Zekaria
7 Na katika mwaka wa ine (4) wa Mufalme Dario, neno la Yehova likakuja kwa Zekaria+ katika siku ya ine ya mwezi wa kenda (9), ni kusema, mwezi wa Kislevu.* 2 Watu wa Beteli wakatuma Shareza na Regem-meleki na watu wake ili kuomba rehema ya* Yehova, 3 wakaambia makuhani wa nyumba ya* Yehova wa majeshi na manabii: “Je, nilie katika mwezi wa tano (5)+ na kujizuia kula, kama vile nimekuwa nikifanya kwa miaka hii mingi?”
4 Neno la Yehova wa majeshi likakuja tena kwangu, na kusema: 5 “Ambia watu wote wa inchi na makuhani, ‘Wakati mulifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano (5) na katika mwezi wa saba (7)+ kwa miaka makumi saba (70),+ je, kweli mulifunga kwa ajili yangu? 6 Na wakati mulikuwa munakula na kunywa, je, hamukukuwa munakula kwa ajili yenu wenyewe na kunywa kwa ajili yenu wenyewe? 7 Je, hamupaswe kutii maneno yenye Yehova alitangaza kupitia manabii wa zamani,+ wakati Yerusalemu na miji yenye kuizunguka ilikuwa na wakaaji na ilikuwa na amani, na wakati Negebu na Shefela zilikuwa na wakaaji?’”
8 Neno la Yehova likakuja tena kwa Zekaria, na kusema: 9 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Muhukumu kwa haki ya kweli,+ na mutendeane kwa upendo mushikamanifu+ na rehema. 10 Musimupunje mujane wala mutoto mwenye hana baba,*+ mugeni+ wala maskini;+ na musipangiane uovu katika mioyo yenu.’+ 11 Lakini waliendelea kukataa kusikiliza,+ na kwa kichwa-nguvu wakageuza migongo yao,+ na wakafunga masikio yao ili wasisikie.+ 12 Wakafanya mioyo yao kuwa kama almasi*+ na hawakutii sheria* na maneno yenye Yehova wa majeshi alituma kwa roho yake kupitia manabii wa zamani.+ Kwa hiyo Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+
13 “‘Kama vile hawakusikiliza wakati niliita,*+ vilevile sikukuwa ninasikiliza wakati waliita,’+ ni vile Yehova wa majeshi anasema. 14 ‘Na niliwatawanya kwa zoruba ya upepo kila mahali katika mataifa yote yenye hawakujua,+ na inchi iliachwa ukiwa nyuma yao, bila mutu wa kupita ndani ao wa kurudia;+ kwa maana waligeuza inchi yenye kutamanika kuwa kitu cha kuogopesha sana.’”