Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Sababu Gani Usome Biblia?
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2017 | No. 1
    • Mwanamuke mumoja anakamata Biblia katika nafasi ya kutilia vitabu

      HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

      Sababu Gani Usome Biblia?

      “Niliwaza kama Biblia itakuwa nguvu sana kuelewa.”—Jovy

      “Niliwaza kama Biblia ingenichokesha.”—Queennie

      “Wakati niliangalia ukubwa wa Biblia, nilipoteza kabisa hamu ya kuisoma.”—Ezekiel

      Umekwisha kufikiria kusoma Biblia lakini ukaacha kuisoma kwa sababu ya mawazo kama hayo yenye kutajwa hapo juu? Watu wengi wanaona kama kusoma Biblia ni jambo lenye kuogopesha. Lakini, unaweza kufanya nini ikiwa unaambiwa kama Biblia inaweza kukusaidia ukuwe na maisha yenye furaha zaidi? Na unaweza kufanya nini ikiwa unatambua kama kuko mambo fulani yenye unaweza kufanya ili ufurahie kusoma Biblia? Unaweza kuwa tayari kuchunguza faida zenye Biblia inaweza kukuletea?

      Ona maelezo kidogo tu ya watu wenye walipata faida wakati walianza kusoma Biblia.

      Ezekiel, mwenye kuwa na miaka 20 hivi, anasema: “Zamani, nilikuwa kama mutu mwenye kutembeza motokari bila kujua nafasi kwenye anaenda. Lakini kusoma Biblia kumenisaidia kuwa na maisha yenye kusudi. Biblia iko na mashauri yenye ninaweza kutumikisha kila siku.”

      Frieda, mwenye kuwa pia na miaka 20 hivi, anasema: “Nilikuwa ninatenda haraka bila kufikiri. Lakini kwa sababu ya kusoma Biblia, nimejifunza kujizuia. Hilo limefanya ikuwe mwepesi zaidi kwangu kusikilizana na wengine, kwa hiyo, sasa niko na marafiki wengi zaidi.”

      Eunice, mwanamuke mumoja mwenye kuwa na miaka 50 hivi, anasema mambo haya juu ya Biblia: “Inanisaidia kuwa mutu muzuri zaidi na kubadilisha tabia za mubaya.”

      Kama vile wasomaji hao na mamilioni ya watu wengine wamejionea, kusoma Biblia kunaweza kukusaidia kuishi maisha yenye furaha zaidi. (Isaya 48:17, 18) Kunaweza pia kukusaidia katika mambo mengi kama vile (1) kukamata maamuzi ya muzuri, (2) kupata marafiki wa kweli, (3) kupambana na mahangaiko ya akili, na (4) zaidi sana, kujifunza ukweli juu ya Mungu. Mashauri yenye kuwa katika Biblia yanatoka kwa Mungu, kwa hiyo, hauwezi hata siku moja kupata matokeo mabaya ikiwa unayafuata. Mungu hatoake mashauri ya mubaya.

      Jambo la maana ni kuanza kusoma. Ni mambo gani yanaweza kufanya ikuwe mwepesi kwako kuanza kusoma Biblia na kufurahia usomaji wako?

  • Namna Gani Ninaweza Kuanza Kusoma Biblia?
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2017 | No. 1
    • HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

      Namna Gani Ninaweza Kuanza Kusoma Biblia?

      Mwanamuke mumoja anasali mbele ya kusoma Biblia

      Ni mambo gani yanaweza kukusaidia ufurahie kusoma Biblia na upate faida wakati unaisoma? Ona mambo tano yenye yamesaidia watu wengi.

      Utafute mahali pa muzuri. Jaribu kutafuta mahali pa kimya. Ujikaze kuepuka mambo yenye yanaweza kukufanya usikazie akili yako juu ya mambo unasoma. Mwangaza muzuri na hewa ya muzuri vinaweza kukusaidia kupata faida wakati unasoma.

      Ukuwe na mawazo ya muzuri. Kwa sababu Biblia inatoka kwa Baba yetu wa mbinguni, utapata faida zaidi ikiwa unakuwa kama mutoto mwenye iko tayari kujifunza kutoka kwa muzazi wake mwenye upendo. Kama uko na mawazo yoyote ya mubaya juu ya Biblia, jaribu kuyatia pembeni ili Mungu akufundishe.​—Zaburi 25:4.

      Usali mbele ya kuanza kusoma. Biblia iko na mawazo ya Mungu, ndiyo sababu tuko na lazima ya musaada wake ili kuielewa. Mungu anaahidi kuwapatia “roho takatifu wale wanaomwomba.” (Luka 11:13) Roho takatifu inaweza kukusaidia kuelewa mawazo ya Mungu. Kisha wakati fulani, itafungua akili yako ili uweze kuelewa “hata mambo mazito ya Mungu.”—1 Wakorintho 2:10.

      Ujikaze kuelewa mambo unasoma. Hapana kusoma juu tu ya kumaliza Biblia. Fikiria sana juu ya mambo yenye unasoma. Kwa mufano, unaweza kujiuliza hivi wakati unasoma habari juu ya mutu fulani: ‘Mutu huyu alionyesha sifa gani? Namna gani ninaweza kutumia habari hii katika maisha yangu?’

      Upange mambo yenye unapenda kutimiza. Ili upate faida wakati unasoma Biblia, ujikaze kujifunza jambo fulani lenye litakusaidia kabisa katika maisha yako. Unaweza kupanga kutimiza mambo kama haya: ‘Ninataka kujifunza mengi zaidi juu ya Mungu.’ ‘Ninapenda kuwa mutu muzuri zaidi, bibi ao bwana muzuri zaidi.’ Kisha chagua Maandiko ya Biblia yenye yatakusaidia kutimiza mambo hayo.a

      Mambo hayo tano yatakusaidia kuanza kusoma Biblia. Lakini unaweza kufanya nini ili ufurahie zaidi kusoma Biblia? Habari yenye kufuata inaonyesha mambo fulani ya kufanya.

      a Kama haujue muzuri ni Maandiko gani ya Biblia yenye yatakusaidia zaidi kufikia mambo yenye unapenda kutimiza, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia.

      Ili Kupata Faida Wakati Unasoma:

      • Tumia muda wa kutosha, na usikuwe haraka

      • Uzame katika mambo yenye unasoma, na ujikaze kuyaona katika akili yako

      • Jaribu kuona namna maandiko yanapatana

      • Tafuta somo ao fundisho fulani katika mambo yenye unasoma

  • Unaweza Kufanya Nini ili Ufurahie Kusoma Biblia?
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2017 | No. 1
    • Mwanamuke mumoja anatumia vifaa vya kusaidia kujifunza Biblia wakati anasoma Biblia

      HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

      Unaweza Kufanya Nini ili Ufurahie Kusoma Biblia?

      Usomaji wako wa Biblia utakuwa wa namna gani? Wa kuchokesha? Ao wa kufurahisha? Jibu linategemea mambo yenye unafanya. Tuone mambo yenye unaweza kufanya ili upendezwe zaidi na usomaji wako na kuufurahia zaidi.

      Utumie Biblia yenye kutumainika, na yenye kuwa na maneno yenye kueleweka. Ikiwa unasoma habari yenye kuwa na maneno mengi yenye kuwa nguvu kuelewa ao maneno ya zamani yenye haujue, pengine hautafurahia usomaji wako. Kwa hiyo, tafuta Biblia yenye kutumia maneno mepesi kuelewa yenye yatagusa moyo wako. Lakini, inapaswa pia kuwa yenye kutafsiriwa kwa uangalifu na kwa uaminifu.a

      Utumie teknolojia ya sasa. Leo, kuko Biblia zenye kuchapishwa kwenye karatasi (papiers) lakini kuko pia Biblia za kielektroniki. Unaweza kusoma tafsiri fulani kwenye Internete ao kuzichukua na kuziweka kwenye ordinatere, tablete, ao telefone yako kwa ajili ya kusoma. Tafsiri fulani ziko na sehemu zenye kukusaidia kuchunguza bila kukawia maandiko mengine yenye kupatana na andiko lenye unasoma, ao sehemu zenye kukusaidia kulinganisha tafsiri mbalimbali. Ikiwa unapenda kusikiliza kuliko kusoma, kuko pia Biblia yenye kurekodiwa ao ya kusikiliza tu. Watu wengi wanapenda kusikiliza usomaji wa Biblia wakati wako katika chombo fulani cha kusafirisha watu kama vile motokari, wakati wanafua manguo, ao wakati wanafanya mambo mengine yenye yanawaruhusu kusikiliza. Unaweza kuchagua namna moja yenye kukufaa.

      Utumie vifaa vya kusaidia kujifunza Biblia. Vifaa vya kusaidia kujifunza Biblia vinaweza kukusaidia upate faida zaidi wakati unasoma. Kuko karte za maeneo yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Karte hizo zitakusaidia kujua nafasi kwenye eneo fulani lilipatikana, na utaelewa muzuri habari hiyo. Habari fulani kama vile habari zenye kuwa katika gazeti hili ao katika sehemu “Mafundisho ya Biblia” yenye kuwa kwenye adresi yetu ya Internete jw.org, zinaweza kukusaidia kuelewa maana ya maandiko fulani ya Biblia.

      Utumie njia mbalimbali. Ikiwa kusoma Biblia kuanzia mwanzo mupaka mwisho kunaonekana kuwa jambo lenye kuogopesha, jaribu kuchochea hamu yako kwa kuanza na sehemu fulani yenye kukupendeza. Kama unapenda kujifunza juu ya watu wenye kuzungumuziwa katika Biblia, unaweza kujaribu kusoma sehemu za Biblia zenye kuzungumuzia watu hao. Mufano fulani unapatikana katika kisanduku chenye kichwa “Chimba Katika Biblia ili Kujua Watu Wenye Kuzungumuziwa Ndani,” chenye kuwa katika habari hii. Ao pengine unafurahia kusoma Biblia kwa kufuata tungo mbalimbali zenye kuwa ndani ao kwa kufuata mupangilio wa namna mambo yalitokea. Unaweza kujaribu kutumia njia moja kati ya hizo.

      a Watu wengi wameona kama Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya imetafsiriwa kwa uaminifu, ni yenye kutegemeka, na ni mwepesi kabisa kuisoma. Biblia hii yenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova inapatikana katika luga zaidi ya 130. Unaweza kuichukua kwenye adresi yetu ya Internete jw.org ao chukua programu ya JW Library. Ao kama unapenda, Mashahidi wa Yehova wanaweza kuja nyumbani kwako ili kukuletea Biblia yenye kuchapishwa.

      CHIMBA KATIKA BIBLIA ILI KUJUA WATU WENYE KUZUNGUMUZIWA NDANI

      Wanawake fulani waaminifu

      Abigaili

      1 Samweli sura ya 25

      Esta

      Esta sura ya 2-5, 7-9

      Hana

      1 Samweli sura ya 1-2

      Maria

      (mama ya Yesu) Mathayo sura ya 1-2; Luka sura ya 1-2; soma pia Yohana 2:1-12; Matendo 1:12-14; 2:1-4

      Rahabu

      Yoshua sura ya 2, 6; soma pia Waebrania 11:30, 31; Yakobo 2:24-26

      Rebeka

      Mwanzo sura ya 24-27

      Sara

      Mwanzo sura ya 17-18, 20-21, 23; soma pia Waebrania 11:11; 1 Petro 3:1-6

      Wanaume fulani wa pekee

      Abrahamu

      Mwanzo sura ya 11-24; soma pia 25:1-11

      Daudi

      1 Samweli sura ya 16-30; 2 Samweli sura ya 1-24; 1 Wafalme sura ya 1-2

      Yesu

      Injili ya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana

      Musa

      Kutoka sura ya 2-20, 24, 32-34; Hesabu sura ya 11-17, 20, 21, 27, 31; Kumbukumbu la Torati sura ya 34

      Noa

      Mwanzo sura ya 5-9

      Paulo

      Matendo sura ya 7-9, 13-28

      Petro

      Mathayo sura ya 4, 10, 14, 16-17, 26; Matendo sura ya 1-5, 8-12

      VIFAA VYA KUSAIDIA KUJIFUNZA BIBLIA VYENYE KUTOLEWA NA MASHAHIDI WA YEHOVA

      • JW.ORG—Adresi hii ya Internete iko na vifaa vingi vya kusaidia kujifunza Biblia, kama vile sehemu “Majibu ya Maswali ya Biblia.” Iko pia na maagizo juu ya namna ya kuchukua programu ya JW Library

      • “Ona Nchi Nzuri”—Broshua hii iko na karte na picha za maeneo yenye kutajwa katika Biblia

      • Étude Perspicace des Écritures—Ni kitabu chenye buku mbili chenye kuwa na mafasirio juu ya watu, nafasi mbalimbali, na maneno fulani yenye kupatikana katika Biblia

      • “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”—Kitabu hiki cha funzo, kinafasiria ni wakati gani, mahali gani na sababu gani kila kitabu cha Biblia kiliandikwa na kinaonyesha kwa kifupi mambo yenye kuzungumuziwa katika kila kitabu

      • Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?—Kitabu hiki kidogo kinachunguza maandiko kwa uangalifu ili kutoa uhakikisho wenye kuonyesha kama Biblia ni Neno la Mungu lenye kuongozwa na roho yake

      • Biblia—Ina Ujumbe Gani?—Broshua hii yenye kurasa 32 inaonyesha kwa kifupi tungo kubwa ya Biblia nzima

  • Namna Gani Biblia Inaweza Kufanya Maisha Yangu Yakuwe Muzuri Zaidi?
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2017 | No. 1
    • Bibi na bwana wanatumika pamoja katika mafiga

      HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

      Namna Gani Biblia Inaweza Kufanya Maisha Yangu Yakuwe Muzuri Zaidi?

      Biblia iko tofauti na vitabu vingine vyote. Iko na mashauri kutoka kwa Muumbaji wetu. (2 Timotheo 3:16) Ujumbe wa Biblia unaweza kuwa na matokeo makubwa juu yetu. Kwa kweli, Biblia inasema hivi: “Neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu.” (Waebrania 4:12) Biblia iko na nguvu ya kufanya maisha yetu yakuwe ya muzuri zaidi katika njia mbili za maana: kwa kututolea muongozo katika maisha yetu ya kila siku sasa, na kwa kutusaidia kujua Mungu na ahadi zake.—1 Timotheo 4:8; Yakobo 4:8.

      Inaweza kufanya maisha yako yakuwe muzuri zaidi leo. Biblia inaweza kukusaidia katika maisha yako. Inatoa mashauri juu ya mambo yenye kufuata.

      • Uhusiano wetu na wengine. —Waefeso 4:31, 32; 5:22, 25, 28, 33.

      • Afya ya kiakili na ya kimwili. —Zaburi 37:8; Methali 17:22.

      • Kanuni za mwenendo.​—1 Wakorintho 6:9, 10.

      • Namna ya kutimiza mahitaji yetu ya kimwili.​—Methali 10:4; 28:19; Waefeso 4:28.a

      Katika Asia bibi na bwana fulani vijana walifurahia sana faida ya mashauri ya Biblia. Kama bibi na bwana wengi wenye kufunga ndoa hivi karibuni, ilikuwa vigumu kwa kila mumoja wao kuzoea tabia ya mwengine na kuzungumuza waziwazi. Lakini walianza kutumikisha mambo yenye walikuwa wanasoma katika Biblia. Walipata matokeo gani? Bwana huyo mwenye kuitwa Vicent, anasema hivi: “Mambo yenye nilisoma katika Biblia yalinisaidia kushugulikia matatizo katika ndoa yetu kwa upendo. Kuishi kulingana na mashauri ya Biblia kumetusaidia kuwa na maisha yenye furaha.” Bibi yake, Annalou, anakubali kwa kusema hivi: “Kusoma mifano mbalimbali katika Biblia kulitusaidia. Sasa ninafurahia ndoa yetu na mambo yenye tumepanga kutimiza katika maisha.”

      Inaweza kukusaidia umujue Mungu. Zaidi ya mambo yenye alisema juu ya ndoa, Vicent anasema tena hivi: “Kupitia kusoma Biblia, ninajisikia kuwa niko karibu zaidi na Yehova kuliko zamani.” Maneno hayo ya Vicent yanakazia jambo la maana sana, ni kusema, Biblia inaweza kukusaidia umujue Mungu. Kwa kusoma Biblia, mashauri ya Mungu yatakuletea faida, lakini utaona pia kwamba unaweza kufikia kumujua kama rafiki. Tena, utaona mambo mbalimbali yenye anafunua juu ya wakati muzuri wenye kuja, wakati huo utaweza kufurahia “uzima ulio wa kweli” ambao utaendelea milele. (1 Timotheo 6:19) Hakuna kitabu kingine chenye kinaweza kukutolea jambo hilo.

      Ikiwa unaanza kusoma Biblia na kuendelea kufanya hivyo, unaweza kupata faida hizo, ni kusema, utakuwa na maisha ya muzuri zaidi leo na utafikia kumujua Mungu. Lakini, wakati unasoma Biblia unaweza kujiuliza maulizo mengi. Na wakati unakuwa na maulizo, kumbuka mufano muzuri wa ofisa Mwethiopia mwenye aliishi kumepita miaka 2000. Alikuwa na maulizo mengi juu ya Biblia. Wakati Filipo alimuuliza ikiwa anaelewa mambo yenye alikuwa anasoma, alimujibu hivi: ‘Kwa kweli, ninawezaje kuelewa, mutu fulani asiponiongoza?’b Kisha alikuwa tayari kukubali musaada kutoka kwa Filipo, mwanafunzi wa Yesu wa wakati wa mitume, mwenye alikuwa tayari mwalimu muzuri wa Biblia. (Matendo 8:30, 31, 34) Wewe pia kama unapenda kujua mambo mengi zaidi juu ya Biblia, tunakualika ujaze fomu yenye kuwa kwenye adresi yetu ya Internete jw.org ao uandikie adresi yenye kuwa katika gazeti hili. Unaweza pia kutafuta Mashahidi wa Yehova wenye kuwa karibu na mahali unaishi ao unaweza kutembelea Jumba la Ufalme lenye kuwa katika eneo lenu. Sababu gani usianze kusoma Biblia leo na kuacha ikusaidie kuwa na maisha ya muzuri zaidi?

      Ikiwa unajiuliza kama unaweza kutumainia kabisa Biblia, tafazali angalia video fupi yenye kichwa, Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? Unaweza kuipata kwa kutumia chombo cha kusoma alama yenye kuwa pembeni ao kwa kufungua jw.org, kwenye kichwa VICHAPO > VIDEO

      a Ili kupata mashauri ya Biblia juu ya mambo mengine, fungua adresi yetu ya Internete, jw.org/sw. Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA.

      b Soma pia habari “Ni Tatizo Ndogo Tu la Kukosa Kuelewa?” yenye kuwa katika gazeti hili.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine