Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matendo 21
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Matendo

      • Safari ya kuenda Yerusalemu (1-14)

      • Kufika Yerusalemu (15-19)

      • Paulo anafuata shauri la wazee (20-26)

      • Muvurugo katika hekalu; Paulo anakamatwa (27-36)

      • Paulo anaruhusiwa kusema na watu wengi (37-40)

Matendo 21:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 173-174

Matendo 21:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 173-174

Matendo 21:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “upande wa bandari.”

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 173-175

Matendo 21:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 21:10-12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 175

Matendo 21:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 176

Matendo 21:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Matendo 21:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 6:3, 5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 176-177

Matendo 21:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mabikira.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoe 2:28; Mdo 2:17; 1 Kor. 11:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 176-177

Matendo 21:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 11:27, 28

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 177

Matendo 21:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 20:22, 23; 21:33
  • +Mdo 9:15, 16

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi,

    uku. 177-178, 189

Matendo 21:12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 177-178

Matendo 21:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kunifanya kuwa zaifu katika moyo?”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 20:24; 2 Kor. 4:10, 11; 2 Tim. 4:6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 177-178

    Munara wa Mulinzi,

    15/5/2008, uku. 32

Matendo 21:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “tukanyamaza.”

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 178

Matendo 21:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 12:17; 15:13; Gal 1:19; 2:9; Yak 1:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 112, 181

Matendo 21:19

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 181-182

Matendo 21:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 15:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 182-183

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2003, uku. 23-24

    15/10/2002, uku. 30

Matendo 21:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Rom. 2:28, 29; 1 Kor. 7:18-20

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 182, 183-185

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2003, uku. 24

Matendo 21:23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 184-185

Matendo 21:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Kor. 9:20

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 184-185

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2003, uku. 24

    15/6/2000, uku. 14

Matendo 21:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “vitu vyenye viliuawa bila kutoshwa damu.”

  • *

    Neno la Kigiriki por·neiʹa. Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 35:2; Kut 34:15
  • +Mwa 9:4; Law. 3:17; 17:10; 1 Sa. 14:32, 33
  • +Law. 17:13; Kum 12:23, 24
  • +Mdo 15:28, 29; 1 Kor. 6:9; Kol 3:5; 1 Tes. 4:3; 1 Pe. 4:3

Matendo 21:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Kor. 9:20

Matendo 21:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 24:5, 6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2001),

    15/12/2001, uku. 22-23

    “Kila Andiko,” uku. 243

Matendo 21:29

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 20:4; 2 Tim. 4:20

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2001),

    15/12/2001, uku. 22-23

Matendo 21:33

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 20:22, 23; 21:10, 11

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2001),

    15/12/2001, uku. 21

Matendo 21:37

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/2/2011, uku. 5

Matendo 21:38

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/3/2010, uku. 15

Matendo 21:39

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Flp 3:4, 5
  • +Mdo 22:3

Matendo 21:40

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 26:14

Maandiko ingine

Mdo. 21:4Mdo 21:10-12
Mdo. 21:8Mdo 6:3, 5
Mdo. 21:9Yoe 2:28; Mdo 2:17; 1 Kor. 11:5
Mdo. 21:10Mdo 11:27, 28
Mdo. 21:11Mdo 20:22, 23; 21:33
Mdo. 21:11Mdo 9:15, 16
Mdo. 21:13Mdo 20:24; 2 Kor. 4:10, 11; 2 Tim. 4:6
Mdo. 21:18Mdo 12:17; 15:13; Gal 1:19; 2:9; Yak 1:1
Mdo. 21:20Mdo 15:1
Mdo. 21:21Rom. 2:28, 29; 1 Kor. 7:18-20
Mdo. 21:241 Kor. 9:20
Mdo. 21:25Mwa 35:2; Kut 34:15
Mdo. 21:25Mwa 9:4; Law. 3:17; 17:10; 1 Sa. 14:32, 33
Mdo. 21:25Law. 17:13; Kum 12:23, 24
Mdo. 21:25Mdo 15:28, 29; 1 Kor. 6:9; Kol 3:5; 1 Tes. 4:3; 1 Pe. 4:3
Mdo. 21:261 Kor. 9:20
Mdo. 21:28Mdo 24:5, 6
Mdo. 21:29Mdo 20:4; 2 Tim. 4:20
Mdo. 21:33Mdo 20:22, 23; 21:10, 11
Mdo. 21:39Flp 3:4, 5
Mdo. 21:39Mdo 22:3
Mdo. 21:40Mdo 26:14
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Matendo 21:1-40

Matendo ya Mitume

21 Wakati mwishowe tuliweza kujiondoa kwao na kusafiri katika bahari, tulienda moja kwa moja mupaka Kosi, siku yenye ilifuata tukafika Rode, na kutoka kule tukaenda Patara. 2 Wakati tulipata mashua* ya kuvuka kuenda Foinike, tukapanda ndani na tukasafiri katika bahari. 3 Kisha kufika mahali kwenye tuliweza kuona kisiwa cha Kipro, tukakiacha nyuma upande wa kushoto* tukaelekea Siria, na tukafika Tiro kwenye mashua* ilipaswa kushusha mizigo yake. 4 Tukatafuta wanafunzi na wakati tuliwapata tukakaa kule siku saba (7). Lakini kupitia roho, wanafunzi wakamuambia Paulo tena na tena asikanyange Yerusalemu.+ 5 Basi, kisha kumaliza wakati wetu kule, tukaondoka na tukaanza kuenda, lakini wote, pamoja na wanamuke na watoto, wakatusindikiza mupaka inje ya muji. Na tukapiga magoti pembeni ya bahari, tukasali 6 na tukaagana. Halafu tukapanda katika mashua,* nao wakarudia kwenye nyumba zao.

7 Kisha tukamaliza safari ya bahari kutoka Tiro na tukafika Tolemai, na tukasalimia ndugu na kukaa nao siku moja. 8 Siku yenye ilifuata tukatoka na kufika Kaisaria, na tukaingia katika nyumba ya Filipo mweneza-injili, mwenye alikuwa mumoja wa wale wanaume saba (7),+ na tukakaa pamoja naye. 9 Mutu huyo alikuwa na mabinti ine (4) wenye walikuwa hawajaolewa,* na walikuwa wanatoa unabii.+ 10 Lakini wakati tulikuwa tumekaa kule kwa siku fulani, nabii mwenye kuitwa Agabo+ akashuka kutoka Yudea. 11 Akakuja mahali tulikuwa na akakamata mukaba* wa Paulo, akajifunga miguu na mikono na kusema: “Roho takatifu inasema hivi, ‘Mwanaume mwenye mukaba huu, Wayahudi watamufunga hivi kule Yerusalemu+ na kumutia katika mikono ya watu wa mataifa.’”+ 12 Sasa wakati tulisikia vile, sisi na wale wenye walikuwa pale tukaanza kumuomba asipande kuenda Yerusalemu. 13 Kisha Paulo akasema: “Sababu gani munalia na kujaribu kuregeza azimio langu?* Mukuwe hakika kwamba niko tayari hapana kufungwa tu lakini pia kufa kwa ajili ya jina la Bwana Yesu+ kule Yerusalemu.” 14 Wakati tulishindwa kumushawishi, tukaacha kumupinga* na tukasema: “Mapenzi ya Yehova* yatendeke.”

15 Sasa kisha siku hizo tukajitayarisha kwa ajili ya safari na tukaanza kuenda Yerusalemu. 16 Wamoja kati ya wanafunzi kutoka Kaisaria wakaenda pia pamoja na sisi, wakatupeleka kwa Munasoni wa Kipro, mwanafunzi wa zamani mwenye tulipaswa kuwa wageni katika nyumba yake. 17 Wakati tulifika Yerusalemu, ndugu wakatukaribisha kwa furaha. 18 Lakini siku yenye ilifuata Paulo akaenda pamoja na sisi kwa Yakobo,+ na wazee wote walikuwa pale. 19 Akawasalimia na kuanza kuwaelezea kwa urefu mambo yenye Mungu alifanya katikati ya mataifa kupitia utumishi wake.

20 Kisha kusikia jambo hilo, wakaanza kumutukuza Mungu, lakini wakamuambia: “Ndugu, unaona namna kuko maelfu ya Wayahudi wenye wamekuwa waamini, na wote ni wenye bidii kwa ajili ya Sheria.+ 21 Lakini wamesikia habari fulani juu yako kwamba wewe umekuwa ukifundisha Wayahudi wote kati ya mataifa kuacha sheria ya Musa, ukiwaambia wasitahiri watoto wao na wasifuate desturi za kawaida.+ 22 Sasa ni nini kinapaswa kufanywa? Hawatakosa kusikia kwamba umefika. 23 Basi fanya jambo lenye tunakuambia: Tuko na wanaume ine (4) wenye walijiwekea wenyewe naziri. 24 Chukua watu hawa na ujitakase pamoja nao kulingana na desturi na uwalipie mambo yenye wako nayo lazima, ili wanyolewe vichwa vyao. Kisha wote watajua kwamba habari zenye waliambiwa juu yako haziko za kweli, lakini unatembea kwa utaratibu na pia unashika Sheria.+ 25 Na waamini wenye kutoka katika mataifa, tumewatumia uamuzi wetu kwa maandishi kwamba wanapaswa kuepuka vitu vyenye vilitolewa zabihu kwa sanamu+ na pia damu,+ na vitu vyenye vilinyongwa,*+ na uasherati.”*+

26 Kisha, siku yenye ilifuata Paulo akachukua wanaume hao na kujitakasa pamoja nao kulingana na desturi+ na akaingia katika hekalu ili kujulisha ni wakati gani siku za kujitakasa zingeisha na ni wakati gani toleo lilipaswa kutolewa kwa ajili ya kila mumoja wao.

27 Sasa wakati zile siku saba (7) zilikaribia kuisha, Wayahudi kutoka Asia, wakati walimuona katika hekalu, wakachochea kile kikundi chote cha watu, na wakamukamata, 28 wakisema kwa sauti kubwa: “Wanaume wa Israeli, mutusaidie! Mwanaume huyu ndiye anafundisha watu kila mahali kupinga watu wetu na Sheria yetu na mahali hapa. Na zaidi ya hayo, aliingiza hata Wagiriki katika hekalu na amechafua mahali hapa patakatifu.”+ 29 Kwa maana walikuwa wamemuona kwanza Trofimo+ Mwefeso katika muji akiwa pamoja naye, na waliwaza Paulo alikuwa amemuingiza katika hekalu. 30 Muji wote ukakuwa katika muvurugo, watu wakakimbia pamoja na wakakuja na kumukamata Paulo na kumukokotea inje ya hekalu, na mara moja milango ikafungwa. 31 Wakati walikuwa wanajaribu kumuua, kiongozi wa kikundi cha maaskari akapata habari kwamba Yerusalemu yote ilikuwa katika muvurugo; 32 na mara moja akachukua maaskari na maofisa wa jeshi na wakashuka mbio kuenda kule. Wakati watu hao waliona ule kiongozi wa jeshi na maaskari, wakaacha kumupiga Paulo.

33 Kisha, ule kiongozi wa jeshi akakaribia, akamukamata na kumutia chini ya ulinzi na kuamuru afungwe kwa minyororo mbili;+ kisha akauliza yeye alikuwa nani na alikuwa amefanya nini. 34 Lakini wamoja kati ya kile kikundi cha watu wakaanza kusema jambo moja kwa sauti kubwa, na wengine jambo lingine. Basi kwa kuwa yeye mwenyewe alishindwa kujua jambo lolote la hakika kwa sababu ya fujo hizo, akaamuru apelekwe kwenye makao ya maaskari. 35 Lakini wakati alifika kwenye ngazi, ilikuwa lazima maaskari wamubebe kwa sababu ya jeuri ya kikundi hicho cha watu, 36 kwa maana watu wengi waliendelea kuwafuata, wakisema kwa sauti kubwa: “Umuue!”

37 Wakati alikuwa karibu kuingizwa katika makao ya maaskari, Paulo akamuuliza ule kiongozi wa jeshi: “Ninaruhusiwa kukuambia jambo fulani?” Akasema: “Je, unaweza kusema Kigiriki? 38 Je, haiko wewe ndiye ule Mumisri mwenye hivi majuzi alichochea uasi na kuongoza wale wanaume elfu ine (4 000) wenye visu kuingia katika jangwa?” 39 Halafu Paulo akasema: “Mimi kwa kweli ni Muyahudi+ wa Tarso+ katika Kilikia, raia wa muji wenye haukose kujulikana. Basi ninakuomba, uniruhusu niseme na watu hawa.” 40 Kisha kumupatia ruhusa, Paulo, akiwa amesimama kwenye ngazi, akafanyia watu alama kwa mukono. Wakati kulikuwa kimya kabisa, akawaambia katika luga ya Kiebrania,+ kwa kusema:

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine