-
1 Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Kusali?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
1 Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Kusali?
WATU wengi wanapendaka kujua mambo yenye Biblia inasema juu ya sala. Ona maulizo 7 yenye watu wanazoeaka kujiuliza juu ya sala; kisha tuchunguze pamoja namna Biblia inajibia ile maulizo. Hizi habari ziko na kusudi ya kukusaidia uanze kusali. Na kama tayari unakuwaka unasali, zitakusaidia ukuwe unasali mu njia yenye itafanya Mungu asikilize sala zako.
MU dunia yote, mu kila desturi na dini, watu wanakuwaka wanasali. Wanakuwaka wanasali peke yao, ao mu vikundi. Wanakuwaka wanasali mu makanisa, mu mahekalu, mu masinagogi, mu misikiti, na fasi zingine za ibada. Wanatumikishaka vitu mbalimbali wakati wako wanasali, sawa vile vitabu vya sala, bushanga, sanamu, ao vitu vingine.
Wanadamu wako tofauti na viumbe vingine vyote ku dunia juu wao tu njo wanakuwaka wanasali. Kwa kweli, kuko mambo yenye tunafanyaka yenye wanyama nao wanafanyaka. Kwa mufano, sawa vile wanyama, tunakulaka, tunapumuaka, na tunakunywaka maji. Tena, siye wote tunazaliwaka, tunaishi, tunazeeka, na tunakufaka. (Muhubiri 3:19) Lakini, ni wanadamu tu njo wanakuwaka wanasali. Juu ya nini?
Bila kuenda huku na huku, jibu ni: tuko na lazima ya kusali. Watu wengi wanakuwaka wanasali juu wanapenda kuzungumuza na Mungu. Biblia inaonyesha kama Mungu alituumba na tamaa ya kufanya vile. (Muhubiri 3:11) Yesu Kristo alisemaka hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho.”—Matayo 5:3.
Kuko nafasi za mingi kwenye watu wanaendaka kuabudu na kusali. Ile yote inaonyesha kama siye wote tuko na mahitaji ya kiroho. Kusema kweli, watu wengi wanawazaka kama wanaweza kujitimizia wao wenyewe mahitaji yao ya kiroho ao kama wengine wanaweza kuwasaidia kutimiza ile mahitaji. Hata vile, hauone kama wanadamu hawana uwezo wa kujitimizia ile mahitaji? Siye wanadamu tuko na mipaka, maisha yetu ni ya mufupi, na kuko mambo mingi yenye hatuelewake. Tuko na lazima ya mutu wa kutusaidia kutimiza mahitaji yetu ya kiroho. Ule mutu anapaswa kuwa na hekima na nguvu kutushinda, na anapaswa kuishi muda murefu kutushinda. Ile mahitaji ya kiroho ni gani?
Waza kidogo: Kuko wakati ulikuwa kabisa na lazima ya kupata muongozo, hekima, ao majibu ya maulizo yenye ulionaka kama hakuna mwanadamu mwenye anaweza kujibia? Kuko siku ulikuwaka na lazima ya faraja kisha mutu mwenye ulikuwa unapenda sana kufa? Ao kuko siku ulikuwaka na lazima ya muongozo juu ukamate uamuzi fulani wa maana sana? Ao kuko wakati ulikuwaka na lazima kabisa ya kusamehewa juu zamiri ilikuwaka inakuhangaisha juu ya jambo fulani yenye ulifanya?
Biblia inaonyesha kama ni sawa kabisa kusali juu ya ile mambo yote. Biblia inaweza kukusaidia ujue namna ya kusali na mambo ya kusema mu sala, juu mu Biblia muko sala za wanaume na wanamuke wenye walikuwaka wanamutumikia Mungu kwa uaminifu. Walisali juu ya kuomba Mungu awafariji, awaongoze, awasamehe, na ajibie maulizo yenye ilikuwa inawahangaisha.—Zaburi 23:3; 71:21; Danieli 9:4, 5, 19; Habakuki 1:3.
Hata kama hawakusali juu ya mambo ileile, wote walijua jambo moja ya maana sana juu ya sala, jambo yenye watu wengi leo hawajue ao hawatiake mu akili. Walijua ni nani njo tunapaswa kusali kwake.
