Hosea
8 “Tia baragumu kwenye kinywa chako!+
Mutu mumoja anakuja kama tai ili kushambulia nyumba ya Yehova,+
Kwa maana wamevunja agano langu+ na wamekosea sheria yangu.+
2 Wananililia, ‘Mungu wangu, sisi, Israeli, tunakujua!’+
3 Israeli amekataa mambo ya muzuri.+
Adui amufuatilie.
4 Wameweka wafalme, lakini hapana kupitia mimi.
Wameweka wakubwa, lakini sikuwatambua.
5 Kitoto-dume chako cha ngombe kimekataliwa, Ee Samaria.+
Kasirani yangu inawaka juu yao.+
Watashindwa kuwa bila kosa* mupaka wakati gani?
6 Kwa maana kitu hiki kimetoka Israeli.
Fundi ndiye alikitengeneza, hapana Mungu;
Kitoto-dume cha ngombe wa Samaria kitavunjwa vipande-vipande.
Kama kitu chochote kinatokezwa, wageni watakimeza.+
Sasa watakuwa kati ya mataifa,+
Kama chombo chenye hakipendwe.
9 Kwa maana wamepanda kuenda Ashuru,+ kama punda wa pori mwenye kuwa peke yake.
Efraimu amelipa wanamuke ili wakuwe wapenzi wake.+
10 Hata kama wapenzi wenye wao walilipa wametoka kati ya mataifa,
Sasa nitawakusanya pamoja;
Wataanza kuteseka+ kwa sababu ya muzigo wenye mufalme na wakubwa waliwalazimisha kubeba.
11 Kwa maana Efraimu ameongeza mazabahu ili kutenda zambi.+
Yamekuwa mazabahu yake ili atende zambi.+
13 Wananitolea zawadi za zabihu, na wanakula nyama,
Lakini Yehova hapendezwe nazo.+
Sasa atakumbuka kosa lao na kuwapatia azabu kwa sababu ya zambi zao.+
Lakini nitatuma moto katika miji yake,
Na utateketeza minara ya kila muji.”+