Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matendo 23
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Matendo

      • Paulo anasema mbele ya Sanhedrini (1-10)

      • Bwana anamutia Paulo nguvu (11)

      • Mupango wa kumuua Paulo (12-22)

      • Paulo anapelekwa Kaisaria (23-35)

Matendo 23:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 24:15, 16; 2 Kor. 1:12; Ebr 13:18; 1 Pe. 3:16

Matendo 23:2

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 187

Matendo 23:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 22:28

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 187

    Munara wa Mulinzi,

    1/11/2002, uku. 5

Matendo 23:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 26:4, 5; Flp 3:4, 5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 187-188

    Munara wa Mulinzi,

    15/4/2005, uku. 31

Matendo 23:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wanatangaza mbele ya watu wote.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 4:1, 2

Matendo 23:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 22:6, 7, 17, 18

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 188

Matendo 23:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 18:9
  • +Mdo 27:23, 24; 28:23, 30, 31

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 189-191

Matendo 23:12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 191

Matendo 23:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

Matendo 23:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

Matendo 23:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:15

Matendo 23:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 190-191

Matendo 23:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, karibu saa 3 ya usiku (21:00).

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 191

Matendo 23:25

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2001),

    15/12/2001, uku. 22

Matendo 23:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 21:31-33
  • +Mdo 16:37; 22:25

Matendo 23:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 22:30

Matendo 23:29

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 25:19

Matendo 23:30

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:16

Matendo 23:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:23, 24

Matendo 23:34

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 21:39; 22:3

Matendo 23:35

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 24:1

Maandiko ingine

Mdo. 23:1Mdo 24:15, 16; 2 Kor. 1:12; Ebr 13:18; 1 Pe. 3:16
Mdo. 23:5Kut 22:28
Mdo. 23:6Mdo 26:4, 5; Flp 3:4, 5
Mdo. 23:8Mdo 4:1, 2
Mdo. 23:9Mdo 22:6, 7, 17, 18
Mdo. 23:11Mdo 18:9
Mdo. 23:11Mdo 27:23, 24; 28:23, 30, 31
Mdo. 23:20Mdo 23:15
Mdo. 23:21Mdo 23:12
Mdo. 23:27Mdo 21:31-33
Mdo. 23:27Mdo 16:37; 22:25
Mdo. 23:28Mdo 22:30
Mdo. 23:29Mdo 25:19
Mdo. 23:30Mdo 23:16
Mdo. 23:31Mdo 23:23, 24
Mdo. 23:34Mdo 21:39; 22:3
Mdo. 23:35Mdo 24:1
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Matendo 23:1-35

Matendo ya Mitume

23 Paulo akakazia Sanhedrini macho, akasema: “Wanaume, ndugu, nimejiendesha kwa zamiri safi+ kabisa mbele ya Mungu mupaka leo.” 2 Halafu kuhani mukubwa Anania akaagiza wale wenye walikuwa wamesimama pembeni yake wamupige kwenye kinywa. 3 Paulo akamuambia: “Mungu atakupiga, wewe ukuta wenye umepakwa rangi nyeupe. Je, unakaa ili kunihukumu kulingana na Sheria na wakati uleule unavunja Sheria hiyo kwa kuamuru nipigwe?” 4 Wale wenye walikuwa wamesimama pembeni wakasema: “Je, unatukana kuhani mukubwa wa Mungu?” 5 Na Paulo akasema: “Ndugu, sikujua kama yeye ni kuhani mukubwa. Kwa maana imeandikwa, ‘Haupaswe kusema mubaya juu ya mutawala wa watu wako.’”+

6 Sasa Paulo, wakati alijua kwamba sehemu moja ilikuwa Wasadukayo na ile ingine Wafarisayo, akasema kwa sauti kubwa katika Sanhedrini: “Wanaume, ndugu, mimi ni Mufarisayo,+ mwana wa Wafarisayo. Ninahukumiwa kwa sababu ya tumaini la ufufuo wa wafu.” 7 Wakati alisema jambo hilo, kukatokea ugomvi kati ya Wafarisayo na Wasadukayo, na mukusanyiko ukagawanyika. 8 Kwa maana Wasadukayo wanasema hakuna ufufuo wala malaika wala roho, lakini Wafarisayo wanakubali* mambo hayo yote.+ 9 Basi kukatokea muvurugo mukubwa, na wamoja kati ya waandishi wa chama cha Wafarisayo wakasimama na kuanza kubishana kwa ukali, na kusema: “Hatuone kosa lolote katika mutu huyu, lakini kama roho ao malaika alizungumuza naye+—.” 10 Basi wakati ugomvi ulikuwa mukubwa, kiongozi wa jeshi akaogopa kwamba watamupasua Paulo vipande-vipande, na akaamuru maaskari washuke wamutoshe katikati yao kisha wamulete kwenye makao ya maaskari.

