Amosi
1 Maneno ya Amosi,* mwenye alikuwa mumoja wa wafugaji wa kondoo wa Tekoa,+ yenye alipokea katika maono kuhusu Israeli katika siku za Mufalme Uzia+ wa Yuda na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mufalme wa Israeli, miaka mbili mbele ya lile tetemeko la inchi.+ 2 Alisema:
“Yehova atanguruma kutoka Sayuni,
Na atapandisha sauti yake kutoka Yerusalemu.
Malisho ya wachungaji yataomboleza,
Na kichwa cha Mulima Karmeli kitakauka.”+
3 “Yehova anasema hivi:
‘“Kwa sababu Damasko ameasi* mara tatu (3), na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu wamepiga Gileadi kama vile watu wanapiga-piga nafaka kwa vifaa vya chuma vya kupiga-piga nafaka.+
4 Kwa hiyo nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli,+
Na utateketeza minara yenye ngome ya Ben-hadadi.+
5 Nitavunja mapingo* ya muji wa Damasko;+
Nitaharibu wakaaji wa Bikat-aveni
Na mutawala* wa Bet-edeni;
Na watu wa Siria watapelekwa katika uhamisho kule Kiri,”+ ni vile Yehova anasema.’
6 Yehova anasema hivi:
‘“Kwa sababu Gaza ameasi mara tatu (3),+ na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa maana walikamata kikundi chote cha watu wenye walihamishwa+ ili kuwatia katika mukono wa Edomu.
7 Kwa hiyo nitatuma moto juu ya ukuta wa Gaza,+
Na utateketeza minara yake yenye ngome.
8 Nitaharibu wakaaji wa Ashdodi,+
Nitanyoosha mukono wangu ili kushambulia Ekroni,+
Na Wafilisti wenye kubakia wataangamia,”+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.’
9 Yehova anasema hivi:
‘Kwa sababu Tiro ameasi+ mara tatu (3), na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu walitia kikundi chote cha watu wenye walihamishwa katika mukono wa Edomu,
Na kwa sababu hawakukumbuka agano la ndugu.+
10 Kwa hiyo nitatuma moto juu ya ukuta wa Tiro,
Na utateketeza minara yake yenye ngome.’+
11 Yehova anasema hivi:
‘Kwa sababu Edomu ameasi mara tatu (3),+ na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu alimufuatilia ndugu yake kwa upanga,+
Na kwa sababu alikataa kuonyesha rehema;
Katika kasirani yake aliendelea kuwapasua vipande-vipande,
Na angali anaendelea kuwakasirikia.+
13 Yehova anasema hivi:
‘“Kwa sababu Waamoni wameasi mara tatu (3),+ na kwa sababu wameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu walipasua wanamuke wenye mimba wa Gileadi ili waongeze ukubwa wa eneo lao.+
14 Kwa hiyo nitawasha moto kwenye ukuta wa Raba,+
Na utateketeza minara yake yenye ngome,
Kutakuwa makelele ya vita katika siku hiyo ya mapigano,
Kutakuwa zoruba kali katika siku hiyo ya upepo wa zoruba.
15 Na mufalme wao atapelekwa katika uhamisho pamoja na wakubwa wake,”+ ni vile Yehova anasema.’