-
-
2 Tunapaswa Kusali kwa Nani?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
2 Tunapaswa Kusali kwa Nani?
MUNGU anasikilizaka sala zote? Vile njo watu wengi wanawazaka leo. Watu wengi wanawazaka kama dini zote ni za muzuri. Kwa hiyo, hata usali kwa mungu gani, ni sawa tu. Lakini, ile ni kweli kabisa?
Biblia inafundisha kama mara mingi watu hawakuwake wanasali kwa Mungu wa kweli. Zamani wakati Biblia iliandikwa, watu walizoea kusali kwa sanamu. Lakini, mara kwa mara Mungu aliwapatia angalisho juu ya ile tabia. Kwa mufano, Zaburi 115:4-6 inasema hivi juu ya sanamu: “Ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia.” Mambo iko wazi: Kusali kwa mungu mwenye hawezi kukusikia, ni kuchokea bure.
Habari fulani ya Biblia inatusaidia kuelewa ile jambo. Nabii wa kweli Eliya aliambiaka manabii wa Baali wasali kwa mungu wao, na kisha yeye atasali kwa Mungu wake. Eliya alisema kama Mungu wa kweli atajibia, lakini mungu wa uongo hatajibia. Manabii wa Baali waliitika kufanya vile. Walisali kwa bidii kwa wakati murefu, na walilia kwa sauti. Lakini, mungu wao hakuwajibia! Biblia inasema hivi: “Hakuna mutu yeyote mwenye alijibu; hakuna mwenye aliwasikiliza.” (1 Wafalme 18:29) Lakini mambo ilikuwa namna gani wakati Eliya alisali?
Kisha Eliya kusali, Mungu wake alijibia palepale. Alituma moto na ukateketeza zabihu ya Eliya. Juu ya nini sala ya Eliya njo ilijibiwa? Mu sala ya Eliya, yenye inapatikana mu 1 Wafalme 18:36, 37, muko jambo fulani ya maana yenye ilifanya Mungu ajibie sala ya Eliya. Sala yake haikukuwa hata ya murefu. Mu Kiebrania ya zamani, ile sala iko tu na maneno 30 hivi. Lakini, mu ile maneno kidogo, Eliya alisali kwa Mungu na kutaya jina yake ya pekee, Yehova, mara tatu.
Baali, mwenye jina yake inamaanisha “mumiliki” ao “bwana,” alikuwa mungu wa Wakanaani, na walikuwa wanamuita mu majina mbalimbali kulingana na fasi kwenye walikuwa wanaishi. Lakini, Yehova ni jina ya pekee ya Mungu mumoja tu mu ulimwengu wote muzima. Ule Mungu aliambiaka watu wake hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu; sipatie mutu yeyote utukufu wangu.”—Isaya 42:8.
Juu ya nini sala ya Eliya ilijibiwa lakini sala za manabii wa Baali hazikujibiwa? Wakati watu walikuwa wanaabudu Baali, walikuwa wanafanya uasherati na kumutolea Baali zabihu za wanadamu. Lakini, ibada ya Yehova iliheshimisha watu wake, Waisraeli, na iliwaepusha na ile matendo ya mubaya. Wazia hii jambo: Kama unapenda kutumia barua rafiki yako mwenye unaheshimia sana, utaituma ku jina ya mutu mwingine na mwenye iko na tabia za mubaya zenye ziko tofauti na zile za rafiki yako? Hapana!
Mambo yenye Eliya aliambiaka manabii wa Baali wafanye inaonyesha kama Mungu hasikilizake sala zote
Wakati unasali kwa Yehova, unasali kwa Muumbaji na Baba ya wanadamu wote.a Nabii Isaya alisali hivi: “Wewe, Ee Yehova, ni Baba yetu.” (Isaya 63:16) Na ule njo Mungu mwenye Yesu alizungumuzia wakati aliambia wanafunzi wake hivi: “Ninapanda kuenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.” (Yohana 20:17) Yehova njo Baba ya Yesu. Yeye njo Mungu mwenye Yesu alikuwa anasali kwake na kufundisha wanafunzi wake wakuwe wanasali kwake.—Matayo 6:9.
Je, Biblia inasema kama tunapaswa kusali kwa Yesu, kwa Maria, kwa watakatifu, ao kwa malaika? Hapana. Tunapaswa kusali kwa Yehova tu. Juu ya nini? Tuone sababu mbili. Ya kwanza, sala ni ibada, na Biblia inasema kama Yehova tu njo tunapaswa kuabudu. (Kutoka 20:5) Ya pili, Biblia inaonyesha kama yeye tu njo “musikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Hata kama Yehova anapatiaka wengine kazi mbalimbali, hakuna mwenye alishakapatia kazi ya kusikiliza sala. Ameahidi kusikiliza sala zetu yeye mwenyewe.
Njo maana, kama unapenda Mungu asikilize sala zako, usisahau hii maneno yenye Biblia inasema: “Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.” (Matendo 2:21) Lakini, Yehova anasikilizaka sala zote? Ao kuko mambo ingine yenye tunapaswa kujua kama tunapenda akuwe anasikiliza sala zetu?
a Watu wa dini fulani wanasema kama ni mubaya kutaya jina ya pekee ya Mungu, hata mu sala. Lakini, ile jina inapatikana karibu mara 7000 mu luga zenye zilitumiwa kuandika Biblia, zaidi sana mu sala za watumishi waaminifu wa Yehova zenye ziko mu kitabu ya Zaburi.
-
-
3 Tunapaswa Kusali Namna Gani?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
3 Tunapaswa Kusali Namna Gani?
DINI za mingi zinakazia kama mutu anapaswa kuwa mu hali fulani wakati iko anasali. Kwa mufano, anapaswa kusali na iko mwenye kusimama, kuikala, ao kupiga magoti. Tena, zinatia mukazo juu ya maneno yenye anapaswa kutia mu sala, na desturi fulani zenye anapaswa kufuata wakati iko anasali. Lakini, Biblia inatusaidia tujue mambo ya maana zaidi yenye tunapaswa kufikiria juu ya namna ya kusali.
Biblia inaonyesha kama watumishi waaminifu wa Mungu walikuwa wanasali mu hali mbalimbali. Wamoja walisali kimya-kimya, na wengine walisali kwa sauti, kupatana na hali yenye walikuwa ndani. Wamoja walisali na wako wanaangalia mbinguni, na wengine walisali na wako wenye kuinama. Hawakukuwa wanatumia sanamu, bushanga, ao vitabu vya sala. Lakini walikuwa wanamuambia Mungu maneno yenye inatoka mu moyo wao. Ni nini ilifanya Mungu asikilize sala zao?
Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, walikuwa wanasali kwa Mungu mumoja tu, Yehova. Kuko jambo ingine ya maana yenye ilifanya Mungu asikilize sala zao. 1 Yohana 5:14 inaonyesha ile jambo. Inasema hivi: “Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.” Tunapaswa kusali kupatana na mapenzi ya Mungu. Maana yake nini?
Juu tusali kupatana na mapenzi ya Mungu, tunapaswa kwanza kuijua. Njo maana, kujifunza Biblia ni jambo ya maana yenye itatusaidia tujue namna ya kusali juu Mungu atusikie. Ni kusema juu Mungu atusikie, inaomba tu tujue sana Biblia? Hapana, lakini Mungu anapenda tujifunze mapenzi yake, tujikaze kuielewa, na tutumikishe mu maisha yetu mambo yenye tuko tunajifunza. (Matayo 7:21-23) Tunapaswa kusali kupatana na mambo yenye tunajifunza.
Juu Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kusali kupatana na mapenzi yake, kuwa na imani, na kusali mu jina ya Yesu
Wakati tunajifunza juu ya Yehova na mapenzi yake, imani yetu inaongezeka. Na ile ni jambo ingine ya maana, juu tunapaswa kuwa na imani juu Mungu asikilize sala zetu. Yesu alisema hivi: “Mambo yote yenye munaomba katika sala, kama muko na imani, mutayapokea.” (Matayo 21:22) Imani haimaanishe kuitika-itika tu mambo bila kufikiri. Lakini, ni kuamini jambo yenye hata kama hatuione, kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama ni ya kweli. (Waebrania 11:1) Mu Biblia muko ushuhuda mbalimbali wenye kuonyesha kama hata kama hatumuonake Yehova, yeye ni mutu wa kweli, mwenye tunaweza kutumainia, na iko tayari kujibia sala za wale wenye wanamuamini. Zaidi ya ile, tunaweza kila mara kumuomba Yehova atupatie imani zaidi, na iko tayari kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima.—Luka 17:5; Yakobo 1:17.
Kuko jambo ingine ya maana yenye inaweza kufanya Yehova asikilize sala zetu. Yesu alisema hivi: “Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.” (Yohana 14:6) Yesu njo njia yenye inatusaidia kumukaribia Baba, Yehova. Njo maana, Yesu aliambia wanafunzi wake wasali mu jina yake. (Yohana 14:13; 15:16) Ile haimaanishe kama tunapaswa kusali kwa Yesu. Lakini, tunapaswa njo kusali mu jina ya Yesu, juu yeye njo alifanya iwezekane tumukaribie Baba yetu mukamilifu na mutakatifu.
Siku moja, wanafunzi wa Yesu walimuambiaka hivi: “Bwana, utufundishe kusali.” (Luka 11:1) Inaonekana kama hawakuwa wanamuomba Yesu awaambie mambo ya musingi yenye tumezungumuzia. Walipenda kabisa kujua mambo ya kutia mu sala. Ni sawa vile walimuuliza, ‘Tunaweza kusali juu ya mambo gani?’
-
-
4 Tunapaswa Kusali Juu ya Mambo Gani?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
4 Tunapaswa Kusali Juu ya Mambo Gani?
SALA ya Baba Yetu njo sala yenye Wakristo wamerudilia-rudilia sana kuliko sala ingine yoyote. Hata vile, wengi wanarudiliaka-rudiliaka maneno ya ile sala bila kuelewa maana yake. Watu wengi wanairudiliaka-rudiliaka kila siku. Lakini Yesu hakupendaka ile sala ikuwe inarudiliwa-rudiliwa vile. Juu ya nini tunasema vile?
Mbele tu Yesu afundishe ile sala, alisemaka hivi: “Wakati munasali, musiseme mambo yaleyale tena na tena.” (Matayo 6:7) Sasa, juu ya nini Yesu alifundishaka watu ile sala? Alipenda watu waiweke mu akili na wakuwe wanairudilia-rudilia? Hapana. Yesu alipenda njo kutufundisha mambo yenye tunapaswa kusema na ya kutia pa nafasi ya kwanza wakati tuko tunasali. Tuchunguze muzuri maneno ya ile sala. Inapatikana mu Matayo 6:9-13.
“Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.”
Kwa kusema vile, Yesu alikumbusha wanafunzi wake kama sala zote zinapaswa kumuendea Baba yake, Yehova. Lakini unajua juu ya nini jina ya Mungu ni ya maana na juu ya nini inapaswa kutakaswa, ao kufanywa kuwa takatifu?
Tangu wanadamu waanze kuishi ku dunia, Mungu amesemewa mambo mingi ya uongo, yenye imechafua jina yake. Shetani, adui ya Mungu, alimuita Yehova kuwa Mutawala muongo, mwenye anatawala tu kwa faida yake, na alisema kama Yehova hana haki ya kutawala viumbe vyake. (Mwanzo 3:1-6) Watu wengi wameunga mukono mawazo ya Shetani, na wanafundisha kama Mungu hana upendo, hana huruma, na anapendaka kulipiza kisasi. Na hata wengine wanasema kama haiko Mungu njo aliumbaka vitu vyote. Tena, wamefikia hata kushambulia jina yake. Wameondoa jina Yehova mu tafsiri fulani za Biblia na wanakataza watu kuitaya.
Biblia inaonyesha kama Mungu atamaliza ile mambo yote ya ukosefu wa haki. (Ezekieli 39:7) Wakati atafanya vile, atakupatia mambo yote yenye uko nayo lazima na atamaliza magumu yako yote. Atafanya vile namna gani? Maneno yenye kufuata mu sala ya Yesu inajibia ile ulizo.
“Ufalme wako ukuje.”
Leo, viongozi wa dini wako na mawazo yenye kupingana juu ya Ufalme wa Mungu. Lakini, wale wenye walikuwa wanamusikiliza Yesu wakati alikuwa anafundisha namna ya kusali, walijua kama manabii walikuwa wamesema kama kutatokea Masiya, Mukombozi mwenye alikuwa amechaguliwa na Mungu. Ule Masiya angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu wenye ungebadilisha ulimwengu. (Isaya 9:6, 7; Danieli 2:44) Ule Ufalme utatakasa jina ya Mungu kwa kuonyesha wazi uongo wa Shetani na kumuharibu Shetani na kuondoa mambo yote ya mubaya yenye ameleta. (Zaburi 46:9; 72:12-16; Isaya 25:8; 33:24) Ile njo mambo yenye unaombaka itimie wakati unakuwaka unasali Ufalme wa Mungu ukuye.
“Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.”
Ile maneno ya Yesu inaonyesha kama mapenzi ya Mungu itafanyika ku dunia sawa vile iko inafanyika mbinguni, kwenye Mungu anaishi. Hakuna kitu yenye imezuia mapenzi ya Mungu kufanyika mbinguni; kule Mwana wa Mungu alipigana vita na Shetani na malaika zake, na akawatupa ku dunia. (Ufunuo 12:9-12) Hii ombi ya tatu, sawa vile tu maombi mbili ya kwanza, inatusaidia tujue jambo ya maana zaidi yenye tunapaswa kutanguliza mu sala, ni kusema, mapenzi ya Mungu, hapana, mapenzi yetu. Ni wakati tu mapenzi ya Mungu inafanyika njo viumbe vyake vyote vinaweza kuwa mu hali ya muzuri. Njo maana, hata Yesu, mwanadamu mukamilifu, aliambiaka Baba yake hivi: “Lakini, mapenzi yako ndiyo yatendeke, hapana yangu.”—Luka 22:42.
“Utupatie leo mukate wetu kwa ajili ya siku hii.”
Kisha, Yesu alionyesha kama haiko mubaya kumuambia Mungu mahitaji yetu. Kufanya vile kunatukumbusha kama Yehova njo “anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” (Matendo 17:25) Biblia inaonyesha kama yeye ni Baba mwenye upendo mwenye anafurahiaka kupatia watoto wake mambo yenye wako nayo lazima. Sawa vile baba muzuri, Yehova hawezi kutupatia mambo yenye haitatusaidia.
“Utusamehe madeni yetu.”
Uko kabisa na deni ya Mungu? Uko na lazima ya kusamehewa ile deni? Watu wengi leo hawaelewe zambi ni nini na hawajue uzito wa zambi. Lakini Biblia inafundisha kama magumu yetu inatokana na zambi, juu zambi njo imeletea wanadamu kifo. Tulizaliwa mu zambi, njo maana tunafanyaka makosa kila mara. Na juu tukuwe na tumaini ya kuishi milele, inaomba Mungu atusamehe. (Waroma 3:23; 5:12; 6:23) Biblia inatutuliza sana wakati inasema: “Wewe, Ee Yehova, uko mwema na uko tayari kusamehe.”—Zaburi 86:5.
“Utukomboe na ule muovu.”
Unajua ni juu ya nini uko na lazima kabisa ya kulindwa na Mungu? Wengi wanakatala kuamini kama “ule muovu,” Shetani, iko kabisa. Lakini Yesu alifundisha kama Shetani iko kabisa, na hata alimuita “mutawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31; 16:11) Shetani amedanganya watu wengi mu hii dunia yenye iko anatawala. Na anapenda sana akudanganye juu usikuwe rafiki ya Baba yako, Yehova. (1 Petro 5:8) Lakini, Yehova iko na nguvu sana kuliko Shetani na anapenda sana kulinda wale wenye wanamupenda.
Hii mambo kidogo yenye tumezungumuzia juu ya sala yenye Yesu alifundisha, haionyeshe mambo yote yenye tunaweza kutia mu sala. Andiko ya 1 Yohana 5:14 inatuambia hivi juu ya Mungu: “Hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.” Njo maana, usiwaze kama mambo yenye iko inakuhangaisha haiko ya maana na kama haupaswe kuiambia Mungu.—1 Petro 5:7.
Sasa, tunapaswa kusali wakati gani na wapi? Ile nayo ni mambo yenye inaomba kufikiria.
-
-
5 Tunapaswa Kusali Wakati Gani na Wapi?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
5 Tunapaswa Kusali Wakati Gani na Wapi?
BILA shaka, umeona kama dini za mingi zinahangaikia sana kujenga nyumba za sala na zinapanga wakati wa kusali. Lakini, Biblia inasema kama tunapaswa kusali tu wakati fulani na fasi fulani?
Biblia inaonyesha kama kuko wakati mbalimbali wenye tunapaswa kusali. Kwa mufano, mbele ya kula na wafuasi wake, Yesu alisali juu ya kumushukuru Mungu. (Luka 22:17) Na wakati wanafunzi wake walikutana juu ya ibada, walikuwa wanasali. Kwa kufanya vile, waliendelesha desturi yenye Wayahudi walikuwa wanafuata tangu zamani mu masinagogi yao na mu hekalu kule Yerusalemu. Mungu alipenda hekalu ikuwe “nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”—Marko 11:17.
Wakati watumishi wa Mungu wanakutana na kusali pamoja, Mungu anasikilizaka maombi yao. Kama wanasali na wako na nia moja na wanafanya vile kupatana na kanuni za Biblia, Mungu anafurahia sala yao. Sala yao inaweza hata kumuchochea Mungu afanye jambo yenye pengine hangefanya. (Waebrania 13:18, 19) Mashahidi wa Yehova wanakuwaka wanasali ku mikutano yao yote. Tunakutia moyo uende ku Jumba ya Ufalme ya karibu na kwako juu ujisikilie vile wanakuwaka wanasali.
Lakini, Biblia haiseme kama tunapaswa kusali wakati fulani tu ao fasi fulani tu. Mu Biblia muko habari za watumishi wa Mungu wenye walisali wakati na fasi mbalimbali. Yesu alisema: “Wakati unasali, ingia ndani ya chumba chako cha peke yako, na kisha kufunga mulango, sali kwa Baba yako mwenye kuwa mahali pa siri. Halafu Baba yako mwenye kuona akiwa mahali pa siri atakulipa.”—Matayo 6:6.
Tunaweza kusali wakati yoyote na fasi yoyote
Mualiko muzuri sana, hauone vile? Unaweza kusali kwa Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi mu ulimwengu wote wakati yoyote, na unaweza kufanya vile na uko peke yako na kuwa hakika kama atakusikiliza. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini mara mingi Yesu alikuwa anapenda kusali na iko yeye peke! Wakati fulani alisali kwa Mungu usiku muzima. Bila shaka alifanya vile juu ya kumuomba Mungu amuongoze mbele ya kukamata uamuzi fulani wa maana sana.—Luka 6:12, 13.
Wanaume na wanamuke mbalimbali wenye Biblia inazungumuzia walikuwa wanasali mbele ya kukamata maamuzi ya maana sana ao wakati walikuwa na magumu ya nguvu. Wakati fulani walisali kwa sauti na wakati ingine walisali kimyakimya. Walisali wakati walikuwa na watu wengine na hata wakati walikuwa peke yao. Ya maana ni vile tu walisali. Hata Mungu anaambia watumishi wake hivi: “Musali bila kuacha.” (1 Watesalonike 5:17) Iko tayari kusikiliza wale wenye wanafanya mapenzi yake, hata wasali mara ngapi. Ile inaonyesha kama Yehova anapenda kabisa tukuwe tunasali kwake.
Leo, watu wengi hawaamini kama sala inaweza kuwasaidia. Pengine na weye unajiulizaka: ‘Sala inaweza kabisa kunisaidia?’
-
-
6 Sala Inaweza Kutusaidia?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
6 Sala Inaweza Kutusaidia?
SALA inaweza kutusaidia? Jibu ni ndiyo, juu Biblia inaonyesha kama sala za watumishi waaminifu wa Mungu zilikuwa zinawasaidia. (Luka 22:40; Yakobo 5:13) Sala inaweza kabisa kutusaidia tukuwe na urafiki muzuri na Mungu, na tujisikie muzuri. Namna gani?
Kwa mufano, tunapendaka kusema aksanti wakati tunapokea zawadi. Juu ya nini ni muzuri kufanya vile? Juu wakati tunaonyesha shukrani yetu, tunajisikia kuwa wenye shukrani zaidi. Ni vile pia wakati tunazungumuza na Mungu. Juu ya nini tunasema vile? Tuone mifano fulani.
Sala za shukrani. Wakati tunamushukuru Baba yetu juu ya mambo ya muzuri yenye iko anatufanyia, tunaonyesha kama tuko tunaona ile mambo. Ile inafanya tukuwe wenye shukrani zaidi, wenye furaha zaidi, na tukuwe na mawazo ya muzuri zaidi.—Wafilipi 4:6.
Kwa mufano: Yesu alimushukuru Baba yake, juu alisikiliza na kujibia sala zake.—Yohana 11:41.
Sala za kuomba musamaha. Wakati tunamuomba Mungu musamaha, zamiri yetu inatumika muzuri zaidi, tunaonyesha kama tunahuzunika juu ya mambo yenye tulifanya, na tunatambua kama ni jambo ya maana kumutii Mungu. Pia, ile inatusaidia tusijilaumu kupita kiasi.
Kwa mufano: Daudi alisali juu ya kuonyesha kama anatubu na kama anahuzunikia mambo yenye alifanya.—Zaburi 51.
Sala za kuomba muongozo na hekima. Kumuomba Yehova atuongoze na atupatie hekima juu tukamate maamuzi ya muzuri, kunatusaidia tukuwe wanyenyekevu kabisa. Tena, kunatusaidia tukumbuke kama kuko mambo yenye hatuna uwezo wa kufanya. Na tena, kunatusaidia tumutumainie zaidi Baba yetu wa mbinguni.—Mezali 3:5, 6.
Kwa mufano: Sulemani alimuomba Mungu amuongoze na amupatie hekima juu aweze kuongoza muzuri Israeli.—1 Wafalme 3:5-12.
Sala za wakati wa magumu. Kama tunamuambia Mungu magumu yetu, tutajisikia kuwa wenye kutulia na tutamutumainia zaidi kuliko kujitumainia siye wenyewe.—Zaburi 62:8.
Kwa mufano: Mufalme Asa alisali wakati adui mubaya alikuwa anapenda kumushambulia.—2 Mambo ya Nyakati 14:11.
Sala kwa ajili ya watu wenye wako na lazima ya musaada. Sala za vile zinatusaidiaka tusikuwe watu wenye kujifikiria wenyewe tu, tukuwe wenye huruma zaidi, na wenye kujitia pa fasi ya wengine.
Kwa mufano: Yesu alisali kwa ajili ya wanafunzi wake.—Yohana 17:9-17.
Sala za kumusifu Mungu. Wakati tunamusifu Yehova juu ya mambo ya ajabu yenye amefanya na juu ya sifa zake, tunamuheshimia zaidi na tunamuona kuwa wa maana zaidi. Tena, sala za vile zinatusaidia tumukaribie zaidi Mungu wetu na Baba yetu.
Kwa mufano: Daudi alimusifu Mungu sana, juu ya vitu vyenye aliumba.—Zaburi 8.
Faida ingine yenye tunapata wakati tunasali ni “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” (Wafilipi 4:7) Haiko mwepesi kupata amani ya akili mu hii dunia yenye inayala muvurugo. Kukuwa na amani ya akili kunaweza hata kutusaidia tukuwe na afya ya muzuri. (Mezali 14:30) Lakini tunaweza kupata amani ya akili kwa nguvu yetu wenyewe? Ao kuko jambo ingine ya maana yenye tunapaswa kufanya?
Sala iko na faida mingi; inatusaidia tujisikie muzuri, na zaidi sana inatusaidia tukuwe na urafiki muzuri na Mungu
-
-
7 Mungu Anasikilizaka na Kujibia Sala?Munara wa Mulinzi—2010 | Mwezi wa 10 1
-
-
7 Mungu Anasikilizaka na Kujibia Sala?
WATU wengi wanapendaka sana kujua kama Mungu anasikilizaka na kujibia sala zetu. Biblia inaonyesha kama hata leo Yehova anasikilizaka sala. Lakini juu Mungu asikilize sala zetu, kuko mambo yenye tunapaswa kufanya.
Yesu alilaumu viongozi wa dini wa wakati wake. Aliwaita wanafiki juu walikuwa wanasali juu tu ya kuonyesha kama wao njo wazuri. Alisema kama “watapata zawabu yao kikamili.” Alipenda kusema kama watapata tu jambo yenye walihangaikia sana, ni kusema, kuonekana na watu; lakini hawangepata jambo yenye walikuwa nayo lazima, ni kusema, kusikiwa na Mungu. (Matayo 6:5) Vilevile, leo watu wengi wanasali kupatana na mapenzi yao, hapana mapenzi ya Mungu. Juu hawafuate kanuni za Biblia zenye tumezungumuzia, Mungu hasikilize sala zao.
Halafu weye? Mungu atasikiliza na kujibia sala zako? Haiko rangi yako ya ngozi, inchi yako, ao cheo yako njo itafanya Mungu asikilize na kujibia sala zako. Biblia inatuhakikishia hivi: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.” (Matendo 10:34, 35) Na weye uko unafanya vile? Kumuogopa Mungu maana yake kumuheshimia sana na kuepuka kufanya mambo yenye haimufurahishe. Kufanya mambo yenye kuwa sawa ni kufuata mawazo ya Mungu, hapana mawazo yetu ao mawazo ya wanadamu wenzetu. Unapenda kabisa Mungu asikilize sala zako? Biblia inaonyesha namna unaweza kusali juu Mungu asikilize sala zako.a
Watu wengi wanapenda Mungu ajibie sala yao kwa kuwafanyia muujiza. Lakini hata mu wakati wa Biblia, Mungu hakukuwaka nafanya miujiza kila wakati. Wakati fulani, kisha muujiza moja kufanyika, kulikuwa kunapita mamia ya miaka njo muujiza ingine inafanyika. Zaidi ya ile, Biblia inaonyesha kama kipindi ya miujiza ilimalizika kisha wakati wa mitume. (1 Wakorinto 13:8-10) Ni kusema Mungu hajibiake sala leo? Hapana! Tuone mambo fulani yenye anafanyaka juu ya kujibia sala leo.
Mungu anapatiaka watu hekima. Hekima yote ya kweli inatoka njo kwa Yehova. Anafurahiaka kuipatia wale wenye wanapenda awaongoze na wenye wanajikaza kufuata kanuni zake mu maisha yao.—Yakobo 1:5.
Mungu anatupatiaka roho yake takatifu. Roho takatifu ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kutimiza mambo mbalimbali. Hakuna nguvu yenye inaipita. Inaweza kutusaidia tuvumilie magumu. Inatusaidia tukuwe na amani wakati tuko na mahangaiko. Inaweza kutusaidia tukuwe na sifa za muzuri. (Wagalatia 5:22, 23) Yesu aliambiaka wanafunzi wake kama Mungu anapatiaka watu roho takatifu, haiimake mutu.—Luka 11:13.
Mungu anasaidiaka wale wenye kumutafuta kwa bidii wamujue. (Matendo 17:26, 27) Mu dunia yote kuko watu wenye wako wanatafuta kabisa kweli. Wanapenda kujua jina ya Mungu, mambo yenye anapanga kufanya juu ya dunia na wanadamu, na mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake. (Yakobo 4:8) Mara mingi Mashahidi wa Yehova wanakutanaka na watu wa vile na wanafurahiaka kuwafasiria ile mambo kwa kutumia Biblia.
Na weye uko unamutafuta Mungu? Ile njo sababu yenye ilifanya ukamate hii gazeti? Pengine hii gazeti njo jibu ya sala yako.
a Kama unapenda kupata habari zaidi juu ya namna ya kusali na mambo yenye unaweza kufanya juu Mungu asikilize sala yako, ona sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, yenye ilitolewa na Mashahidi wa Yehova.
-