Amosi
6 “Ole wao wale wenye kujitumainia* katika Sayuni,
Wale wenye kujisikia salama katika mulima wa Samaria,+
Watu wa maana wa taifa la kwanza kati ya mataifa,
Wale wenye nyumba ya Israeli inaenda kwao!
2 Muvuke muende Kalne na muone.
Mutoke kule na muende katika Hamati Kubwa,+
Na mushuke mupaka Gati ya Wafilisti.
Je, miji hiyo iko muzuri kuliko falme hizi,*
Ao je, eneo lao ni kubwa kuliko lenu?
4 Wanalala kwenye vitanda vya pembe za tembo+ na kujinyoosha kwenye vitanda,+
Na wanakula wana-kondoo wa kundi na vitoto-dume vya ngombe vyenye kunenepa;*+
5 Wanatunga-tunga nyimbo wakati wanasikia sauti ya kinubi,*+
Na kama Daudi, wanatengeneza vyombo vya muziki;+
6 Wanakunywa divai ndani ya mabakuli yenye kujaa+
Na wanajipakaa mafuta ya muzuri sana.
Lakini hawaogope* musiba wa Yosefu.+
7 Kwa hiyo wataenda katika uhamisho wakiwa mbele ya wenye kuenda katika uhamisho,+
Na karamu za kupitisha mipaka za wale wenye kujianika zitaisha.
8 ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova ameapa kwa jina lake,’*+ ni vile Yehova Mungu wa majeshi anasema,
‘“Ninachukia kiburi cha Yakobo,+
Ninachukia minara yake yenye ngome,+
Na nitatia muji wake katika mukono wa maadui pamoja na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake.+
9 “‘“Na watu kumi (10) wakibakia katika nyumba moja, wao pia watakufa. 10 Mutu wa jamaa* atakuja ili kuwapeleka inje na kuwateketeza mumoja mumoja kwa moto. Atatosha mifupa yao ndani ya nyumba; kisha atauliza kila mutu mwenye kuwa katika vyumba vya ndani, ‘Je, ungali hapa na watu wengine?’ Naye atasema, ‘Hakuna mutu!’ Kisha atasema, ‘Nyamaza! Kwa maana huu hauko wakati wa kutaja jina la Yehova.’”
11 Kwa maana Yehova ndiye anatoa amri,+
Na atabomoa nyumba kubwa na kuifanya kuwa rundo la majiwe,
Na nyumba ya kidogo kuwa mabomoko.+
12 Je, farasi wanakimbia kwenye mwamba,
Ao je, mutu anaweza kulima na ngombe kwenye mwamba?