-
“Tafazali, Musikilize Ndoto Hii”Munara wa Mulinzi—2014 | Mwezi wa 8 1
-
-
Bila kuwazia jambo lolote ambalo walikuwa wanapanga juu yake, Yosefu aliwakaribia ndugu zake, akiwazia kwamba watakutana kwa amani. Tofauti na hilo, ndugu zake wakamukamata! Kwa ukali, wakamutosha kanzu yake ya pekee, wakamukokota na kumutupa katika shimo la maji lenye kukauka. Yosefu akaanguka katika shimo hilo! Alipotulia kisha mushituko huo, alijaribu kutoka ndani, lakini hangeweza kutoka ndani kwa uwezo wake mwenyewe. Aliona tu anga wakati sauti ya ndugu zake ilipofifia. Aliwalalamikia, na kuwabembeleza, lakini hawakumuhangaikia. Bila huruma, walikula chakula karibu na shimo hilo. Wakati Reubeni hakuwa hapo, walipanga tena kumuua kijana huyo, lakini Yuda aliwaomba wamuuzishe kwa wafanya-biashara waliokuwa wakipita kuliko kumuua. Muji wa Dothani ulikuwa kwenye barabara ya biashara iliyoenda Misri, na muda mufupi kisha Yuda kusema hivyo kikundi cha Waishmaeli na Wamidiani kikapita. Mbele Reubeni arudi, walitimiza mupango wao. Walimuuzisha ndugu yao kama mutumwa kwa shekeli 20.b—Mwanzo 37:23-28; 42:21.
Yosefu alitetea mambo yaliyokuwa sawa, hata ikiwa ndugu zake walimuchukia
-
-
“Tafazali, Musikilize Ndoto Hii”Munara wa Mulinzi—2014 | Mwezi wa 8 1
-
-
b Hata katika maelezo haya madogo, habari ya Biblia inaonekana kuwa ya kweli. Maandishi ya wakati huo yanaonyesha kwamba bei ya kawaida ya mutumwa huko Misri ilikuwa shekeli 20.
-