11 Lakini usiku wenye ulifuata, Bwana akasimama pembeni yake na kumuambia: “Usiogope!+ Kwa maana kama vile umekuwa ukitoa ushahidi kamili juu yangu katika Yerusalemu, ni vile unapaswa kutoa ushahidi katika Roma+ pia.”

12 Wakati ilikuwa muchana, Wayahudi wakafanya shauri na wakajifunga kwa kiapo, wakisema kwamba hawatakula ao kunywa mupaka wakuwe wamemuua Paulo. 13 Kulikuwa watu zaidi ya makumi ine (40) wenye walifanya mupango huo mubaya kwa njia ya kiapo. 14 Watu hao wakaenda kwa wakubwa wa makuhani na wazee na kusema: “Sisi tumejifunga kabisa kwa kiapo kwamba tulaaniwe kama tunakula kitu chochote mbele ya kumuua Paulo. 15 Basi sasa ninyi pamoja na Sanhedrini mumuambie kiongozi wa jeshi amushushe kwenu ikuwe kama vile munataka kuchunguza mambo yake muzuri zaidi. Lakini mbele afike karibu, tutakuwa tayari ili kumuua.”

16 Hata hivyo, mwana wa dada ya Paulo akasikia juu ya mupango wa kumuvizia wenye walikuwa wamefanya, akaingia katika makao ya maaskari na akamujulisha Paulo. 17 Kisha Paulo akamuita mumoja wa maofisa wa jeshi na kumuambia: “Peleka kijana huyu kwa kiongozi wa jeshi, kwa maana iko* na jambo fulani la kumuambia.” 18 Basi akamukamata na kumupeleka kwa kiongozi wa jeshi na kusema: “Mufungwa Paulo aliniita na kuniomba nilete kijana huyu kwako, kwa sababu iko* na jambo fulani la kukuambia.” 19 Kiongozi wa jeshi akamukamata kwenye mukono akamupeleka mahali kwenye hakuna watu na kumuuliza: “Unataka kuniambia nini?” 20 Akasema: “Wayahudi wamekubaliana kukuomba umushushe Paulo kwenye Sanhedrini kesho, ikuwe kama vile wanakusudia kupata habari zaidi juu ya mambo yake.+ 21 Lakini usiwaache wakushawishi, kwa maana kuko wanaume wao zaidi ya makumi ine (40) wenye wako tayari kujificha ili kumushambulia, na wamejifunga kwa kiapo kwamba walaaniwe kama wanakula ao kunywa mbele ya kumuua;+ na sasa wako tayari, wanangojea ahadi kutoka kwako.” 22 Basi ule kiongozi wa jeshi akamuacha kijana huyo aende, kisha kumuamuru: “Usiambie mutu yeyote kwamba umenijulisha jambo hili.”

23 Akaita wawili kati ya maofisa wa jeshi na kuwaambia: “Mutayarishe maaskari mia mbili (200) waende moja kwa moja mupaka Kaisaria, pia wapanda-farasi makumi saba (70) na watu mia mbili wenye mikuki, saa ya tatu (3) usiku.* 24 Pia, mutayarishe farasi kwa ajili ya Paulo ili apande juu yao, na wamupeleke salama mupaka kwa gavana Feliksi.” 25 Na akaandika barua yenye ujumbe huu:

26 “Klaudio Lisia, kwa Muheshimiwa, Gavana Feliksi: Jambo! 27 Mwanaume huyu alikamatwa na Wayahudi na walikuwa karibu kumuua, lakini nikakuja mbio pamoja na maaskari wangu na kumuokoa,+ kwa sababu nilijua kwamba ni Muroma.+ 28 Na kwa kuwa nilitaka kujua sababu gani walikuwa wanamushitaki, nilimupeleka katika Sanhedrini+ yao. 29 Nikatambua kwamba ameshitakiwa juu ya mambo ya Sheria yao,+ lakini hakushitakiwa kwa jambo hata moja lenye linastahili kifo ao kufungwa katika gereza. 30 Lakini kwa sababu nimejulishwa+ mupango mubaya wenye umefanywa juu ya mwanaume huyu, ninamutuma kwako mara moja na ninaamuru wale wenye wanamushitaki wamushitaki mbele yako.”

31 Basi wale maaskari wakamukamata Paulo+ kama vile waliagizwa na wakamupeleka usiku mupaka Antipatri. 32 Siku yenye ilifuata wakaruhusu wapanda-farasi waendelee pamoja naye, lakini wao wakarudia kwenye makao ya maaskari. 33 Wale wapanda-farasi wakaingia Kaisaria na wakamupatia gavana ile barua na pia wakamuleta Paulo mbele yake. 34 Basi akaisoma na kuuliza ametoka katika jimbo gani, na akajua kwamba alikuwa ametoka Kilikia.+ 35 Akasema: “Nitasikiliza mambo yako yote wakati wale wenye wanakushitaki watafika.”+ Na akaamuru awekwe chini ya ulinzi katika nyumba ya kifalme ya Herode.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine