Obadia
1 Maono ya Obadia:*
Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi juu ya Edomu:+
“Tumesikia habari kutoka kwa Yehova,
Mujumbe ametumwa kati ya mataifa:
‘Musimame, na tujitayarishe kupigana naye.’”+
2 “Angalia! Nimekufanya kuwa mudogo sana kati ya mataifa;
Unazarauliwa sana.+
3 Kimbelembele cha moyo wako kimekudanganya,+
Wewe mwenye kukaa katika makimbilio ya mwamba,
Mwenye kukaa katika nafasi ya juu, unasema katika moyo wako,
‘Ni nani mwenye atanishusha chini katika dunia?’
4 Hata kama unajenga makao yako juu* kama tai,
Ao kama unatia chicha yako* kati ya nyota,
Nitakushusha chini kutoka pale,” ni vile Yehova anasema.
Je, hawangeiba tu kile wanataka?
Ao kama ni wakusanya-zabibu ndio wangekuja kwako,
Je, hawangeacha masalio fulani nyuma?+
6 Ona namna Esau ametafutwa!
Namna hazina zake zenye kufichwa zimetafutwa!
7 Wamekufukuza kufikia kwenye mupaka.
Wote wenye walifanya agano pamoja na wewe wamekudanganya.
Watu wenye walifanya amani pamoja na wewe wamekushinda.
Wale wenye wanakula mukate pamoja na wewe wataweka mutego wa wavu* chini yako,
Lakini hautatambua.
8 Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,
“Je, sitaharibu wenye hekima katika Edomu+
Na wenye utambuzi katika eneo lenye milima la Esau?
9 Na wapiganaji-vita wako wataogopa sana,+ Ee Temani,+
Kwa sababu kila mutu mwenye kuwa katika eneo lenye milima la Esau ataharibiwa katika mauaji.+
11 Siku yenye ulisimama pembeni,
Siku yenye wageni walipeleka jeshi lake katika utekwa,+
Wakati wageni waliingia katika mulango wake mukubwa na kupiga kura+ juu ya Yerusalemu,
Ulitenda kama wao.
12 Haukupaswa kufurahi juu ya siku ya ndugu yako katika siku ya musiba wake,+
Haukupaswa kushangilia siku watu wa Yuda waliangamia,+
Na haukupaswa kujivuna siku walikuwa wanateseka.
13 Haukupaswa kuingia katika mulango mukubwa wa watu wangu katika siku ya musiba wao,+
Haukupaswa kushangilia taabu yake katika siku ya musiba wake,
Na haukupaswa kuweka mikono yako juu ya mali yake katika siku ya musiba wake.+
14 Haukupaswa kusimama kwenye makutano ya barabara ili kuua wenye kuponyoka,+
Na haukupaswa kutoa wenye waliokoka kwa maadui wao katika siku ya musiba.+
15 Kwa sababu siku ya Yehova ya kuhukumu mataifa yote inakaribia.+
Kama vile umefanya, ni vile utafanyiwa.+
Mambo yenye ulitendea wengine yatarudia juu ya kichwa chako mwenyewe.
16 Kwa sababu kama vile mulikunywa divai kwenye mulima wangu mutakatifu,
Ni vile mataifa yote yataendelea kukunywa.+
Yatakunywa na kumeza kasirani yangu,
Na yatakuwa kama hayajapata kuwa hata siku moja.
17 Lakini wale wenye wataponyoka watakuwa juu ya Mulima Sayuni,+
Nao utakuwa mutakatifu;+
Na nyumba ya Yakobo itariti mali ya watu hao.+
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto,
Nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto,
Na nyumba ya Esau itakuwa kama majani yenye kukauka;
Watawachoma na kuwateketeza kwa moto,
Na hakuna mutu mwenye ataokoka katika nyumba ya Esau,+
Kwa maana Yehova mwenyewe amesema vile.
Watariti eneo la mashamba la Efraimu na eneo la mashamba la Samaria,+
Na Benyamini atariti Gileadi.
20 Na watu wenye walihamishwa wa boma hili,*+
Watu wa Israeli watariti inchi ya Wakanaani mupaka Sarefati.+
Na watu wa Yerusalemu wenye walipelekwa katika uhamisho, wenye walikuwa Sefaradi, watariti miji ya Negebu.+