Mika
6 Tafazali, musikie jambo lenye Yehova anasema.
Musimame, mupeleke kesi ya hukumu mbele ya milima,
Na vilima visikie sauti yenu.+
2 Musikie kesi ya hukumu ya Yehova, Enyi milima,
Ninyi misingi imara ya dunia,+
Kwa maana Yehova iko* na kesi ya hukumu pamoja na watu wake;
Atabishana na Israeli:+
3 “Watu wangu, nimewafanya nini?
Nimewachokesha namna gani?+
Mushuhudie juu yangu.
4 Kwa maana niliwatosha katika inchi ya Misri,+
Niliwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa;+
Nilituma Musa, Haruni, na Miriamu mbele yenu.+
5 Watu wangu, tafazali, mukumbuke jambo lenye Mufalme Balaki wa Moabu alipendekeza,+
Na jambo lenye Balaamu mwana wa Beori alimujibu+
—Mambo yenye yalitokea kuanzia Shitimu+ mupaka Gilgali+—
Ili mujue matendo yenye haki ya Yehova.”
6 Nitakuja na nini mbele ya Yehova?
Nitainama na nini mbele ya Mungu mwenye kuwa juu?
Je, nikuje mbele yake na matoleo mazima ya kuteketezwa,
Na vitoto-dume vya ngombe vya mwaka mumoja?+
7 Je, Yehova atafurahia maelfu ya kondoo-dume,
Na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+
Je, nitoe mwana wangu muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya uasi wangu,
8 Ee mwanadamu, amekuambia mambo mema.
Na Yehova anataka* ufanye nini?
9 Sauti ya Yehova inaita muji;
Watu wenye kuwa na hekima yenye kutenda wataogopa jina lako.
Musikilize fimbo na mwenye aliiweka.+
10 Je, hazina za uovu zingali katika nyumba ya muovu
Na kipimo cha efa* chenye hakienee chenye kuchukiza?
11 Je, ninaweza kuwa na mwenendo safi* kama niko na mizani* ya uovu,
Na mufuko wa majiwe ya kupimia ya udanganyifu?+
12 Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri,
Na wakaaji wake wanasema uongo;+
Ulimi wao unasema udanganyifu katika kinywa chao.+
13 “Kwa sababu hiyo, nitakuumiza kwa kukupiga,+
Na kukufanya kuwa ukiwa kwa sababu ya zambi zako.
14 Utakula lakini hautashiba;
Utakuwa bila kitu ndani yako.+
Vitu vyenye utaondoa, hautavibeba kwa usalama,
Na vyenye unabeba, nitavitoa kwa upanga.
15 Utapanda mbegu, lakini hautavuna.
Utakanyanga zeituni, lakini hautatumia hayo mafuta;
Na utatengeneza divai mupya, lakini hautaikunywa.+
16 Kwa sababu unafuata maagizo ya Omri na kazi yote ya nyumba ya Ahabu,+
Na unafuata mashauri yao.