu na sehemu kubwa ya Waamoni. 42 Na ataendelea kunyoosha mukono wake juu ya inchi hizo; na kuhusu inchi ya Misri, haitaponyoka. 43 Na atatawala juu ya hazina zenye kufichwa za zahabu na feza na juu ya vitu vyote vyenye kutamanika* vya Misri. Na Walibya na Waetiopia watafuata hatua zake.*

44 “Lakini habari kutoka mashariki* na kutoka kaskazini zitamusumbua, na ataenda kwa kasirani kali ili kuharibu na kuangamiza watu wengi. 45 Na atasimamisha mahema yake ya kifalme kati ya bahari kubwa na mulima mutakatifu wa lile Pambo;*+ na atakuja mupaka kwenye mwisho wake, na hakutakuwa mwenye atamusaidia.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine