Amosi
4 “Musikie neno hili, ninyi ngombe wa Bashani,
Wenye kukaa kwenye mulima wa Samaria,+
Ninyi wanamuke wenye kuiba watu wa hali ya chini+ na kuponda-ponda maskini,
Wenye kuambia bwana zao,* ‘Mutuletee kitu fulani cha kunywa!’
2 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova ameapa kwa utakatifu wake,
‘“Muangalie! Siku zinakuja wakati atawainua kwa kulabu* za muchinjaji
Na wenye kubakia kati yenu kwa ndoano za samaki.
3 Mutaenda inje kupitia matundu katika ukuta, kila mumoja akienda mbele moja kwa moja;
Na mutatupwa inje kuelekea Harmoni,” ni vile Yehova anasema.’
5 Muteketeze kwa moto zabihu ya shukrani ya mukate wenye kutiwa chachu;+
Mutangaze kwa sauti kubwa matoleo yenu ya kujipendea!
Kwa maana ni vile munapenda kufanya, Enyi watu wa Israeli,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
6 ‘Na kwa upande wangu, nilifanya meno yenu yakuwe safi kwa sababu ya kukosa chakula* katika miji yenu yote
Na nilifanya mukate ukosekane katika nyumba zenu zote;+
Lakini hamukunirudilia,’+ ni vile Yehova anasema.
7 ‘Pia niliwaima mvua miezi tatu (3) mbele ya mavuno;+
Nilifanya mvua inyeshe juu ya muji mumoja lakini sikuifanya inyeshe juu ya muji mwingine.
Shamba moja lilipata mvua,
Lakini shamba lingine lenye halikupata mvua lilikauka.
8 Watu wa miji mbili ao tatu (3) walienda kwenye muji mwingine wakiyumba-yumba ili kunywa maji,+
Na hawakukuwa wanatosheka;
Lakini hamukunirudilia,’+ ni vile Yehova anasema.
9 ‘Niliwapiga kwa joto lenye kuunguza na kuvu.+
Muliongeza bustani na mashamba yenu ya mizabibu,
Lakini nzige wakakula miti ya tini na mizeituni yenu;+
Na bado hamukunirudilia,’+ ni vile Yehova anasema.
10 ‘Nilituma kati yenu ugonjwa wa kuambukiza kama ule wa Misri.+
Niliua vijana wenu wanaume kwa upanga+ na nilikamata farasi wenu.+
Nilifanya harufu ya mubaya ya kambi zenu ipande mupaka katika matundu ya pua zenu;+
Lakini hamukunirudilia,’ ni vile Yehova anasema.
11 ‘Nilitokeza uharibifu kati yenu
Kama vile uharibifu wa Mungu juu ya Sodoma na Gomora.+
Na mulikuwa kama kipande cha muti chenye kilitoshwa katika moto;
Lakini hamukunirudilia,’+ ni vile Yehova anasema.
12 Kwa hiyo hayo ndiyo mambo yenye nitakutendea, Ee Israeli.
Kwa sababu nitakutendea mambo hayo,
Ujitayarishe ili kukutana na Mungu wako, Ee Israeli.