Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matendo 26
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Matendo

      • Paulo anajitetea mbele ya Agripa (1-11)

      • Paulo anaeleza namna aligeuka kuwa muamini (12-23)

      • Festo na Agripa wanatoa mawazo yao (24-32)

Matendo 26:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 25:13

Matendo 26:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 24:5, 9

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/11/2003, uku. 15-16

Matendo 26:3

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/11/2003, uku. 15-16

Matendo 26:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “taifa langu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Gal 1:13, 14

Matendo 26:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:6; Flp 3:4, 5
  • +Mdo 22:3

Matendo 26:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 24:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 198-199

Matendo 26:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 24:20, 21

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 199

Matendo 26:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “munahukumu.”

Matendo 26:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoh 16:2; Mdo 8:3; 1 Kor. 15:9; Gal 1:13; 1 Tim. 1:13
  • +Mdo 9:1, 2, 14

Matendo 26:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 9:3-5; 22:6-8

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 200

Matendo 26:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Muchokoo ni fimbo yenye chongo yenye inatumiwa ili kumuongoza munyama.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, uku. 1958

    Munara wa Mulinzi,

    1/8/2011, uku. 23

    1/10/2003, uku. 32

    Kutoa Ushahidi, uku. 199-200

Matendo 26:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 22:14, 15; Gal 1:11, 12; 1 Tim. 1:12

Matendo 26:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 22:21; Rom. 11:13

Matendo 26:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 61:1
  • +Kol 1:13
  • +Yoh 8:12; 2 Kor. 4:6
  • +Efe 2:1, 2
  • +1 Yo. 3:5

Matendo 26:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 9:22
  • +Mdo 9:28
  • +Mt 3:8

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 200

Matendo 26:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 21:30, 31

Matendo 26:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Lu 24:27, 44; Rom. 3:21

Matendo 26:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 22:7; 35:19; Isa 50:6; 53:5
  • +Zab 16:10
  • +Zab 18:49; Isa 11:10; Lu 2:30-32

Matendo 26:24

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 201-202

    Munara wa Mulinzi (2001),

    15/12/2001, uku. 24

Matendo 26:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kwenye pembe.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoh 18:20

Matendo 26:27

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/11/2003,

    uku. 16-17

Matendo 26:28

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 202

    Munara wa Mulinzi,

    15/11/2003, uku. 16-17

Matendo 26:30

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 202

Matendo 26:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:26, 29; 25:24, 25

Matendo 26:32

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 25:11, 12

Maandiko ingine

Mdo. 26:1Mdo 25:13
Mdo. 26:2Mdo 24:5, 9
Mdo. 26:4Gal 1:13, 14
Mdo. 26:5Mdo 23:6; Flp 3:4, 5
Mdo. 26:5Mdo 22:3
Mdo. 26:6Mdo 24:15
Mdo. 26:7Mdo 24:20, 21
Mdo. 26:10Yoh 16:2; Mdo 8:3; 1 Kor. 15:9; Gal 1:13; 1 Tim. 1:13
Mdo. 26:10Mdo 9:1, 2, 14
Mdo. 26:13Mdo 9:3-5; 22:6-8
Mdo. 26:16Mdo 22:14, 15; Gal 1:11, 12; 1 Tim. 1:12
Mdo. 26:17Mdo 22:21; Rom. 11:13
Mdo. 26:18Isa 61:1
Mdo. 26:18Kol 1:13
Mdo. 26:18Yoh 8:12; 2 Kor. 4:6
Mdo. 26:18Efe 2:1, 2
Mdo. 26:181 Yo. 3:5
Mdo. 26:20Mdo 9:22
Mdo. 26:20Mdo 9:28
Mdo. 26:20Mt 3:8
Mdo. 26:21Mdo 21:30, 31
Mdo. 26:22Lu 24:27, 44; Rom. 3:21
Mdo. 26:23Zab 22:7; 35:19; Isa 50:6; 53:5
Mdo. 26:23Zab 16:10
Mdo. 26:23Zab 18:49; Isa 11:10; Lu 2:30-32
Mdo. 26:26Yoh 18:20
Mdo. 26:31Mdo 23:26, 29; 25:24, 25
Mdo. 26:32Mdo 25:11, 12
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Matendo 26:1-32

Matendo ya Mitume

26 Agripa+ akamuambia Paulo: “Unaruhusiwa kujitetea.” Kisha Paulo akanyoosha mukono wake na kuanza kusema ili kujitetea:

2 “Kuhusu mambo yote yenye Wayahudi wananishitaki,+ Mufalme Agripa, ninajiona mwenyewe kuwa na furaha kwamba ni mbele yako ninajitetea leo hii, 3 zaidi sana kwa sababu unajua muzuri kabisa desturi zote na vilevile mabishano kati ya Wayahudi. Kwa hiyo, ninakuomba unisikilize kwa uvumilivu.

4 “Kwa kweli, namna niliishi tangu ujana kati ya watu wangu* na katika Yerusalemu inajulikana muzuri na Wayahudi wote+ 5 wenye walinijua zamani, kama watapenda kutoa ushahidi, kwamba niliishi nikiwa Mufarisayo+ kulingana na musimamo mukali wa ibada+ katika zehebu* letu. 6 Lakini sasa, kwa sababu ya tumaini la ahadi yenye Mungu alitolea mababu zetu,+ nimeitwa kwenye hukumu; 7 ni ahadi ileile ndiyo makabila yetu kumi na mbili (12) yanatumaini kuona inatimia, kwa kumutolea utumishi mutakatifu kwa bidii usiku na muchana. Juu ya tumaini hili, ninashitakiwa na Wayahudi,+ Ee Mufalme.

8 “Sababu gani munaona* kuwa ni jambo lenye haliwezi kuaminika kwamba Mungu afufue wafu? 9 Mimi kwa upande wangu, niliamini kwamba nilipaswa kufanya matendo mengi ili kupinga jina la Yesu Munazareti. 10 Ni vile kabisa nilifanya kule Yerusalemu, na nilifunga watakatifu wengi katika gereza,+ kwa maana nilikuwa nimepewa mamlaka na wakubwa wa makuhani;+ na wakati walipaswa kuuawa, nilipiga kura yangu ili kukubali jambo hilo. 11 Kwa kuwapatia azabu mara nyingi katika masinagogi yote, nilijaribu kuwalazimisha wakane imani yao; na kwa sababu nilikuwa nimewakasirikia sana, nilifikia kuwatesa hata katika miji ingine.

12 “Nilikuwa ninafanya vile wakati nilikuwa katika safari ya kuenda Damasko na nilikuwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa wakubwa wa makuhani, 13 katikati ya muchana niliona katika barabara, Ee Mufalme, mwangaza kutoka mbinguni wenye kupita mwangaza wa jua ukanizunguka mimi na wale wenye walikuwa wanasafiri pamoja na mimi.+ 14 Na wakati tulikuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti inaniambia katika luga ya Kiebrania: ‘Sauli, Sauli, sababu gani unanitesa? Kuendelea kupiga-piga miguu yako kwenye michokoo* kutafanya uumie.’ 15 Lakini nikasema: ‘Wewe ni nani Bwana?’ Na Bwana akasema: ‘Mimi ni Yesu, mwenye unatesa. 16 Hata hivyo, inuka na usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuchague ukuwe mutumishi na shahidi wa mambo yenye umeona na pia mambo yenye nitakuonyesha juu yangu.+ 17 Na nitakuokoa kutoka kwa watu hawa na kutoka kwa mataifa yenye ninakutuma kwao+ 18 ili kuwafungua macho,+ kuwageuza kutoka katika giza+ kuingia katika mwangaza+ na kutoka kwenye mamlaka ya Shetani+ wageukie kwa Mungu, ili wasamehewe zambi+ na wapate uriti kati ya wale wenye walitakaswa kupitia imani yao katika mimi.’

19 “Kwa hiyo, Mufalme Agripa, mimi sikukosa kutii maono hayo kutoka mbinguni, 20 lakini kwanza kwa wale wenye kuwa Damasko+ kisha kwa wale wenye kuwa Yerusalemu,+ na katika inchi yote ya Yudea, na pia kwa mataifa, nilipeleka ujumbe kwamba wanapaswa kutubu na kugeukia kwa Mungu kwa kufanya matendo yenye yanaonyesha kwamba wametubu.+ 21 Ndiyo sababu Wayahudi walinikamata katika hekalu na wakataka kuniua.+ 22 Lakini, kwa sababu nimepata musaada kutoka kwa Mungu, ninaendelea mupaka leo kutoa ushahidi kwa wadogo na kwa wakubwa pia, bila kusema jambo lolote isipokuwa tu yale yenye Manabii na pia Musa walisema yatatokea+⁠—⁠ 23 kwamba Kristo angeteseka+ na kwamba akiwa wa kwanza kufufuliwa kutoka kwa wafu,+ angetangaza mwangaza kwa watu hawa na pia kwa mataifa.”+

24 Sasa wakati Paulo alikuwa anajitetea kwa kusema mambo hayo, Festo akasema kwa sauti kubwa: “Unapoteza akili, Paulo! Kusoma sana kunakufanya upoteze akili!” 25 Lakini Paulo akasema: “Mimi sipoteze akili, Ee Mutukufu Festo, lakini ninasema maneno ya kweli na ya akili ya muzuri. 26 Kwa maana, kwa kweli, mufalme mwenye ninazungumuza naye kwa uhuru anajua muzuri mambo haya; niko hakika kwamba kati ya mambo haya hakuna hata jambo moja lenye hajue, kwa maana kati ya mambo hayo hakuna hata jambo moja lenye lilifanywa kwa uficho.*+ 27 Mufalme Agripa, je, unaamini Manabii? Ninajua unawaamini.” 28 Lakini Agripa akamuambia Paulo: “Kwa wakati kidogo ungenishawishi nikuwe Mukristo.” 29 Halafu Paulo akasema: “Ninamuomba Mungu kwamba ikuwe ni kwa wakati kidogo ao murefu, haiko wewe tu lakini pia watu wote wenye wananisikia leo wakuwe kama vile mimi niko, lakini tu wasikuwe na vifungo hivi vya gereza.”

30 Kisha mufalme akasimama, vilevile gavana na Bernike na watu wenye walikuwa wamekaa pamoja nao. 31 Lakini wakati walikuwa wanaondoka, wakaanza kuambiana: “Mutu huyu hafanye jambo lolote lenye linastahili kifo ao vifungo vya gereza.”+ 32 Kisha Agripa akamuambia Festo: “Mutu huyu angeachwa huru kama hangekuwa ameomba kesi yake ya hukumu isikilizwe na Kaisari.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine