Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Unaweza kuwa na tumaini hata kama kuko magumu
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • Unaweza kuwa na tumaini hata kama kuko magumu

      “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.”​—2 TIMOTEO 3:1.

      ULISHAKASIKIA ao ulishakajionea moja kati ya mambo ya kuhuzunisha yenye inaonyeshwa hapa chini?

      ● Ugonjwa mubaya unaua watu wengi.

      ● Watu wengi sana wanakufa juu ya njala.

      ● Tetemeko ya inchi inaua maelfu ya watu na kuacha wengine bila fasi ya kuishi.

      Mu habari zenye kufuata utasoma mambo yenye itakufanya uwaze sana juu ya hali zenye ziko mu dunia leo. Tena, utavumbula kama Biblia ilikuwaka ilishatabiri kama zile hali zitatokea mu wakati wenye unaitwa “siku za mwisho.”

      Kusudi ya zile habari haiko kukusadikisha kama tunaishi mu dunia yenye inajaa magumu. Juu inawezekana na weye uko unajionea ile magumu. Lakini, kusudi ni kukusaidia ukuwe na tumaini. Zitazungumuzia maunabii sita na namna iko inatimia. Na ile itakusaidia uone kama “siku za mwisho” zinakaribia kumalizika. Zitaonyesha pia mawazo yenye watu fulani wanatoa juu ya kupinga kama tunaishi mu siku za mwisho, na zitatutolea sababu ya kuamini kama hivi karibuni maisha itakuwa muzuri.

  • 1. Matetemeko makubwa ya inchi
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • 1. Matetemeko makubwa ya inchi

      “Kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi.”​—LUKA 21:11.

      ● Winnie alikuwa na mwaka moja na nusu hivi wakati aliokolewa kutoka katika mabomoko ya nyumba mu inchi ya Haiti. Watangazaji wa habari wa televizyo fulani wenye walikuwa pale walisikia wakati alikuwa analia mu ile mabomoko. Aliokoka ile tetemeko ya inchi lakini wazazi wake walikufa.

      USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Wakati tetemeko ya inchi ya kipimo cha 7.0 ilitokea mu inchi ya Haiti mu Mwezi wa 1, 2010, watu zaidi ya 300 000 walikufa. Na wengine milioni 1.3 walibakia bila fasi ya kuishi. Hata kama ile tetemeko ya inchi njo ilikuwa ya nguvu sana, kulikuwa matetemeko ingine ya inchi. Matetemeko makubwa karibu 18 ilitokea mu maeneo mbalimbali kati ya Mwezi wa 4, 2009 na Mwezi wa 4, 2010.

      WATU FULANI WANASEMA NINI? Leo hakuna matetemeko mingi kuliko zamani; matetemeko inaonekana kuwa ya mingi juu tu teknolojia ya sasa inatusaidia kupata habari za mingi juu ya ile matetemeko kupita zamani.

      ILE NI KWELI? Fikiria hii jambo: Biblia haikazie hesabu ya matetemeko ya inchi mu siku za mwisho. Lakini inasema kama “matetemeko makubwa ya inchi” itatokea “mahali pamoja kisha pengine;” na ile njo inafanya ile matetemeko ikuwe moja kati ya alama za siku za mwisho.​—Marko 13:8; Luka 21:11.

      UNAWAZA NINI? Tuko tunaona matetemeko makubwa ya inchi sawa vile Biblia ilisemaka?

      Matetemeko ya inchi haiko tu njo alama yenye kuonyesha kama tunaishi mu siku za mwisho. Lakini, ni unabii moja kati ya maunabii mbalimbali yenye iko inatimia. Fikiria unabii wa pili.

      [Kwenye Picha Zilitoka ukurasa wa 4]

      © William Daniels/​Panos Pictures

  • 2. Njala
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • 2. Njala

      “Kutakuwa upungufu wa chakula.”​—MARKO 13:8.

      ● Mwanaume mumoja anafika mu kijiji ya Quaratadji, mu inchi ya Niger. Ndugu zake, dada zake, na watu wengine fulani wa jamaa yake wametoka pia mu eneo ya mbali juu ya kukimbia njala. Lakini ule mwanaume analala yeye peke ku murago. Juu ya nini iko yeye peke? Sidi, mukubwa wa kile kijiji anasema hivi: “Hana uwezo wa kulisha [familia yake] na anashindwa kuendelea kuona vile wako wanateseka.”

      USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Mu dunia yote karibu mutu 1 kati ya watu 7 hapate chakula yenye iko nayo lazima kila siku. Hali iko mubaya zaidi mu inchi zenye kuwa kusini ya jangwa (désert) ya Sahara, kwenye mutu 1 kati ya watu 3 anashindwaka kabisa kupata chakula ya kuenea. Juu ya kuelewa muzuri ile jambo, fikiria familia yenye iko na baba, mama, na mutoto. Kama kuko chakula ya kuenea tu watu wawili, nani njo atabakia na njala? Baba? Mama? Ao mutoto? Ule ni uamuzi wenye familia fulani zinalazimika kukamata kila siku.

      WATU FULANI WANASEMA NINI? Dunia inatoshaka chakula ya kuenea kila mutu. Inaomba tu kuigawanya muzuri.

      ILE NI KWELI? Ni kweli kama leo watu wenye kufanya kazi ya kulima wako wanavuna chakula mingi na kuisafirisha sana kuliko zamani. Na serikali za wanadamu zinapaswa kugawanya muzuri ile chakula juu ya kumaliza njala. Lakini, hata kama zimejikaza kufanya vile kwa miaka mingi, zimeshindwa.

      UNAWAZA NINI? Marko 13:8 iko inatimia? Hata kama teknolojia inaendelea sana, watu wako wanateseka kwa sababu ya njala mu dunia yote?

      Mara mingi, matetemeko ya inchi na njala vinaletaka tatizo ingine yenye nayo ni alama ya siku za mwisho.

      [Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 5]

      “Mutoto 1 hivi kati ya watoto 3 wenye wanakufaka kwa sababu ya ugonjwa wa pneumonie, ugonjwa wa kuhara, na magonjwa ingine angepona kama angekuwa anakula muzuri.”​—ANN M. VENEMAN, MWENYE ALIKUWA MUMOJA WA WASIMAMIZI WA UNICEF.

      [Kwenye Picha Zilitoka ukurasa wa 5]

      © Paul Lowe​/Panos Pictures

  • 3. Magonjwa
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • 3. Magonjwa

      “Kutakuwa . . . magonjwa.”​—LUKA 21:11.

      ● Bonzali, alikuwa munganga mu inchi moja ya Afrika kwenye watu wameteseka kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe. Alifanya yake yote juu ya kutunza kikundi fulani ya wafanyakazi wenye walikuwa wanakufa kwa sababu ya ugonjwa wa Marburg.a Aliomba musaada kwa wakubwa wa serikali wenye walikuwa mu muji ingine mukubwa zaidi, lakini hawakumusaidia. Musaada ulifika kisha miezi ine, lakini Bonzali alikuwa alishakufa. Wafanyakazi wenye alikuwa anajaribu kuokoa walimuambukiza ugonjwa wa Marburg.

      USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Magonjwa ya mapafu (sawa vile pneumonie), magonjwa ya kuhara, SIDA, tuberculose, na malaria iko kati ya magonjwa ya mubaya yenye inatesa sana wanadamu. Mu mwaka wa 2004, ile magonjwa tano iliua watu karibu milioni 10.7. Ni kusema ile mwaka yote, ile magonjwa ilikuwa inaua mutu moja kila segonde tatu.

      WATU FULANI WANASEMA NINI? Watu wanaendelea kuongezeka mu dunia, njo maana hesabu ya wagonjwa inapaswa tu kuwa mingi. Kuko watu wengi wenye wanaweza kuambukizwa.

      ILE NI KWELI? Watu wemeongezeka sana mu dunia. Lakini pia, uwezo wa mwanadamu wa kupima magonjwa, kuizuia, na kuitunza umeongezeka. Kwa hiyo, magonjwa na matokeo ya ile magonjwa inapaswa kupunguka. Lakini mambo haiko vile, iko njo inaongezeka.

      UNAWAZA NINI? Watu wako wanateseka kwa sababu ya magonjwa ya mubaya, sawa vile Biblia ilisemaka?

      Matetemeko ya inchi, njala, na magonjwa inafanya watu wengi sana wateseke. Watu wengine wengi wako wanateswa na wanadamu wenzao; wengi wanateswa na watu wenye wanapaswa kuwalinda. Ona mambo yenye Biblia ilisema kama ingetokea.

      [Maelezo ya chini]

      a Marburg ni homa ya kutokwa na damu, yenye inaletwa na virusi fulani yenye inafanana na virusi ya Ebola.

      [Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 6]

      “Sawa vile ni mubaya sana kukuliwa na simba ao munyama mwingine wa pori, vilevile ni mubaya sana kukuliwa na ugonjwa wenye kuwa ndani ya mwili wetu na kuona vile ule ugonjwa uko unaua watu wengine.”​—MICHAEL OSTERHOLM, MUTU MWENYE KUJIFUNZA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA.

      [Kwenye Picha Zilitoka ukurasa wa 6]

      © William Daniels/​Panos Pictures

  • 4. Watu hawatapenda watu wa familia yao
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • 4. Watu hawatapenda watu wa familia yao

      “Watu watakuwa wenye . . . hawana upendo wa asili.”​—2 TIMOTEO 3:1-3.

      ● Chris anaishi kaskazini mwa Pays de Galles. Anatumikaka na kikundi ya kusaidia watu wenye kutendewa mubaya ku nyumba. Anasema hivi: “Ninakumbuka mwanamuke mwenye alikuwa amepigwa sana kiasi ya kwamba sikumutambua, hata kama nilikuwaka nilishamuona. Wanamuke wengine wameumia sana katika moyo mupaka wanashindwa hata kukuangalia.”

      USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Mu inchi moja ya Afrika karibu mutu 1 kati ya watu 3 alitendewa mubaya kingono wakati alikuwa mutoto. Uchunguzi wenye ulifanywa mu ile inchi ulionyesha kama zaidi ya mwanaume 1 kati ya wanaume 3 aliona kama haiko mubaya mutu kupiga bibi yake. Lakini haiko wanamuke tu njo wanatendewaka mubaya ku nyumba. Kwa mufano, mu inchi ya Kanada, karibu wanaume 3 kati ya wanaume 10 wamepigwa ao kutendewa mubaya na bibi zao.

      WATU FULANI WANASEMA NINI? Tangu zamani watu wanatendewaka mubaya ku nyumba. Leo tu njo watu wanakazia akili ile jambo kuliko zamani.

      ILE NI KWELI? Ni kweli kama leo njo watu wengi wanazungumuzia sana tatizo ya kutendewa mubaya ku nyumba. Lakini, ile imefanya hesabu ya watu wenye kutendewa mubaya ku nyumba ipunguke? Hapana. Leo, hesabu ya watu wenye hawaonyeshane upendo mu familia inaendelea kuongezeka.

      UNAWAZA NINI? 2 Timoteo 3:1-3 iko inatimia? Watu wengi wanakosa kuonyesha watu wa familia yao upendo wenye kwa kawaida watu wa familia wanapaswa kuonyeshana?

      Unabii wa tano wenye uko unatimia leo unahusu dunia. Ona jambo yenye Biblia inasema juu ya ule unabii.

      [Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 7]

      “Watu hawazoee kujulisha polisi wakati wanatendewa mubaya ku nyumba. Kwa kukadiria, mwanamuke anaendaka kushitaki bwana yake kisha bwana yake kumutendea mubaya mara 35.”​—MUSEMAJI WA KIKUNDI YA KUTETEA WATU WENYE KUTENDEWA MUBAYA KU NYUMBA, MU PAYS DE GALLES.

  • 5. Kuharibu dunia
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • 5. Kuharibu dunia

      “[Mungu] ataharibu wale wenye wanaharibu dunia.”​—UFUNUO 11:18.

      ● Mwanaume mwenye kuitwa Pirri anatengenezaka pombe ya muti ya ngazi mu muji wa Kpor, Nigeria. Mafuta mingi ilimwangika fasi kwenye muto Niger unajigawanya, na ile iliharibisha biashara yake. Anasema hivi: “Inaua samaki, inaharibisha ngozi yetu, na inachafua mito yetu. Sina tena kazi ya kunisaidia kupata mambo yenye niko nayo lazima.”

      USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Watu fulani wenye kufanya uchunguzi wanasema kama tone milioni 6.5 za uchafu zinaingiaka mu bahari za mu dunia kila mwaka. Karibu nusu ya ile uchafu ni vitu vya plastike vyenye vitabakia mu maji kwa miaka mingi mbele vifikie kuoza. Zaidi ya kuharibu dunia, wanadamu wako wanatumia mali ya dunia haraka sana. Uchunguzi umeonyesha kama dunia iko na lazima ya mwaka moja na miezi tano ili kutokeza tena vitu vyenye wanadamu wametumia mu mwaka moja. Gazeti moja ya Australia inasema hivi: “Kama watu wanaendelea kuongezeka na kutumia sana mali ya dunia, kufikia mwaka wa 2035, tutakuwa na lazima ya dunia mbili.”​—Sydney Morning Herald.

      WATU FULANI WANASEMA NINI? Wanadamu wako na akili sana. Wanaweza kumaliza ile matatizo na kuokoa dunia.

      ILE NI KWELI? Vikundi mbalimbali na watu fulani-fulani wamejikaza sana kuelezea watu faida ya kutunza dunia yetu. Lakini dunia inaendelea kuchafuliwa sana.

      UNAWAZA NINI? Inaomba Mungu afanye jambo fulani juu ya kuokoa dunia, sawa vile amesema?

      Zaidi ya maunabii tano yenye tumezungumuzia, Biblia ilitabiri pia mambo fulani ya muzuri yenye ingetokea mu siku za mwisho. Moja kati ya ile mambo inazungumuziwa mu unabii wa sita.

      [Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 8]

      “Zamani, kwenye ninaishi kulikuwa sawa vile paradiso, lakini sasa ninaishi fasi kwenye kunayala uchafu wenye unayala sumu​—MANENO YA ERIN TAMBER KUHUSU MATOKEO YA MAFUTA (PETROLE) YENYE ILIMWANGIKA KWENYE GUBA YA MEKSIKO MU 2010. ANAISHI PEMBENI YA BAHARI, MU INCHI YA AMERIKA.

      [Sanduku katika ukurasa wa 8]

      Ni Kosa ya Mungu?

      Juu Biblia ilitabiri mambo ya mubaya yenye tuko tunaona leo, ni kusema ni kosa ya Mungu kama ile mambo iko inatokea? Yeye njo anatuleteaka mateso? Unaweza kupata majibu ya ile maulizo mu sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

      [Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 8]

      U.S. Coast Guard photo

  • 6. Kazi ya kuhubiri mu dunia yote
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • 6. Kazi ya kuhubiri mu dunia yote

      “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”​—MATAYO 24:14.

      ● Vaiatea anaishi mu kisiwa kidogo yenye kuwa mbali sana mu Bahari ya Pasifike na watu kidogo njo wanaishi kule. Hata vile, Mashahidi wa Yehova wametembelea Vaiatea na majirani wake. Juu ya nini? Juu Mashahidi wa Yehova wanapenda kuhubiria watu wote habari njema ya Ufalme wa Mungu, hata ikuwe wanaishi wapi.

      USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Mashahidi wa Yehova wako wanahubiri habari ya Ufalme wa Mungu mu dunia yote. Mu mwaka wa 2010 tu, walipitisha saa miliare 1.6 mu kazi ya kuhubiri, na walifanya vile mu inchi 236. Kwa kukadiria, kila Shahidi alihubiri dakika 30 kila siku. Mu miaka kumi yenye ilipita, walitoa na kugawanya vichapo miliare 20 vya kusaidia watu wajifunze Biblia.

      WATU FULANI WANASEMA NINI? Habari yenye iko mu Biblia inahubiriwaka tangu zamani.

      ILE NI KWELI? Ni kweli kwamba watu wengi wamehubiri habari fulani zenye kuwa mu Biblia. Lakini wengi wamefanya vile mu wakati kidogo tu na mu eneo ya kidogo. Tofauti na wale watu, Mashahidi wa Yehova wanahubiri mu dunia yote kwa njia yenye kupangwa muzuri, na wameweza kuhubiria mamilioni ya watu. Matengenezo yenye nguvu na yenye haina huruma imewapinga sana, hata vile wameendelea kuhubiri. (Marko 13:13) Zaidi ya ile, Mashahidi wa Yehova hawalipwe juu ya kuhubiri. Lakini wanatoa wakati wao juu ya kuhubiri, na wanapatia watu vichapo bila kuwaomba feza. Michango ya kujipendea njo inasaidia kazi yao iendelee.

      UNAWAZA NINI? “Habari njema ya Ufalme” iko inahubiriwa mu dunia yote? Kutimia kwa ule unabii kunaonyesha kama mambo ya muzuri iko karibu kutokea?

      [Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 9]

      “Tutaendelea kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii, na kufanya yetu yote ili kuhubiria watu mupaka wakati Yehova atasema tuache sasa.”​—KITABU CHA MWAKA CHA MASHAHIDI WA YEHOVA CHA 2010.

  • Karibuni mambo itakuwa muzuri
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 5 1
    • Karibuni mambo itakuwa muzuri

      “Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena . . . Lakini wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”​—ZABURI 37:10, 11.

      UNAPENDA kuona namna ule unabii utatimia? Tunatumaini unapenda. Kuko mambo yenye kutuhakikishia kama karibuni ule unabii utatimia.

      Habari zenye zilitangulia zilizungumuzia maunabii mbalimbali ya Biblia yenye inaonyesha waziwazi kama tunaishi mu “siku za mwisho.” (2 Timoteo 3:1-5) Mungu aliongoza waandikaji wa Biblia waandike ile mambo juu itupatie tumaini. (Waroma 15:4) Kutimia kwa ile maunabii kunaonyesha kama mateso yenye tuko napata leo inakaribia kuisha.

      Kisha siku za mwisho, kutatokea nini? Ufalme wa Mungu utatawala wanadamu wote. (Matayo 6:9) Ona maunabii ya Biblia yenye inaonyesha namna hali itakuwa ku dunia ile wakati:

      ● Hakutakuwa njala. “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima.”​—Zaburi 72:16.

      ● Hakutakuwa magonjwa. “Na hakuna mukaaji mwenye atasema: ‘Niko mugonjwa.’”​—Isaya 33:24.

      ● Dunia itakuwa tena ya muzuri. “Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”​—Isaya 35:1.

      Ile ni maunabii kidogo tu yenye kutia moyo yenye itatimia karibuni. Tunakutia moyo uombe Mashahidi wa Yehova wakuonyeshe juu ya nini wanaamini kabisa kama karibuni mambo itakuwa muzuri.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine